Dizasta Vina a.k.a Maradona


Ngoma. yenyewe kuchi kuchi nai nai[emoji28][emoji2305]
 
Namshukuru sana Rapcha kwa kujibu Diss ya Dizasta
Maana hakuna nachosubiri hapa zaid ya Best friend-2

Game is on [emoji91][emoji91]

Dizasta kupitia hii dis naona watu wengi wameanza kumfatilia hope atapata airtime aende mainstream
Dizasta vina hawezi kwenda mainstream eti kwa sababu amedisiana na Rapcha, na nimeskia pia Rapcha kampiga na hiyo Line kwamba kwakuwa kamtaja basi inabidi Dizasta atusue lasivyo atampiga makosi ya Ass

Dizasta vina ataingia mainstream pale atakapoamua mwenyewe kubadirika, kulegeza uandishi wake na kuanza kutumia beat laini bila kusahau kuwa karibu na baadhi ya watu Fulani kwenye industry

Dizasta vina ni msanii ambae yeye mwenyewe haitaji kwenda mainstream na hili ashalitolea sana ufafanuzi, hataki kwa sababu itamlazimu abadirike kwenye vitu vingi sana

Anasema itamtaka abadirike vile anavofikilia, abadirike vile anavyoandika, abadirike life style na vitu vingi ambayo yeye anaona hayupo teyari

Anachosema yeye ni kwamba msanii akiwa underground stream ndio sehemu ambayo anakuwa huru kuandika chochote kile ambacho anaona ni sawa, nayeye anapenda kuendelea kuwa huru maana anaamini mashabiki wake wanastahili kilicho Bora

Mwisho wa siku anachotaka yeye ni mashabiki kumfata yeye alipo na sio kuwafata mashabiki walipo, na actually with time hii kitu itakuja kutokea, maana anajitangaza kutokana na ubora wa kazi zake na sio skendo,Kiki wala Diss track

Kwa Dizasta vina ndie "Most Influencer underground Stream Rapper" na pia ndie msanii peke kutoka underground stream ambae anafatiliwa zaidi kuliko ata baadhi ya wasanii ambao wapo mainstream
 
[emoji1666][emoji1666]
 
[emoji1666][emoji1666]
 
[emoji91][emoji91][emoji1666][emoji1666]
 
Hii hajib Dizasta
 
We jamaaaa unamfatilia sana Dizasta[emoji1666][emoji1666][emoji1666]
 
We jamaaaa unamfatilia sana Dizasta[emoji1666][emoji1666][emoji1666]
Ndio mkuu, jamaa nimewahi kuwa karibu nae kipindi tunaskuli university akiwa na harakati zake za hip-hop ndomana napenda kumfatilia...! Jamaa ana misimamo yake anayoijua yeye mwenyewe tangu kitambo

Jamaa alikuwa atheism tangu miaka ya 2015 hadi kupelekea kulichana KANISA, wakati huo sie wengine ata hatujui chochote kuhusu atheists
 
Misimamo ya Tamaduni kama wanaharakati lakini kwa nini huwa wana bifu na mainstream artists

Mfano Nick mbishi huwa naona live ana stress za kuwa na jina kubwa kwa fans wake ambao hawawezi mpa hiyo hela anayostahili ndio maana anakuwa bitter kwa wasanii ambao wanapewa hiyo spotlight ambayo haitamani kishingo upande

By the way, mimi sio pro fan wa Hip pop lakini napenda nyimbo zenye punchlines za kufikirisha na sio za kunogesha flow,

Hiphop ya kumbadilisha mtu mindset

Ukiwa na list yenye wimbo kama sihitaji marafiki ya Fid au misemo ya FA, nibariki nazo nikazisikiliize mkuu🙏🏽🙏🏽
 
Kumbe mwamba umepiga nae university mzee

Chuo gani alisoma na course gani

Ilo la atheist nililigundua kupitia mashairi yake

Jamaa kuwa comfortable na u-underground nilimskia mwenyew akifafanua kupitia interview

Jamaa linajikubali sana kitu ambacho ni kizuri lakini kuna gharama anailipia

Mi ni shabiki yake naweza sema namba moja ( He's my favourite rapper) na of course ni mwanafalsafa mwenzake japo tunapishana kimtazamo at point still he's the best to me

I wish him all the best nna uhakika anayayajua na kuyasema na hela anazozipata kupitia hiki anachokifanya havilingani, ni kama industry inamdhulum

I wish to meet him in person one day
 
"achieving greatness" inajadiliwa lini?View attachment 2478737
King of "Bilingual"

"Wametutosa tunaofoka ndani ya focus makini"

Nimepita chap chap na hizi ndio zime catch brain kwa haraka

1: Achieving Greatness ft TK
2: In my Heart ft TK Nendeze
3: Acha Niende ft Rossie
4: Skia skiza Skika ft Triple S
5: Uchizi ft Rossie
6: vitendo dhidi ya maneno
 

