Dk Slaa Mbumbumbu - Kamala

Dk Slaa Mbumbumbu - Kamala

Masikini wee, nilimuona alivyokuwa akijing'ata ng'ata sijui na yeye alilazimishwa kwenda kuyasema yale, vitu vingine kama maigizo flani hivi
 
Huyo hana data achaneni naye, angekuwa jimboni anapiga kampeni asingeyasema haya. Ni kwakuwa hana kazi ndo maana anajikeep busy kwa kubwabwaja tu. Hivi alishahama kwenye nyumba ya serikali au anasubiri kufukuzwa?
 
Mfano uliotumia si sahihi.China ni nchi ya kisoshalist na sisi ujamaa umetushinda.HIzo subsidies hatuzitaki,ni mzigo wa bure kwa serikali.
Kila mtu abebe mzigo wake.Slaa wa kwake na Kikwete wa kwake.Mwenye pesa ya kujengea nyumba abebe mfuko wake wa saruji.

Wewe na Kamala chungu chenu kimoja. Subsidy inatumika sana nchi za kibepari. Wakulima wao wanapewa subsidy kubwa sana ndo maana nchi zetu tunawalalamikia kila siku.
 
Kweli kabisa

"Dk Kamala alisema ahadi hiyo ni ya uongo kwani Sh 5,000 ni gharama ya usafirishaji wa mfuko kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa njia ya reli na tani moja ya saruji ya mifuko 20 ni Sh 100,000 hivyo gharama kwa mfuko kuwa Sh 5,000 sawa na bei anayowaahidi Watanzania. Alisema gharama za uzalishaji si chini ya Sh 7,000 kwa mfuko na kabla ya kuongeza gharama nyingine, mfuko wa saruji unapofika Mwanza gharama inakuwa zaidi ya Sh 12,000, hivyo kwa bei yake kuwa kubwa."
Ushabiki kweli mbaya?Hamuoni kitu hapo?
 
"Dk Kamala alisema ahadi hiyo ni ya uongo kwani Sh 5,000 ni gharama ya usafirishaji wa mfuko kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza kwa njia ya reli na tani moja ya saruji ya mifuko 20 ni Sh 100,000 hivyo gharama kwa mfuko kuwa Sh 5,000 sawa na bei anayowaahidi Watanzania. Alisema gharama za uzalishaji si chini ya Sh 7,000 kwa mfuko na kabla ya kuongeza gharama nyingine, mfuko wa saruji unapofika Mwanza gharama inakuwa zaidi ya Sh 12,000, hivyo kwa bei yake kuwa kubwa."
Ushabiki kweli mbaya?Hamuoni kitu hapo?

Takwimu hazidanganyi.Likiwachoma hawataki kuliona.Wanaharakati uchwara waje wampinge Dr.Kamala na tuwaone sasa.
 
Kama Kiwete akiulizwa kwa nini watanzania masikini na hajui kwa nini ndio utegemee nini toka Chama cha Majambazi???

Kikwete knows why we are poor.Do you remember who asked him that question?International journalist right?
Ulitaka aseme watanzania wengi ni wavivu na bado wana ota kuhusu ujamaa?
 
Wewe na Kamala chungu chenu kimoja. Subsidy inatumika sana nchi za kibepari. Wakulima wao wanapewa subsidy kubwa sana ndo maana nchi zetu tunawalalamikia kila siku.

Vipi kuhusu international regulations kwa local subsidies?Hivi unafahamu unachoongea kweli?
 
Kamara hana lolote yeye ndo mbumbumbu, unajua kilichomponza kule Nkenge mpaka akapigwa chini na mwanamama Nshunga?wananchi wa Nkenge walimwambia mheshimiwa nyani wanakula mazo yetu yeye akawajibu kwa kuwaambia kuleni hao nyani ili wapungue,"waganda kyaka"wakamsubiri kwenye kura za maoni wakamfundisha adabu,kesho yake aliondoka na ndege ya Auric air ya saa kumi na mbili yeye,karamagi.Lucy msafiri na Masilingi.hana lolote anataka apewe nafasi ya ubunge wa upendeleo.
 
