Dk Hoseah akiri Takukuru ‘kunuka’ rushwa

Dk Hoseah akiri Takukuru ‘kunuka’ rushwa

...labda na Kikwete atakubali hivi karibuni kwamba Ikulu yake inanuka rushwa na inaongoza kwa kupokea rushwa kuliko taasisi yoyote ile nchini.

Zile fedha za ESCROW zilizogaiwa kupitia Benki ya Stanbic zinathibitisha hili!!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ungefanya ustaarabu na ujasiri mkubwa kama ungekubali umeshindwa kazi na kuamua kustaafu ili utoe nafasi mtu mwingine achukue nafasi yako.
 
Wakati mwingine tunatafuta majibu mepesi kwenye maswali magumu,dk hosea tangu kaingia Takukuru ndo tumeanza kuskia kazi ya Takukuru tumeona watu wakipelekwa mahakamani na wengine kuchukuliwa hatua,kwa Tanzania ya leo kusema Rushwa haiwezi kuwepo ni ndoto maana Rushwa ilikuwepo tangu enzi za mwalimu,kwa hiyo Rushwa ni jukumu letu sote sio la Takukuru wala la Serikali maana watoa Rushwa si ndo sisi
 
Taasisi ya kuzuia rushwa inazuiaje wakati inapokea. Mkono mmoja unapokea mwingine unanazuia! Very contradicting.
Ilipaswa iwe ishachunguza na kuchukua hatua kwa sababu kazi yake kubwa ni kuchunguza ili iweze kuzuia. sasa iweje isubiri utafiti halafu iutumie badala ya kutumia taaluma yake yenyewe ya uchunguzi!
 
Kazi kubwa ya jeshi ni kulinda mipka ya nchi dhidi ya maadui kutoka nje. hii haina maana kuwa jeshi halihusiki na maasi ya ndani. kwa hiyo Takukuru isiangalie nje ya Takukuru pekee bali hata ndani ya Taasisi yenyewe.
 
Rushwa ipo hata kabla ya utawala wa Mwalimu,miaka ya mwanzo ya uhuru kuna waziri alihusishwa na tuhuma za Rushwa na hatua za kisheria zilifatwa. Japo rushwa ilikuwepo lakini vitendo vya rushwa vilifanywa kwa kificho sana na vyombo vya usalama vilikuwa vinafanya kazi yake ipasavyo. Leo rushwa ni waziwazi bila kificho kwa hizi tunazoita rushwa ndogo ndogo kila panapotolewa huduma ya umma ni lazima utatoa rushwa! huko juu ndiyo balaa kunanuka rushwa mpaka unapata kichefuchefu kwa hiyo harufu!Tunacholia ni rushwa kufanywa BAYANA bila hofu na kibaya zaidi wanaotakiwa kupambana na rushwa ndiyo wanatuhumiwa kuwa wala rushwa!!
 
Anasahau yeye kama Kiongozi wa TAKUKURU ndiye aliyeshindwa kusimamia taasisi hiyo vizuri na hivyo chini ya uongozi wake rushwa imekithiri ndani ya taasisi hiyo na Tanzania nzima. Kwa kifupi uongozi wa kupambana na rushwa nchini umemshinda.

Anayo mapungufu yake lakini anafanya kazi ktk mazingira ya aina gani? Wewe ungepewa nafasi yake ktk mazingira haya ungefanyaje?
 
Usitake kubadili huu uzi kama anafanya kazi katika mazingira ambayo hajaridhika nayo kuna kitu kinaitwa kujiuzulu kutokana na mazingira magumu ya kufanya kazi badala ya kuendelea kupokea mshahara na marupurupu makubwa huku taasisi ikishindwa vibaya sana na matokeo yake rushwa kuzidi kukithiri nchini.

Anayo mapungufu yake lakini anafanya kazi ktk mazingira ya aina gani? Wewe ungepewa nafasi yake ktk mazingira haya ungefanyaje?
 
Usitake kubadili huu uzi kama anafanya kazi katika mazingira ambayo hajaridhika nayo kuna kitu kinaitwa kujiuzulu kutokana na mazingira magumu ya kufanya kazi badala ya kuendelea kupokea mshahara na marupurupu makubwa huku taasisi ikishindwa vibaya sana na matokeo yake rushwa kuzidi kukithiri nchini.


Huu ndio unafiki tunao waafrika wengi....

Kuwajibika kwetu ni mwiko ila kulaumu na kuzoza tu....

Huyo Hosea amewahi anikwa na wikileaks. akiwa analalamika jinsi JK alivyo kikwazo ktk kupambana na Rushwa but still anakalia office mpaka Leo....
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nakumbuka Mkuu jinsi Hosea alivyokana kwamba yeye alihusika na yaliyoandikwa kwenye wikileaks ambayo yalikuwa ni ukweli mtupu. Wengi tulidhani Kikwete angemtimua au angemwambia ajiuzulu kama ilivyo kawaida yake lakini hadi leo hii bado kakalia kiti. Shinikizo la Kinana na Nape kwa Kikwete labda lingeweza kumng'oa lakini ndiyo hivyo tena awamu ya DHAIFU aliyechoka ndio inaelekea ukingoni.

Huu ndio unafiki tunao waafrika wengi....

Kuwajibika kwetu ni mwiko ila kulaumu na kuzoza tu....

Huyo Hosea amewahi anikwa na wikileaks. akiwa analalamika jinsi JK alivyo kikwazo ktk kupambana na Rushwa but still anakalia office mpaka Leo....
 
Nakumbuka Mkuu jinsi Hosea alivyokana kwamba yeye alihusika na yaliyoandikwa kwenye wikileaks ambayo yalikuwa ni ukweli mtupu. Wengi tulidhani Kikwete angemtimua au angemwambia ajiuzulu kama ilivyo kawaida yake lakini hadi leo hii bado kakalia kiti. Shinikizo la Kinana na Nape kwa Kikwete labda lingeweza kumng'oa lakini ndiyo hivyo tena awamu ya DHAIFU aliyechoka ndio inaelekea ukingoni.
BAK Jk hana ubavu wa kumtambua Hosea hata iweje.! Kwakuwa ni 'mshirika muhimu' 'kibiashara', biashara zile ambazo hazina hasara hazikatwi kodi, na faida zake ni nono.!
Ipo syndicate ambayo ina link ya moja kwa moja na mamlaka za juu kabisa ikijumuisha watu muhimu na maarufu wakiwemo wafanyabiashara wa kubwa. !dili zote chafu na za kawaida zina baraka na mkono wa hii syndicate
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Sasa kama takukuru ya TZ inapokea rushwa hebu tuazime ya Kenya itusaidie kukamata takukuru wa TZ
 
Back
Top Bottom