Amebukuka hapo kwa hayati waziri Sokoine alipiga Course moja ya kudeal na "Majani (chakula) na wadudu wasambazao magonjwa kwenye Mifugo" code

Fanya ukutane nae mkuu kama nawewe ni mwanafalsafa ili mbadirishane mawazo/mitazamo maana kiuhalisia Dizasta vina sio mtu wa kawaida kama watu wanavyomchukulia

Nadhani kupitia mashairi yake unaweza kuhisi jamaa ni mtu wa namna gani, na kwenye mashairi yake jamaa anajitahidi sana kurahisisha ili kila mtu aweze kuelewa ila bado kuna watu hatumuelewi

kwenye kuandika ni kama vile anatumia ¼ tu ya uwezo wa Akili yake, waliokaa karibu na Edgar na sio "Dizasta vina" ndio wanaweza kuthibitisha haya nayosema

Anyway, let's enjoy his work brother.
 
Mbishi waga ana shida zake tu binafsi mkuu, pride huwa inamzidi, Mbishi ndie naweza kusema msanii ambae yupo obsessed na kwenda mainstream kuliko msanii yoyote yule tangu yupo Tamaduni hadi kikosi kazi

Kuna wasanii wengine wao wameridhika na sehemu walipo na huwezi kuskia wanapiga kelele kama za Mbishi, mwangalie One,Songa

Alafu kuna hawa P mawenge,Sterio hawa wapo kote kote, wanafight kuingia mainstream at the same hawaichukii underground stream kwahiyo wao hawana stress ambazo anazo nick

Kinachomponza nick ni "kujijua kama anajua" hii kitu inataka kumfanya aamini kuna baadhi ya wasanii wanapata ambacho hawastahili kukipata kwa sababu tu amewazidi uwezo kwenye vitu vingi

Sasa tukija kwenye issue ya Dizasta vina, yeye kwake ni tofauti sana, HATAKI kwenda mainstream either iwe kwa bahati mbaya au makusudi ndomana huwezi kuskia anakuwa na bifu na wasanii waliopo mainstream, hatqki kwa sababu itamnyima Uhuru alionao katika kuandika

Huwezi ukawa Mainstream alafu ukaimba wimbo kama KANISA itakuwa ni suicide katika career yako huwezi ukawa Mainstream ukaandika wimbo kama "A CONFESSION OF MAD PHILOSOPHER" ukiwa mainstream ni ngumu kuandika wimbo kama "SHAHIDI" huwezi kuandika "KIFO"

Skiliza album kama Super Nyota alafu skiliza The verteller ndio utaona tofauti ilipo, sio kwamba Young killer hawezi kufanya anachofanya Dizasta vina, hapana bali Hana hizo Gut's, sasa hicho ndio Dizasta hataki kukipoteza pindi atakapokuwa mainstream Kwa sababu mainstream wana code zao

Dizasta vina hawezi kuandika eti "Napotokea hakuna alietoboa labda alietoboa maskio" ili tu watu wafurahi na apate viewer's wengi au streaming za kutosha ila hao watu wasijifunze chochote kupitia uandishi wake
 
Nimekusoma mkuu

Nick mbishi akubali kuwa soft kama anaona wengine wanafaidi au awe pure mwanaharakati kama Roma ambaye yupo mainstream lakini akituliza kichwa huwa anakuja na bombs

Kingine huyu dizasta vina na Tamaduni kwa ujumla , hawana excuse kwa nini hawana popularity maana kuna digital platforms sasa itakuwa bora watumie hizo big brains wanaojiona wanazo.. Kuuza muziki wako
 

Roma uzuri wake aliingia moja Kwa moja Mainstream kutumia siasa kipindi ambacho kila mtanzania alikuwa anapenda siasa kwahiyo akajizolea mashabiki wa kila lika na kila jinsia na ndio hao hadi leo hii wanaendelea kustick na jamaa

Actually Nick hawezi kuwa kama Roma maana harakati za nick na Roma ziko tofauti japokuwa zote ni harakati, Roma harakati zake zinamgusa kila mtu kwakuwa anaongelea siasa na kuna nyimbo za Radha tofauti anajumuika na Stamina zinazidi kumbeba, ila harakati za Nick kukugusa ni hadi uchague mwenyewe

Na of course ni kweli mkuu inabidi watumie vizuri digital platform kujiuza ili kupunguza lawama,hasa kwa Nick maana Dizasta hajawahi kulalamika sehemu yoyote ile kuwa anachokipata hakitoshi hadi alete bifu na wasanii walio Mainstream

With time Dizasta anaongeza wigo wa mashabiki kila kukicha hivo ata streaming zake kwenye baadhi ya platform zinapanda taratibu plus na diehard fans wachache alionao ndio wanaosapoti kazi zake kwa kununua basi maisha yanaenda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…