Dk Hoseah akiri Takukuru ‘kunuka’ rushwa

Dk Hoseah akiri Takukuru ‘kunuka’ rushwa

...labda na Kikwete atakubali hivi karibuni kwamba Ikulu yake inanuka rushwa na inaongoza kwa kupokea rushwa kuliko taasisi yoyote ile nchini.

Serikali nzima inanuka rushwa. Mfumo mzima JK aliorithi toka kwa Mkapa na kuuendeleza na kuweka wake ndo shida ilipoanzia. Sasa hivi watu wanakimbilia serikalini kwasababu nje ya mapato yao halali kuna rushwa na upigaji kibao.

Takukuru ni sehemu ya serikali ya JK kwahiyo usitegemee miujiza ya wao kufanya vyema. Takukuru na system nzima haisafishiki hadi uingie utawala mwingine mpya na kusafisha uozo wote wa ccm.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Naelewa nachozungumza kwa kuwa tatizo si la TAKUKURU kama TAKUKURU kwani tumeunda taasisi kwa maana ya kupambana na kuzuia rushwa lakini wahusika ambao ni serikali wanachukulia poa tu kuwa support hawa jamaa kiasi kwamba mtu kiongozi kabisa anatamka hadharani 'hawa mafisadi wana nguvu na mtandao mkubwa ni kwenda nao kwa tahadhari', unategemea nini sasa hapa kwa Hosea na timu yake. Wangepewa menu na nguvu na kuweka siasa pembeni wangefanya kazi lakini hawapewi

Kama Polisi wameshindwa kuwa "imara" sasa hivi kwa hiyo watakuwa "imara" wakipewa kazi ya kupambana na rushwa?
 
...labda na Kikwete atakubali hivi karibuni kwamba Ikulu yake inanuka rushwa na inaongoza kwa kupokea rushwa kuliko taasisi yoyote ile nchini.

Wala haitaji kukiri maana hilo lipo wazi. Haiwezekani kila mahali kukawa na rushwa - polisi, mahakama, serikalini (kwenye wizara mbali mbali), TAKUKURU nk lakini Ikulu ikawa safi.

Siamini kama subordinate anaweza kuwa mla rushwa kama bosi wake si mla rushwa! Huu usemi wa Hosea maana yake nini?

Dk Hoseah alisema ili kupambana na rushwa lazima Serikali iwe na uongozi bora na imara
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Na mzito mmoja wa PCCB aliyepewa sh millioni 30 na Benki Kuu ya Tanzania wakati wa kashfa ya EPA je? Muda umefika wa kuonyesha alivyopokea na aliyempelekea. Hii ndo itakuwa funga kazi ya rushwa nchini.
wekeni ushahidi hapa tuwamalize mafisi hawa. tumewakabidhi bucha wakati meno yao yamechongoka wanakula hadi mifupa.
 
Taasisi ya
Kuchunguza na
Kusaidia/kusafisha/kuficha
Rushwa kubwa zilizo na maslahi ya wakubwa au zenye maslahi ya kisiasa.

Maono: Usalama na ulinzi wa serikali na wezi walio madarakani dhidi ya rungu la mahakama.
Mkakati: Kuchunguza, kubaini, kuficha taarifa, kuzuia uchukuliawaji wa hatua au inapobidi hatua zichukuliwe na kesi zisimamiwe kwa lengo la kuuhadaa uma lakini matokeo ya kesi hizo hata kama zitahusisha adhabu ndogo ya mwaka mmoja au miwili au kuuambia umma hela ilioibiwa imerudishwa(kiini macho) ili mwishowe ufalme bado usimame na mavuno yawe mengi.


Frankly speaking, mpaka leo sijajua hiki kitengo kilianzishwa kwa madhumuni gani....... serious!
 
