Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 988
*************
Habari ifuatayo unaweza kuisoma kwenye attachment niliyoweka humu ambayo ni cutting kutoka gazeti la DIRA la leo uk. 02
*************
Mmoja wa madiwani wa CHADEMA wa Jiji la Arusha waliofukuzwa kwa kukaidi amri ya Kamati Kuu, Charles Mpanda (Rasta) amekataa kushiriki vikao vya Baraza la Madiwani na kuchukua posho, licha ya Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa, George Mkuchika, kusisitiza kuwatambua na hivyo kumuumbua.
Rasta alitoa msimamo huo baada ya kudai kuwa alijikuta akiingia katika mzozo na viongozi wake wa juu, baada ya kuponzwa na wenzake bila kujijua.
Alisema kwa sasa ameamua kuachana na siasa na kushughulika zaidi na shughuli zake na kwamba hatoshiriki kwenye vikao vya baraza la madiwani.
Mpanda alisema hawezi kuchukua posho kwani atakuwa hawatendei haki wananchi wakati hawatumikii.
Aidha, diwani huo anajuta kujiingiza kwenye siasa kwani kabla ya hapo alikuwa na maisha mazuri na alikuwa akiheshimiwa na jamii tofauti na sasa ambapo jamii inamchukulia kama adui na msaliti asiyeaminika.
Alisema, awali aliamini nafasi yake ya udiwani ingempatia uzoefu mkubwa ili baadaye ndoto yake ya kuwania katika jimbo mojawapo mkoani Mwanza, lakini sasa amesitisha zoezi hilo baada ya kubaini siasa zinamletea madhara makubwa.
"Kwa sasa sina mpando kabisa na siasa, kwanza zimeniharibia mambo yangu mengi sana na wala sitegemeu kushiriki hata vikao vya madiwani, wameniletea baru kushiriki kikao tarehe 8 mwezi huu, nimewaambia sitakuwepo," alisema Mpanda.
Hata hivyo kumekuwepo taarifa kwamba diwani huyo amekuwa akizomewa mara kwa mara anapopita karibu na mshabiki wa chama hicho na kudiriki hata kutaka kumpiga wakidai msaliti.
Taarifa zimedai kwamba Mpanda alivamiwa na kundi la vijana alipokuwa akipita eneo la Makao Mapya karibu na shina la Ngome Imara la CHADEMA na kuanza kuzongwa na vijana huku baadhi yao wakimtemea kohozi la mate usoni.
"Ni kweli nimekuwa katika wakati mgumu sana kila ninapopita mitaani, hasa sehemu walipo mashabiki wa CHADEMA," alisema
Katika hatua nyingine, katibu mkuu wa CCM mkoa wa Arusha, Mary Chtanda amejikuta kwenye wakati mgumu, kufuatia kundi la vijana kuibuka mara kadhaa na kumzomea hadharani.
Matukio hao yamekuwa yakiibuka Mahakama Kuu ya Arusha, wakati umati wa watu wakitoka ama kuingia kufuatilia kesi ya kupinga matokeo ya ushindi wa mbunge wa Arusha Godbless Lemma.
Katika kesi hiyo iliyoanza kuunguruma hivi karibuni, umati mkubwa wa watu wamekuwa wakifika mahakamani hapo wakiwemo mashabiki wa CCM na CHADEMA, hatua ambayo imempelekea Chatanda kuzomewa wakidai kwamba amechangia CCM kukosa jimbo.
*************
Habari ifuatayo unaweza kuisoma kwenye attachment niliyoweka humu ambayo ni cutting kutoka gazeti la DIRA la leo uk. 02
*************
Mmoja wa madiwani wa CHADEMA wa Jiji la Arusha waliofukuzwa kwa kukaidi amri ya Kamati Kuu, Charles Mpanda (Rasta) amekataa kushiriki vikao vya Baraza la Madiwani na kuchukua posho, licha ya Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa, George Mkuchika, kusisitiza kuwatambua na hivyo kumuumbua.
Rasta alitoa msimamo huo baada ya kudai kuwa alijikuta akiingia katika mzozo na viongozi wake wa juu, baada ya kuponzwa na wenzake bila kujijua.
Alisema kwa sasa ameamua kuachana na siasa na kushughulika zaidi na shughuli zake na kwamba hatoshiriki kwenye vikao vya baraza la madiwani.
Mpanda alisema hawezi kuchukua posho kwani atakuwa hawatendei haki wananchi wakati hawatumikii.
Aidha, diwani huo anajuta kujiingiza kwenye siasa kwani kabla ya hapo alikuwa na maisha mazuri na alikuwa akiheshimiwa na jamii tofauti na sasa ambapo jamii inamchukulia kama adui na msaliti asiyeaminika.
Alisema, awali aliamini nafasi yake ya udiwani ingempatia uzoefu mkubwa ili baadaye ndoto yake ya kuwania katika jimbo mojawapo mkoani Mwanza, lakini sasa amesitisha zoezi hilo baada ya kubaini siasa zinamletea madhara makubwa.
"Kwa sasa sina mpando kabisa na siasa, kwanza zimeniharibia mambo yangu mengi sana na wala sitegemeu kushiriki hata vikao vya madiwani, wameniletea baru kushiriki kikao tarehe 8 mwezi huu, nimewaambia sitakuwepo," alisema Mpanda.
Hata hivyo kumekuwepo taarifa kwamba diwani huyo amekuwa akizomewa mara kwa mara anapopita karibu na mshabiki wa chama hicho na kudiriki hata kutaka kumpiga wakidai msaliti.
Taarifa zimedai kwamba Mpanda alivamiwa na kundi la vijana alipokuwa akipita eneo la Makao Mapya karibu na shina la Ngome Imara la CHADEMA na kuanza kuzongwa na vijana huku baadhi yao wakimtemea kohozi la mate usoni.
"Ni kweli nimekuwa katika wakati mgumu sana kila ninapopita mitaani, hasa sehemu walipo mashabiki wa CHADEMA," alisema
Katika hatua nyingine, katibu mkuu wa CCM mkoa wa Arusha, Mary Chtanda amejikuta kwenye wakati mgumu, kufuatia kundi la vijana kuibuka mara kadhaa na kumzomea hadharani.
Matukio hao yamekuwa yakiibuka Mahakama Kuu ya Arusha, wakati umati wa watu wakitoka ama kuingia kufuatilia kesi ya kupinga matokeo ya ushindi wa mbunge wa Arusha Godbless Lemma.
Katika kesi hiyo iliyoanza kuunguruma hivi karibuni, umati mkubwa wa watu wamekuwa wakifika mahakamani hapo wakiwemo mashabiki wa CCM na CHADEMA, hatua ambayo imempelekea Chatanda kuzomewa wakidai kwamba amechangia CCM kukosa jimbo.
*************