DIT VS COeT, UDSM!

mdogo wandu chuo bora tanzania katika kozi ya engineer ni DIT, MUST, ARUSHA TECH, kwa nn vyuo hvi ni practical oriented UD wape sheria,biashara, siasa na uongozi lakini sio engineer mwenye akill ataona mm nimesha kua field na mtu wa degree UD na mtu mwenye diploma tu DIT na mbeya kwa kwel madogo wa dip wako poa zaidi unavyozani.
 
ua ryt kaka bt kumbuka dit ni kama college,i mean unaweza ukalinganisha na coet udsm na wanatoa koz za uhandisi wote bt ukitaka kuongelea udsm huwez linganisha na dit..udsm ni chuo cha 15 africa na 1032 dunia bt dit haimo kabisa!
Interest yang ni ktk koz za uhandis nchni c udsm kama udsm datz y nkamention coet tu!
kaka tatizo sio chuo ni cha ngapi inabebwa na masomo ya sanaa na sio engineer ata siku moja, mfano taa za barabaran usalama dar es salaal walichukuliwa wanafunzi UD wakazifunde zikawashinda wakawachukua watoto wa DIT tena diploma wakaweza hicho unajisifia ni chuo
 
tatizo Mkikosa nafasi udsm ndo mnakuja hapa kuanza kuiponda Ud. .
Kuna rafiki angu amedisco ud anakuja Dit hapa. Am sure na yeye ataanza kuiponda ud siku si nyingii.
ukipitia hii thread vizuri kuna jamaaa mmoja katoa point sana pale juu.
Kwanini kile siku ni Ud vs UDOM mara ud vs . Mzumbee , ud vs Ardhi .
Kwanini ud always...??
 
tatizo Mkikosa nafasi udsm ndo mnakuja hapa kuanza kuiponda Ud. .
Kuna rafiki angu amedisco ud anakuja Dit hapa. Am sure na yeye ataanza kuiponda ud siku si nyingii.
ukipitia hii thread vizuri kuna jamaaa mmoja katoa point sana pale juu.
Kwanini kile siku ni Ud vs UDOM mara ud vs . Mzumbee , ud vs Ardhi .
Kwanini ud always...??

Yawezekana ud wanachukua wanafunzi waliofanya vizuri form six,dit wanachukua wa kawaida sasa linganisha product zao,dit wako bora sana kuliko hawa vipanga wa Ud
 
Yawezekana ud wanachukua wanafunzi waliofanya vizuri form six,dit wanachukua wa kawaida sasa linganisha product zao,dit wako bora sana kuliko hawa vipanga wa Ud
tena ukikukutana na alieanza diploma then degree pale pale dit anakuwa nondo balaa
 
kaka tatizo sio chuo ni cha ngapi inabebwa na masomo ya sanaa na sio engineer ata siku moja, mfano taa za barabaran usalama dar es salaal walichukuliwa wanafunzi UD wakazifunde zikawashinda wakawachukua watoto wa DIT tena diploma wakaweza hicho unajisifia ni chuo
Barabara gani. .??
Msituletee story za mtaani hapa
 
Chuo kinaeza kikawa bora lakin wanaoenda hapo wasiwe nondo ila chuo kinaweza kua sio bora sana lakin waendao hapo ni nondo kwel..sasa udsm mnatushambulia sana kwanin.?hiv walim bora wako wap?si udsm.sasa udsm kinaweza kisiwe bora kwa usemavyo wew ila watu wanaoenda hapo ni nondo na ndomana walim wanatufundisha as if sis tunajua tayar..sasa hvyo vyuo vingne mnamegewa kila kitu sabab wanajua nyi hamko vzur kichwan,nkama watoto wa ndege yan mnalishwa kila ktu
 
I think aliye nacho huongezewa, ndo maana SUPERCOMPUTER IKAWEKA DIT!
Lakini mi uhalisia, practically, DIT wapo vizuri sana kwa wengi wao.
Theoretically, COET wapi vizuri sana wengi wao.
Kwa dunia ya LEO yenye ushindani kila kona, ni lazima practally uwe vizuri sana.
1. COET sometime wanaenda DIT kufanya practical-uhalisia hii sio practical ni study tour!