Kama Polisi wameshindwa kuwa "imara" sasa hivi kwa hiyo watakuwa "imara" wakipewa kazi ya kupambana na rushwa?
Tatizo unasoma kwa jicho la seriousness sana mkuu, nimesema hao polisi wenyewe yao yamewashinda bora waongezewe na hili itaonekana wana mambo mengi kuliko kutengeneza kitu maalumu kwa ajili ya rushwa alafu linapokuja suala la kushitaki kunakuwa na muingiliano kati ya DPP na PCCB na mwisho wa siku watu wanaachiwa, natambua uwepo wao ila concern yangu wapewe meno na waachiwe wafanye kazi vingenevyo hakuna maana ya kuwa nao,
 
Hivi Edward Hosea ni mfalme ndani ya PCCB? Tangu niifahamu hii idara huwa namsikia tu huyu mzee???

Rais afanye uteuzi upya maana inaoneka Hosea idara imemshinda kabisa.
 
Anasahau yeye kama Kiongozi wa TAKUKURU ndiye aliyeshindwa kusimamia taasisi hiyo vizuri na hivyo chini ya uongozi wake rushwa imekithiri ndani ya taasisi hiyo na Tanzania nzima. Kwa kifupi uongozi wa kupambana na rushwa nchini umemshinda.

Mkuu BAK na bado jamaa anakula mshahara wa nguvu wakati taasisi ya kupambana na rushwa inapokea rushwa naona tuuiite taasisi ya kupokea na kutakatisha rushwa
 
Nakubaliana na yote uliyoandika Bulldog.

Serikali nzima inanuka rushwa. Mfumo mzima JK aliorithi toka kwa Mkapa na kuuendeleza na kuweka wake ndo shida ilipoanzia. Sasa hivi watu wanakimbilia serikalini kwasababu nje ya mapato yao halali kuna rushwa na upigaji kibao.

Takukuru ni sehemu ya serikali ya JK kwahiyo usitegemee miujiza ya wao kufanya vyema. Takukuru na system nzima haisafishiki hadi uingie utawala mwingine mpya na kusafisha uozo wote wa ccm.
 
Last edited by a moderator:
Kilianzishwa kwa usanii tu ili kutuzuga Watanzania kwamba Serikali inafanya juhudi kupambana na rushwa wakati hali halisi haiko hivyo. Pamoja na TAKUKURU kupewa bajeti kubwa sana kila mwaka lakini rushwa ndiyo inazidi kuota mizizi nchini tena hadi ya Ikulu ambapo mabilioni ya peza za walipa kodi yanagawiwa kama njugu na Rais wa nchi akiwa kimya kabisa.

Frankly speaking, mpaka leo sijajua hiki kitengo kilianzishwa kwa madhumuni gani....... serious!
 
Serikali ina pretend kulipa Mishahara ... wafanyakazi wanajitafutia vyanzo vya kujazia vipato vyao... Hali hiii itaendelea hadi CCM ing'olewe madarakani ...
 
Mkuu Sibonike hapo kwenye rangi maana yake uongozi wa nchi ni mbovu na dhaifu hii ni kuanzia ndani ya Ikulu, Baraza la Mawaziri na taasisi nyingine zote nchini ikiwemo TAKUKURU ambazo zinapaswa kuwemo katika hii vita ya kupambana na rushwa. Vita ambayo uongozi huu mbovu nchini umeshindwa vibaya sana.

Wala haitaji kukiri maana hilo lipo wazi. Haiwezekani kila mahali kukawa na rushwa - polisi, mahakama, serikalini (kwenye wizara mbali mbali), TAKUKURU nk lakini Ikulu ikawa safi.

Siamini kama subordinate anaweza kuwa mla rushwa kama bosi wake si mla rushwa! Huu usemi wa Hosea maana yake nini?

Dk Hoseah alisema ili kupambana na rushwa lazima Serikali iwe na uongozi bora na imara
 
Last edited by a moderator:
dk+hosea.jpg

Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini, Dk Edward Hosea.
Na Anthony Kayanda, Mwananchi

Posted Jumatano,Februari11 2015 saa 17:39 PM
Kwa ufupi
Dk Hoseah alisema wanapokea utafiti huo kama changamoto na watatumia sheria, kanuni na taratibu kuwapa adhabu watumishi watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Kigoma. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imekiri kuwapo kwa baadhi ya watumishi wake wanaojihusisha na vitendo vya kupokea rushwa, hivyo kuchafua sifa ya taasisi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kigoma jana, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hoseah alisema tuhuma zilizotolewa hivi karibuni na taasisi zilizofanya utafiti juu ya masuala ya rushwa nchini, baadhi yake zina ukweli.

