Dk. Mwakyembe bado India, aendelea vizuri

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,080
Mwakyembe%2827%29.jpg

Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe.


Madaktari wa Hospitali ya Apollo, nchini India bado wanaendelea na uchunguzi wake dhidi ya ugonjwa unaomkabili Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe.
Akizungumza na NIPASHE jana kwa njia ya simu msemaji wa familia ambaye ni mbunge wa jimbo la Lupa (CCM) mkoani Mbeya, Victor Mwambalaswa, alisema bado haijafahamiki ni lini Dk. Mwakyembe atarudi kwa kuwa bado madaktari wake wanaendelea na uchunguzi.
Alisema kilichokuwa kimebainika kwenye seli nyekundu (Red bone marrow) katika mwili wake, madaktari walitegemea kukuta kimeisha ila walivyomfanyia uchunguzi bado wamekuta tatizo lipo.
Mwambalaswa alisema kutokana na hali hiyo madaktari wake wanaendelea na uchunguzi mpaka hapo watakapokamilisha suala hilo.
Alisema hali ya Dk. Mwakyembe inaendelea vizuri kwani huwa anawasiliana naye mara kwa mara.
Dk. Mwakyembe amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya ngozi, Oktoba 9 mwaka jana, alilazimika kupelekwa katika Hospitali ya Appolo nchini India kwa matibabu zaidi ambapo alirudishwa mwishoni mwa mwaka.
Baada ya kurudishwa hivi karibuni Februari 19 mwaka huu alisafiri tena kuelekea hospitalini huko kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi dhidi ya ugonjwa unaomsumbua.




CHANZO: NIPASHE
 
Mwakyembe%2827%29.jpg

Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe.


Madaktari wa Hospitali ya Apollo, nchini India bado wanaendelea na uchunguzi wake dhidi ya ugonjwa unaomkabili Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe.
Akizungumza na NIPASHE jana kwa njia ya simu msemaji wa familia ambaye ni mbunge wa jimbo la Lupa (CCM) mkoani Mbeya, Victor Mwambalaswa, alisema bado haijafahamiki ni lini Dk. Mwakyembe atarudi kwa kuwa bado madaktari wake wanaendelea na uchunguzi.
Alisema kilichokuwa kimebainika kwenye seli nyekundu (Red bone marrow) katika mwili wake, madaktari walitegemea kukuta kimeisha ila walivyomfanyia uchunguzi bado wamekuta tatizo lipo.
Mwambalaswa alisema kutokana na hali hiyo madaktari wake wanaendelea na uchunguzi mpaka hapo watakapokamilisha suala hilo.
Alisema hali ya Dk. Mwakyembe inaendelea vizuri kwani huwa anawasiliana naye mara kwa mara.
Dk. Mwakyembe amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya ngozi, Oktoba 9 mwaka jana, alilazimika kupelekwa katika Hospitali ya Appolo nchini India kwa matibabu zaidi ambapo alirudishwa mwishoni mwa mwaka.
Baada ya kurudishwa hivi karibuni Februari 19 mwaka huu alisafiri tena kuelekea hospitalini huko kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi dhidi ya ugonjwa unaomsumbua.




CHANZO: NIPASHE

Mungu akuponye Dr kwani Taifa likombioni kukombolewa,njoo tumalizie vipolo vilivyo baki.
 
Wenye haki wangu wataishi kwa imani.Mungu akupe nguvu na afya yako iimalike.wazee wa kyela,mbeya na Tanzania kwa ujumla tunakuombea.
 
pona haraka uje ukawafundishe vijana wetu sheria pale chuo. siasa noma especialy zinapokuwa za majungu majungu, ila tatizo ma v8 chuo hamna labda uende REDET kwanza
 
Pamoja na kuficha baadhi ya mambo kwenye scam ya richmond, tunakupa second chance, tunakuombea upone haraka uje ueleze kwa uwazi kuhusu richmond na kilichokupata,
 
GWS Dr. Utaporudi malizia yale uliomwachia sir God maana yale yalipaswa kusema LIVE pengine kwa haya yote tusingehangaika kumtafuta mchawi
 
Nimesikia kama ameukana ule waraka ulisadikiwa kiandikwa naye kuhusu jinsi alivyowekewa sumu au sikusikia vizuri?
 
Nawashauri Mwakyembe na Mwandosya waandike barua ya kujiuzulu uwaziri ili wapate mda mwingi wa kushughulikia afya zao.Sioni kama ni sahihi kuendelea kushika nyazifa hizo wakiwa katika hali hiyo,N y Mungu awanusuru,Hii ndio Dunia Hujafa Ujaumbika.
 
Hao wazee wa mbeya waliosema watamfata mkuu wa kaya washaenda au?

hawana lolote la maana wamekuja kuona magari tu mjini hapa...waje kumuone baba mwanaasha kwani yeye ndo daktari anayemtibu mwakyembe? sula la ugonjwa ni siri ya daktari na mgonjwa mwenyewe...sasa hawa wanataka kulifanya suala la mwakyembe kuumwa ukurutu wa milele ni tatizo la kitaifa...hebu watupishe bana tuna issues nyingi sasa za ku deal nazo...kwanza madokta wanataka kugoma hebu watupe muda tushugulikie issue ya madokta
 
Dr. unateseka na yale uliyoacha kuyamwaga pale Dom ili kukinusuru chama chako na serikali yako. Siku ukiyaweka hadharani na moyo wako utaoina. Hata kama mwili utakufa
 
hawana lolote la maana wamekuja kuona magari tu mjini hapa...waje kumuone baba mwanaasha kwani yeye ndo daktari anayemtibu mwakyembe? sula la ugonjwa ni siri ya daktari na mgonjwa mwenyewe...sasa hawa wanataka kulifanya suala la mwakyembe kuumwa ukurutu wa milele ni tatizo la kitaifa...hebu watupishe bana tuna issues nyingi sasa za ku deal nazo...kwanza madokta wanataka kugoma hebu watupe muda tushugulikie issue ya madokta

Mkuu usipuuze hivyo wazee wananafasi yao pia, huwezi jua mambo ya mila.....unajua nini kilichomsababishia mstuko hadi akapelekwa Ujerumani mzee wa nywele nyeupe wa Monduli?.... Heshimu tu wazee, ya duniani mengi huwezi yamaliza!
 
Back
Top Bottom