Kata ya Rutoro iko katika Tarafa ya Nshamba, jimbo la Muleba Kasikazini, Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera. Diwani wa kata hiyo Bw. Abubakary Said (CHADEMA) amebambikiziwa kesi ya mauaji ya watu wanne ambao mauaji yao yametokana na mgogoro wa ardhi kati ya Wawekezaji (waliomirikishwa vitaru maarufu kama Blocks) na wananchi.
UFUATAO NI MRORONGO WA TUKIO LENYEWE;
1. Tar.17/04/2013 mlinzi wa Block No.18 linalomilikiwa na Bw. Medard Langile alipeleka mifugo kwenye mashamba ya wananchi na baada ya wananchi kuona wanaharibiwa mali zao kwa asila walimshambulia mlinzi huyo hadi kufariki.
2. Tar.18/04/2013: Walinzi walijikusanya katika eneo hilo hilo la Block No.18 kwa ajiri ya kulipa kisasi. Mlinzi mmoja kati yao alimpiga risasi raia (mwananchi) na kufariki hapo hapo. Wananchi wote walichachamaa na kuanza kuwashambulia walinzi/wafugaji hao. Katika mapambano hayo walinzi/wafugaji watatu walipoteza maisha.
3.Tar.21/04/.2013: RPC kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Kagera alifika katika eneo la tukio akiwa na Wawekezaji wawili. Baadaye aliondoka na Diwani pamoja na mtendaji wa kijiji hicho Bw. Josephat Kyeyamba na kuwaweka ndani katika kituo cha polisi cha wilaya ya Muleba kwa maelezo kuwa wanachochea vurugu na migogoro ya ardhi katika eneo hilo.
4. Tar.22/04/2013: Mtendaji wa kata ya Rutoro Bw. Lameck Byarugaba aliwadhamini Diwani pamoja na mtendaji wa kijiji, na kesi yao ilitajwa tena tar.29/04/2013. Hata hivo walipohudhuria polisi tar.29/04/2013 hawakusomewa mashitaka bali kesi yao ilitajwa tena 6/05/2013
5.Tar.24/04/2013: Mkuu wa Wilaya aliitisha Mkutano kwa ajiri ya kuleta amani katika eneo hilo.Baada ya mkutanoaliondoka na mwenyekiti wa kitongoji Bw.Alcheraus Kahatano na kumweka ndani katika kituo cha polisi Muleba.
6.Tar.27/04/2013: Kwa mara nyingine Mkuu wa wilaya aliitisha mkutano mwingine kwa ajiri ya kuleta amani katika eneo hilo. Alipofika kwa Diwani alikuta kuna Bendera ya CHADEMA ikipepea. Alimuamuru Diwani kuiteremsha bendera hiyo lakini Diwani alikataa.Baada ya mkutano huo Mkuu wa Wilaya aliondoka na watu sita na kuwaweka ndani katika kituo cha polisi Muleba. Kesho yake watu wawili kati yao walipata dhamana.
7. Tar.30/04/2013: Mtendaji wa kata Bw. Lameck Byarugaba alipokea simu kutoka kwa askari wa kituo cha polisi Muleba, Afande Aloyce akimtaka kuwa tar.02/05/2013 awapeleke aliowadhamini (Diwani na mtendaji wa kijiji) kwa ajiri ya kuandika maelezo ya ziada juu ya mgogoro huu.
8. Tar.02/05/2013: Bila kukosa, Diwani na mtendaji wa kijiji walifika kituoni saa 4. Hawakuulizwa chochote zaidi ya kuwekwa chini ya ulinzi. Ilipofika saa6 walisomewa mashitaka mawili ya mauaji na kutakiwa kutojibu chochote zaidi ya kupelekwa mahabusu.
Yatokanayo;
- Hii inaonyesha kuwa mkuu wa Wilaya alichukizwa na Diwani kukaidi agizo lake la kumtaka ateremshe bendera. Ndiyo maana hakusubiri hata siku ya kutajwa kesi yao yaani tar.6/5/2013 badala yake akawataka wafike polisi mapema tar.2/05/2013
- Wananchi walioshiriki katika ugomvi huo na kusababisha vifo vya walinzi/wafugaji wanajulikana na tayari wamekimbia kijiji. Pia majina yao yamepelekwa kwa OCD
- Walinzi/wafugaji waliouawa ni wa Block.No 18 lakini ugomvi na mauaji vilitokea katika Block.No 17. Hii inaonyesha walivokuwa wamejiandaa kufanya uhalifu na vurugu kwa kutumia bunduki zao.
- Pia cha kushangaza, mtu aliyempiga risasi na kumuua raia/mkulima katika Block No.18 linalomilikiwa na Bw.Medard Langile yupo na hajakamatwa.