amoneyazan
JF-Expert Member
- Jan 10, 2013
- 698
- 473
Haahaaa hapo umetumia busara kiongoziHahahaha jamaa anataka kunihamishia msala. Haya mambo mkuu wangu yanahitaji ushahidi usio na shaka ndo uweze kusema huyu ni mzinzi au laa.
Sasa mimi huyo Malasusa wala hata sijawahi kumwona hata kwenye picha, nna mamlaka gani ya kumtuhumu au kumtetea mwenue masuala ya uzinzi?
Hahahahahaa.....Haahaaa hapo umetumia busara kiongozi
Maana kwenye hizi maada ukitelezaa tu utajikutaa umegeuzwa mbuzi wa kafara
Tuhumaa zote zinakugeukiaa
Tena we ndo unageuka source kuu ya habari unaanza kuulizwa, wengine wanakufata PM wanahoji "ilikuajee mkuu tupe mkandaa"[emoji28] [emoji109]
Sasa jiulize, Malasusa ni Mkaskazini?Lakini mbona wale wapendwa wa Kaskazini ndo wengi na wanatengenezewa michongo ya kupeana kazi? Ama wa-Pwani wanatumika?
Many people dies spiritually out of these... I dont know the exact number but it could be lot more than you might think...How many died in this one?[emoji15]
[emoji23] [emoji23] [emoji23]Majungu, fitna,chuki, husuda dhidi ya Mnyakyusa Malasusa. Wenyewe Wazaramo wanataka Dayosisi yao
Mm mwenyw hii story n ngeni kwanguHuyo mchungaji leita ndo nani? Na wanahusiana vipi na malasusa?
This story is new to me? What happened?
Jambo usilolijua ni usiku wa giza, nilifanikiwa kusoma tuhuma hizi kwenye moja ya gazeti na kwa bahati nzuri nimejaribu kufuatilia kidogo ili kujua nini hasa kinatokea katika Dayosisi ya mashariki ya Pwani. Kwa watu ambao hawaijui hii dayosisi ya mashariki na pwani sio rahisi kuelewa haya mambo, wengi watachukulia mambo haya kwa uzito usio stahili.Taarifa ndani ya dayosisi hiyo zinasema, katibu mkuu wa DMP, Godfrey Nkini, amenukuliwa akimueleza Mchungaji Leita kuwa utendaji wa Askofu Malasusa wa kuhudumu ofisini umezorota tangu kuibuka kwa tuhuma hizo.
Akamtaka kwenda likizo ili kurejesha amani ya kiongozi mkuu wa dayosisi.
Haya yameibuka baada ya jitihada za kutaka wachungaji kutetea Askofu wao kushindikana. Hoja ya kutaka kanisa limfanyie maombi Askofu Malasusa iliwasilishwa kikaoni na msaidizi wa Askofu.
“Baada ya mpango huu kukwama, katibu mkuu wa dayosisi alimwita Mchungaji Leita ofisini mwake na kumtaka achukue likizo ya muda mrefu ili asionekane machoni mwa waumini na wageni wengine.
“Mchungaji Leita alitoa masharti mawili: Kwanza, yuko tayari kuchukua likizo endapo katibu mkuu atampa barua rasmi ikieleza sababu ya hatua hiyo na pili endapo mtuhumiwa mwenzake, Askofu Malasusa, naye atapewa likizo.”
Amesema, “katibu mkuu Nkini ameshindwa kutekeleza masharti hayo, jambo ambalo limesababisha Mchungaji Leita kuendelea kubaki ofisini.”
Haya yanaibuka, siku mbili baada ya Asime Modern Mwakilima,muumini wa dayosisi ya Mashariki na Pwani akisema, anatafakari upya uumini wake katika kanisa hilo.
Alisema, “suala la imani ni langu mwenyewe na Mungu. Lakini katika hili, naona mkuu wetu amepoteza sifa ya kuhudumu.
Badala ya kusimamia ukweli,kanisa limeamua kukandamiza haki.”
Mchungaji mmoja wa kike aliyezungumza kwa sharti la kutotajwa gazetini ameutuhumu uongozi wa dayosisi hiyo kukumbatia alichoita, “mfumo dume.”
Alisema, “hapa kuna mfumo dume. Ndiyo unaotaka kutumika kumuonea huyu mama na kumlinda Askofu aliyetuhumiwa naye. Haya ni makosa makubwa sana.
Hata Bwana Yesu alipoletewa mwanamke aliyefumaniwa akizini, alimwuliza yuko wapi mtuhumiwa mwenzako?”