Dk Hoseah alisema wanapokea utafiti huo kama changamoto na watatumia sheria, kanuni na taratibu kuwapa adhabu watumishi watakaobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa.

“Takukuru siyo malaika, iwapo nitasema hakuna kabisa rushwa ndani ya taasisi hii nitakuwa ninajidanganya kwani hili tatizo lipo sehemu zote, inawezekana maofisa wasio waadilifu wanapokea rushwa lakini ninawahakikishia kwamba tutachukua hatua kali dhidi ya yeyote atakayebainika,” alisema Dk Hoseah na kuongeza:

“Serikali imefanya jitihada kubwa kuhakikisha Takukuru inaboreshwa, ndiyo maana bado sielewi kwanini kuna baadhi ya watumishi wanalalamikiwa kujihusisha na ulaji rushwa, wanalipwa vizuri na kuna mazingira mazuri ya kufanya kazi. Nitafanya jitihada kuondoa changamoto hizi.”


Pia, alitoa tahadhari kwa wananchi kuwa makini na matapeli wanaojitangaza kwamba wao ni maofisa wa Takukuru, hivyo kuomba rushwa kwa baadhi ya maofisa wa Serikali na watu wengine ambao wanabainika kufanya makosa yanayohusiana na ubadhirifu mbalimbali.

Dk Hoseah alisema ili kupambana na rushwa lazima Serikali iwe na uongozi bora na imara,
ambao utasaidia kuweka mipango thabiti kwa maendeleo ya wananchi, kufanya mambo kwa uwazi, kuwajibika kwa umma, kuwashirikisha watu katika mipango mbalimbali na kusimamia utawala wa kisheria.

CC: Tized, Mr Rocky, Fixed Point, lyinga, NATA, Chakaza, Elly B, Ablessed, MziziMkavu, afrodenzi, Heaven on Earth, Power to the People, Jasusi, Eiyer, idawa, nguruvi, Mentor, Sikonge, Dingswayo, MANI, tpaul, Bramo, Bulesi Bulldog, Sangarara, MTAZAMO, Erythrocyte, Mag3, Mimibaba, zumbemkuu, Crashwise, amkawewe, Idimi, Ogah, Chakaza, mshana jr, JokaKuu, MWALLA, genekai, PRINCE CROWN, Tuko, Shark, lynxeffect22, samaki2011, MoudyBoka adolay, Elli, nyabhingi, Janjaweed, S.N.Jilala, MEANDU, Tabby, Candid Scope, Honolulu, August, dyuteromaikota, BONGOLALA, Gefu, Bigirita, Kozo Okamoto, Daudi Mchambuzi Kill 3





Nilitaraji Dr Hosea kujiuzulu Mara moja baada ya ripoti ile inayoonyesha pccb/Takukuru kuwa miongoni mwa taasisi za serikali zinazoongoza kwa rushwa, lakini kwa serikali hii ya chama chawala hiyo ni ndoto isiyo na tija
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nilitaraji Dr Hosea kujiuzulu Mara moja baada ya ripoti ile inayoonyesha pccb/Takukuru kuwa miongoni mwa taasisi za serikali zinazoongoza kwa rushwa, lakini kwa serikali hii ya chama chawala hiyo ni ndoto isiyo na tija

Wewe MGOMVI sana ,mara ya mwisho kupelekwa polisi lini?Ajiuzulu halafu kile kiyoyozi kwenye ile VX yake apigwe nani?
 
Nawahakikishieni huyu Dkt anachukia sana jinsi mambo yanavyoenda hapanchini. Mfumo wa sheria umewekewa kigingi na watawala
 
Back
Top Bottom