Si mbumbumbu kwenye uchumi tu, hata katika maisha yake binafsi amejionyesha ni mbumbumbu... Utatembeaje na mke wa mtu bila kujua?
Haya ndugu, kwa kutumia hiihii lugha yako ya majitaka...je na huyo wa KWENU anayetembea na vyangudoa utamwitaje?
 
Huyu kamala siyo mbumbumbu tu bali pia limbukeni alipopata uwazili akawadharau hata wapiga kura wake kiasi kwamba alikuwa akiwaambia kuwa yuko bussy na rais kwa hiyo hawezi kuwasaidia.

Sana sana ni kuwaambia alivyokuwa UK na USA akifikiria hayo ndiyo matatizo ya wananchi wake. Nafikiri kafulia sasa anaangalia kama atapata kacheo angalau aweze kupata mkate wa kila siku, vinginevyo uzee utamwijia hivi karibuni maana hata vyeti vyake kishule havikubaliki.

Lakini si unaona kwa ulimbukeni wa kuwa dharau mpaka wapiga kura wake sasa wameamua kumpiga chini kwenye kura za maoni. Hivi sasa hata future yake mwenyewe imekuwa kitendawili. Mwache aendelee kumsaidia JK kupiga jalamba wakati Dr wetu anaelekea House No.1 Magogoni Street (aka Ikulu🙂
 
Hivi tulitegemea nini sisi watanzania kwa kuongozwa na viongozi wenye mawazo mfu kama ya huyu Dr Kamala? Naililia Tanzania ya Nyerere na Sokoine.

Tatizo ni pale tunapoiacha siasa na uongozi mikononi mwa wapuuzi ama kwa kuogopa misukosuko ya siasa ama kutoona umuhimu, na kuruhusu wasio na upeo walio katika siasa wafanye maamuzi kwa niaba yetu. Ni wakati wa wale wenye uwezo wa kiakili, kimaadili na wazalendo kujitoa muhanga kwa maslahi ya taifa.
 
Huyo hana data achaneni naye, angekuwa jimboni anapiga kampeni asingeyasema haya. Ni kwakuwa hana kazi ndo maana anajikeep busy kwa kubwabwaja tu. Hivi alishahama kwenye nyumba ya serikali au anasubiri kufukuzwa?

"...anajikeep busy kwa kubwabwaja tu." = Upofu + Ushabiki.
 
kweli Kamala ni mjinga na sijui kama anasoma.jamani huyu waziri hajui kwamba EAC ni hiari,leo katiba ya kenya wakenya wamejiondoa katika jumuhia hiyo simply they are not ready prepared.mwambieni atafute gazeti East africa asome,viongozi kama hawa hawafai.

Hilo gazeti la East African umelisoma mwenyewe au umesomewa? Usije kuwa wee ndo mjinga maradufu!
 
Huyu Kamala ana matatizo kichwani. Ushirikiano wa EAC kama hauna faida kwa wananchi hauna maana. Kushusha bei ya saruji inawezekana sana tu, kama wao wameshindwa wawaachie wanaoweza, ebo!:yield:
 
Haya ndugu, kwa kutumia hiihii lugha yako ya majitaka...je na huyo wa KWENU anayetembea na vyangudoa utamwitaje?


Hivi Babu seya aliwekwa ndani kwa ajili ya nani vile?alikula vya mkulu eeehhhh? kesho kutwa mzee lao kwishineyi
 
Huyo hana data achaneni naye, angekuwa jimboni anapiga kampeni asingeyasema haya. Ni kwakuwa hana kazi ndo maana anajikeep busy kwa kubwabwaja tu. Hivi alishahama kwenye nyumba ya serikali au anasubiri kufukuzwa?

"..kubwabwaja.."
Kweli mchambuzi.
 
Hili lenyewe liligushi cheti na halijioni kuwa ni zuzu na mbumbumbu mzungu wa reli! Kweli nyani haoni nonihino lake!
 
Back
Top Bottom