Dk. Slaa: CHADEMA tutashiriki midahalo yote ya Uchaguzi Mkuu

Tumaini Makene

JF-Expert Member
Jan 6, 2012
2,642
6,071
Tutashiriki midahalo yote ya uchaguzi. Kauli iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Chama, Dk. Slaa inaweka wazi namna ambavyo CHADEMA kitashiriki midahalo mbalimbali inayohusu uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba, mwaka huu, malengo yakiwa ni kuwapatia ufahamu wa kutosha wananchi kwa ujumla ili wafanye maamuzi sahihi kutokana na uelewa wa masuala ya uchaguzi, pia kuwafikia wapiga kura wa aina mbalimbali kupitia njia tofauti.

Huku akihoji kama kinachoandaliwa na CEOrt ni kongamano au mdahalo, Katibu Mkuu Dk. Slaa amesisitiza mambo muhimu yanayoweka ushiriki bora wa CHADEMA katika midahalo ya uchaguzi, amesema;

1. CHADEMA inaendeshwa kwa katiba, kanuni na taratibu zake. Hadi sasa taratibu
zetu hazijafikia kupata aspirants wa urais (watangazania).

2. Kama kuna waliopata aspirants,
CHADEMA bado mchakato wetu unaendelea.

3. Midahalo inafanywa kwa msingi wa ilani.
CHADEMA ilani yetu haijafika bado mbele ya vikao vya maamuzi, yaani Baraza Kuu na Mkutano Mkuu. Hivyo tukienda mdahalo tutakuwa tunazungumzia ilani ipi?

"Hivyo tuko tayari kwa midahalo yote baada ya mchakato wetu wa ndani kukamilika."

Kauli ya Dk. Slaa kupitia Gazeti la Mwananchi ambalo lilitaka kujua ushiriki wa CHADEMA kwenye mdahalo wa wagombea urais kama ulivyokuwa umetangazwa kupitia facebook na watu CEOrt.

Makene
 
Dr.Slaa, unasema hauna cha kuongea kwenye mdahalo sababu Chadema bado hawajawa na ilani sasa huko kwenye mikutano yako hivi karibuni ulikuwa unaongea nini na wananchi kuhusu Chadema?

Alikwenda kukagua uandikishaji wa BVR na shughuli za Chama wapi ameripoti amekwenda kutangaza nia. Watanzania tuwe tunaelewa thats why kwenye mitihani Failure zinakuwa nyingi
 
Dr.Slaa, unasema hauna cha kuongea kwenye mdahalo sababu Chadema bado hawajawa na ilani sasa huko kwenye mikutano yako hivi karibuni ulikuwa unaongea nini na wananchi kuhusu Chadema?

Usiwe mbayu mbayu, kuwa Imara. Acha kutanga tanga!

Asante Makene, Asante CHADEMA kwa ufafanuzi au taarifa hiyo.
 
Sound comments, hawa round table kwanza wao sio waandishi wa habari wanataka kuhoji nini,

Tuwaachie ITV & star TV waandaye midahalo professionally
 
Dr.Slaa, unasema hauna cha kuongea kwenye mdahalo sababu Chadema bado hawajawa na ilani sasa huko kwenye mikutano yako hivi karibuni ulikuwa unaongea nini na wananchi kuhusu Chadema?

Ukijibiwa hili swali,kuanzia leo naanza kuvaa magwanda.
 
Niliyasema haya kwenye ule mdahalo wa kwanza wagombea wa vyama vya siasa Tanzania wanaongozwa na ilani ya vyama vyao na mpaka sasa hakuna chama kilichotoa ilani sasa ukimwita mtangaza nia ataongea nini?

Nikasema huyu mzee atulize boli kihelehele chake ndiyo maana ATCL ilikufa sababu hatumii akili kufikiri ana-copy kila kitu bila kutazama mazingira yanaashiria nini?

Hii nchi tabu sana kuna mapungufu kila sehemu, mpaka akili za raia na viongozi wake wana mapungufu.
 
Dr.Slaa, unasema hauna cha kuongea kwenye mdahalo sababu Chadema bado hawajawa na ilani sasa huko kwenye mikutano yako hivi karibuni ulikuwa unaongea nini na wananchi kuhusu Chadema?
alikuwa na mambo matatu; 1) Kuhamasisha watu kujiandikisha ili wapige kura ifikapo mwezi wa October 2) wapige kura ya kuhakikisha ccm inaondoka madarakani 3) elimu ya urai na haki za binadamu. Haya sio mambo ya kuingia kwenye ilani za uchaguzi. Hata ingawa haki za binadamu inawezakuwepo kwenye ilani, lakini ni jambo la wakati wote na muda wote kuliongelea ili watu wajue haki zao
 
Ritz, kwa nini unaanika uj.uha wako hapa? Kama hujui communication ethics unanyamaza. Hivi unafikiri CHADEMA ni level yako ya kubwabwaja bila mpangilio? Anachokiongea kwenye mikutano ndicho unalazimisha akiongee kwenye mdahalo?

Halo, unaudhi hadi kupitiliza. Nenda kasomee mawasiliano kwanza vinginevyo, CHADEMA siyo saizi yako utaishia kudhalilika tu mjukuu wangu.


Dr.Slaa, unasema hauna cha kuongea kwenye mdahalo sababu Chadema bado hawajawa na ilani sasa huko kwenye mikutano yako hivi karibuni ulikuwa unaongea nini na wananchi kuhusu Chadema?
 
Dr.Slaa, unasema hauna cha kuongea kwenye mdahalo sababu Chadema bado hawajawa na ilani sasa huko kwenye mikutano yako hivi karibuni ulikuwa unaongea nini na wananchi kuhusu Chadema?

Slaa hana chakuongea kabisa! Halafu neno aspirant bado gumu..

Slaa ana muogopa sana Zitto sijui kwanini?
 
Back
Top Bottom