meningitis
JF-Expert Member
- Nov 17, 2010
- 8,349
- 4,674
Huyu ni diwani wa tatu katika jimbo la Arusha mjini kuhamia CCM ndani ya mwaka huu.
Diwani wa chadema ,kata ya Kimandolu,Greyson Ngowi jana aliwaduwaza viongozi wa chadema Jiji la Arusha baada ya kutangaza kujiunga na ccm na kupokelewa na rais Magufuli,lakini kabla ya uamuzi huo aliambatana na Meya wa Arusha ,Calist Lazaro (chadema) na viongozi wengine wa chama hicho, kwenye gari moja kumsikiliza rais wakati akitunuku vyeo askari wa JWTZ.