Dk. Kilahama aibiwa, aomba msaada JF

Dk. Kilahama aibiwa, aomba msaada JF

Manyerere Jackton

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
2,438
Reaction score
4,461
Wadau, hapa chini nakuleteeni kilio cha Dk. Kilahama. Ameniomba niwasilishe ujumbe huu kwa wadau akiamini JF ipo kila mahali. Tafadhali usomeni na tuone namna ya kumsaidia.

Kupitia huduma ya mitandao ya kijamii, Dk. Felician B. Kilahama, anayo masikitiko makubwa sana kutokana na kitendo cha baadhi ya watu wasiokuwa na nia njema walisababisha apoteze begi lake lililokuwa na vifaa vyake muhimu. Hali hii ilitokea tarehe 06 Julai 2014 akiwa njiani kutoka Iringa na ilikuwa kati ya Morogoro na Picha ya Ndege-Kibaha ilipodhihirika kuwa hilo begi ambalo lilikuwa na vifaa muhimu likawa halipo sehemu ambako alilihifadhi.

Vifaa hivyo ni pamoja na laptop, camera (canon ndogo), kisanduku cha miwani ya kusomea kikiwa na miwani pamoja na modems za internet mbili- Voda na Zantel; funguo za nyumbani, simu yenye njia mbili - Tigo na Zantel, flash discs kadhaa, nyaraka muhimu na dawa kadhaa za kisukari na BP. Hali ya kuibiwa kwa begi hiyo ilijulikana baada ya kufika Picha ya Ndege, Kibaha na kijana mmoja akawa anateremka hapo na akasema ameibiwa computer yake. Ndipo Dk. Kilahama aliposhtuka na akaangalia sehemu aliyokuwa amehifadhia begi lake ikawa halioni na kutafuta kila sehemu bila ya mafanikio. Hivyo kuashiria kuwa limeibwa.

Pia Msafiri mwingine naye akaona sehemu alipoweka computer yake haipo! Kikawa ni kilio. Inasemekana wanaume wawili waliteremkia sehemu ya Mlandizi na kwa kuwa ilikuwa saa tatu usiku na ilikuwa giza; lakini baadhi ya abiria waliowaona wakiteremka na mabegi yanayodhaniwa kuwa ni hayo yaliyotea.

Kwa hali hiyo wakazi wa Mlandizi wanaombwa kuwa wadadisi kwa watu watakaoonekana wakiuza vitu kama hivyo. Waliochukua vitu hivyo wanefanya kitendo cha kinyama na ni dhahiri kuwa hawatatumia vitu hivyo, bali wataviuza. Wakazi wa Mlandizi na maeneo mengineyo wanatahadharishwa kuwa waangalifu katika hili. Watakaoona dalili zozote za picha au nyaraka zinazomhusu Dk. Kilahama watoe taarifa katika Kituo cha Polisi au kwa viongozi wa eneo husika.

Pia ikitokea kuwa nyaraka au dawa zimetupwa mahali tafadhali peleka kwa viongozi au kituo cha polisi au piga simu 0783 007400 au 0756 007400. Tafadhali sana tushirikiane katika hili na tufichue wahalifu wa aina hii.

NB. Dk. Kilahama ni Mkurugenzi wa Misitu mstaafu katika Wizara ya Maliasili na Utalii
 
Nampa pole sana, kuibiwa usawa huu inachosha sana
 
Naendelea Kushangaa na ninaomba mnisaidie kushangaa nyie wenzangu, mtu mwenye hadhi ya ukurugenzi kisha doctor anapanda gari la abiria ya tsh 35,000?
tatizo nini hajapewa gari? hajapewa dereva?
 
Naendelea Kushangaa na ninaomba mnisaidie kushangaa nyie wenzangu,
mtu mwenye hadhi ya ukurugenzi kisha doctor anapanda gari la abiria ya tsh 35,000?
tatizo nini hajapewa gari? hajapewa dereva?