Taarifa zinasema, mkuu mpya wa KKKT, Askofu Fredrick Shoo amemuita Mchungaji Leita kwa lengo la kujadiliana naye juu ya suala hilo; lakini amegoma hadi mahojiano hayo yamshirikishe Askofu Malasusa.
“Hii inaonyesha mchungaji huyu wa kike alivyonusa mbinu chafu za kutaka kutelekezwa na kanisa ili kumuokoa Askofu Malasusa,” ameeleza mtoa taarifa ndani ya kanisa hilo.
MwanaHALISI Online ilipokea nakala ya waraka wa kichungaji uliosambazwa kwa watu mbalimbali, ukiwataka waumini wa kanisa hilo kuchukua hatua za haraka kuikoa dayosisi yao iliyotumbukia katika mgogoro wa kuongozwa na anayemuita,“kiongozi aliyepungukiwa na uadilifu.”
Nmepitia msg zoteeeeTusihukumu tusije tukahukumiwa?je sisi tunaonyoosha vidole vyetu ni wasafi kiasi gani? ? ?
Huenda kuna kitu unajua hebu tuthibitishie kwamba anaandamwa sababu alikwenda kwenye Sherehe zakuapishwa Magufuli......Nitarudihuyu askofu malasuxa ameanza kuandamwa na mwanaHALISI mbona ataipatapata nakwambia, akamwulize muumini wake lowaxa. kubenea akikuandama na gazeti lake huchomoki asee!!, yote haya yanatokana na huyu askofu kuhudhuria sherehe za kuapishwa rais JPM wakati msimamo wa kanisa lake ilikuwa ni kususia tukio lile. pole sana askofu.
Alimuungaje mkonoMalasusa kosa lake ni kumuunga mkono Magufuli kipindi cha kampeni.
Unajua kuna majitu humu hayajui chanzo cha hizo Kashfa yaokoteza Maneno eti...sababu alimuunga mkono Magufuli...Tatizo DMP imekuwa mahari pamavuno kwa Viongozi walafi....wengi wao wamegeuza Kanisa kama kampuni...ndio sababu ya hayo yoteMkuu, dayosisi ya Mashariki na Pwani ni pwani kwelikweli. Kuna majungu pale, fitna pale, kuna mijitu imetajirika Kwa kuingiza vitu Kwa jina la kanisa kumbe ni Mali zao binafsi wanakwepa kodi, watu hao wana fedha za kutosha kununua vichambio kama mwanahalisi. Usishtuke mkuu
Ukiondoa sababu ya kuhudhuria sherehe (ambayo si inayotajwa na MwanaHalisi), hoja kuhusu tuhuma zake nako ni kuandamwa?huyu askofu malasuxa ameanza kuandamwa na mwanaHALISI mbona ataipatapata nakwambia, akamwulize muumini wake lowaxa. kubenea akikuandama na gazeti lake huchomoki asee!!, yote haya yanatokana na huyu askofu kuhudhuria sherehe za kuapishwa rais JPM wakati msimamo wa kanisa lake ilikuwa ni kususia tukio lile. pole sana askofu.
Alikuzini nini....!! Waswahili wanasema aiSIFUYE MVUA imNYESHEAHuyu malasusa Ni mzinzi kuliko kile kizazi cha sodoma na gomora
Nikumpa Shetani Ushindi...!!Wangejiuzulu tu wote wawili.
Ndugu ukienda Kanisani kwa kumfuata MTU utaumia sana Roho...Kama hii stori ni ya kweli basi huyu mchungaji noma. Analiwa na kondoo wake afu anamgaia na bosi wake.
Mi ndo maana kwenda kanisani imekuwa ngumu sana. Makanisani kumejaa full unafiki, ufedhuli, uzinzi nk.... tena ukifanywa na viongozi na makasisi.
Kuna watu hawajui wanachofata huko maKanisani...ndio maana Ibada ikiendelea yeye anakoroma kwa Usingizi sasa MTU kama huyo kumaliza makanisa hakuna Tatizo!Kama imani yako haijajengeka katika Yesu kristo jiwe kuu la pembeni, bali umeijenga kwa kiongozi flani au mtu flani basi nikupe pole saaana bi dada
Kwa mwendo huoo utahamaa sanaaa makanisa , hata huko AIC nako utahamaa , utakako hamia nako utahamaa
Utaendaaaa mpka utafikia kanisani kwetu nako utahaamaaa tena