Nani amekwambia alikuwa amepanda gari la abiria, hata km ni la abiria kuna tatizo gani? we ni mshamba kweli.
 
Naendelea Kushangaa na ninaomba mnisaidie kushangaa nyie wenzangu,
mtu mwenye hadhi ya ukurugenzi kisha doctor anapanda gari la abiria ya tsh 35,000?
tatizo nini hajapewa gari? hajapewa dereva?
Huwa namuona kwenye tv mara nyingi akikagua hifadhi za ardhi!duuh hawa wezi hawa balaa
 
Naendelea Kushangaa na ninaomba mnisaidie kushangaa nyie wenzangu,
mtu mwenye hadhi ya ukurugenzi kisha doctor anapanda gari la abiria ya tsh 35,000?
tatizo nini hajapewa gari? hajapewa dereva?

Soma vizuri ni Mkurugenzi Mstaafu...........

NB. Dk. Kilahama ni Mkurugenzi wa Misitu mstaafu katika Wizara ya Maliasili na Utalii
 
Dah now I can connect the dots!kumbe mapovu yote kuhusu ufisadi wa Waziri vs waandamizi wizara ya maliasili kumbe una interest?
Tanzania nakupenda kwa moyo wote
 
Nani amekwambia alikuwa amepanda gari la abiria, hata km ni la abiria kuna tatizo gani? we ni mshamba kweli.

Unaponiita Mshamba hua una maanisha nini? kwamba mimi naishi shamba au sijawahi kufika mjini au una maanisha nini?
Soma Thread vizuri
 
@Manyerere Jackton aripoti pia kwa polisi...hasa kitengo cha cyber crime!!!
 
Ni mzee ambaye tukiwasiliana mara kwa mara kupitia internet na mara ya mwisho nimemtumia mail yangu ni last weekend hajanijibu kumbe wamemuibia kifaa cha mawasiliano.

Pole sana Dr. Kilahama, mzee wangu mwadilifu na mzalendo wa kweli uliyelitumikia taifa kwa upendo.
Mwenyezi Mungu akujaze roho ya kusamehe!
 
Ni mzee ambaye tumekuwa tukiwasiliana mara kwa mara kupitia internet na mara ya mwisho nimemtumia mail yangu ni last weekend hajanijibu kumbe wamemuibia kifaa cha mawasiliano!

Pole sana Dr. Kilahama, mzee wangu mwadilifu na mzalendo wa kweli uliyelitumikia taifa kwa upendo.

Mwenyezi Mungu akujaze roho ya kusamehe!
 
Na wewe soma vizuri haya maneno nilioandika kwa herufi kubwa ni MKURUGENZI mstaaf wa MISITU NA MALI ASILI na UTALII halafu niambie.

Umeyasema wapi hayo?

user-online.png
SPANISH CP
Today 11:54
#5
JF Senior Expert MemberArray


Join Date : 5th April 2014
Posts : 390
Rep Power : 392
Likes Received166
Likes Given61


[h=2]
icon1.png
Re: Dk. Kilahama aibiwa, aomba msaada JF[/h]
Naendelea Kushangaa na ninaomba mnisaidie kushangaa nyie wenzangu,
mtu mwenye hadhi ya ukurugenzi kisha doctor anapanda gari la abiria ya tsh 35,000?
tatizo nini hajapewa gari? hajapewa dereva?​


 
Naendelea Kushangaa na ninaomba mnisaidie kushangaa nyie wenzangu,
mtu mwenye hadhi ya ukurugenzi kisha doctor anapanda gari la abiria ya tsh 35,000?
tatizo nini hajapewa gari? hajapewa dereva?

Alishastaafu ukurugenzi ndivyo nijuavyo
 
Unaponiita Mshamba hua una maanisha nini? kwamba mimi naishi shamba au sijawahi kufika mjini au una maanisha nini?
Soma Thread vizuri

Eti anamaanisha wewe ni wa mashambani na kama ni wa muyini basi umekuja jana!
 
Back
Top Bottom