2. COET hawana vifaa Vya kutosha vya kisasa vingi ni zana za kale, wakati technologia inabadilika kila mili-second iondokayo.
Mfano, Digital total station SOKIA X 105, COET amna! While DIT zipo more zan 30.
Ufungaji wa mfumo wa digital kutoka anology, mkoa wa kigoma DIT walichukua zabuni na vijana wao walipiga kazi, na kazi ilikua nzuri.
Hivyo,
INSTITUTE OF TECHNOLOGY haitofanana na COLLEGE OF ENGINEERING katika kipindi hiki cha Mawasiliano angani (kipindi cha ushindani kitechnolojia)
In general, UDSM siasa imejaa sana hivyo panaoneka pako vzr ki knowledge wakati ni sifa ambazo haziwasitahi!
Mungu bariki tanzania
 
Kibaya zaidi unaweza kutanisha Diploma ya DIT(Full technician) na Degree ya Udsm akachukuliwa wa DIT hasa kwenye interview za mashirika kuna wakongwe huko wanaiamini sana DIT.
 
wapi ni pazuri kwa kusomea na usanifu katika kozi za uhandisi(Engineering)?
I mean mwanafunz akitoka anakuwa compitent!
Mostly kwa kozi za COMPUTER ENG and ELECTRONICS & TELECOM ENG for dit and COMP N IT ENG & TELECOM ENG for udsm,coet?
Duh kweli kazi ipo.
 
Jamani mm kila nikisoma conversation za maswala ya vyuo nakuta majigambo, kejeli, matusi na kebehi za wana-udsm wakikashifu vyuo vingine,

Sometimes najiuliza: hivi mtu unaweza kuonekana bora kwasababu umeweza kuonesha udhaifu wa mtu mwingine?

Kila nikisoma hoja za wana-udsm naona wanaeleza historia tu na sio current logic,

Utaskia:
- udsm chuo kikongwe ( hii hatukatai na kimetoa mchango mkubwa sana kwa taifa, but twambie; currently kuna nn?)
- walimu wa vyuo vingi nchini wametoka udsm (hapa utakumbuka kauli ya mwana falsafa; John Dewey aluyesema "the quality of education shall never be raised above the quality of teachers" kama walimu wa vyuo hivi wametoka udsm then vyuo hivi viwe poor,
Unadhani huo u-poor umeanzia wapi?)
-udsm ina-rank the first kitaifa: (hapa tunapaswa tuelewe vigezo vinavyotumika ku-rank vyuo.
Kwa kifupi wanaangalia popularity, number of search engines, number professors n.k.
Academic ina less than 10% ktk ku-rank vyuo kwasababu kila chuo kina mtaala wake.
Kwakuangalia vigezo hivyo,
Udsm ina-rank the first kwasababu imeanzishwa zamani hivyo ime-gain popularity, ina product nyingi n.k.
BUT ukisoma ranking ya vyuo, mwishoni hua wanaeleza kua rank hiyo isitumike ku-jaji academic excellence ya vyuo kwasababu sio academic based ranking.

Kwa ufupi tu udsm mnapaswa kubadilika,
Vyuo vingi kwasasa viko vizuri sana,
Hata hapa nikipitia majadiliano yenu,
Naona DIT wakitoa evidence hadi video za mambo wanayoyafanya lkn UDSM wana historia, matusi, kejeli na vijembe.
Hii ni aibu kubwa sana,

Nime-experience uwezo wa vijana wanaosoma education UDSM na UDOM, nnachoweza kusema ni kua mwanafunzi wa education UDOM anauwezo Mara tatu zaidi ya wa UDSM kuanzia discipline, content (ACK & PCK).

Ningeshauri UDSM mjifunze busara kutoka UDOM, SAUT, SUA na vyuo vingine ambao kwao wakiona mtu anakosea au ana udhaifu wanamrekebisha na kushirikiana nae na sio kumkebehi na kumuona hafai,

Mm ningeomba tu vijana mchape kazi muache majigambo yasiyo na tija,
Ktk ranking ya vyuo,
Undergraduate una mchango wa approximately 0.001%

Ikumbukwe, TCU walifanya uhakiki wa vyuo na wakavifungia vyuo vilivyokosa ubora au program zilizokua na mapungufu ktk vyuo husika,
Kwa maana hiyo vyuo vilivyobaki vyote ni bora.
Kilichobaki ni jitihada za mtu binafsi.

Ikumbukwe pia wanafunzi walio ktk vyuo vikuu wote walikubaliwa na NECTA, wengine na NACTE na sasa approved by TCU kua wasake degree; jitihada hizi si za kubezwa Hata kidogo na hakuna kilaza atakayepitishwa organizations zote hizo.

Wakati huo pia tukumbuke kuna vijana wamesoma shule za kata lkn saiv ni international figures na kuna wengine wamesoma international schools then saivi ni ma-admin wa magroup ya WhatsApp na waanzisha uzi maarufu jf.

Mwanachuo utaonekana bora ikiwa una mchango thabiti kwa familia yako na jamii yako na si vinginevyo.

NAWAPENDENI WANACHUO WOTE LAKINI NTAZIDI KUWAPENDA IKIWA MTAHESHIMIANA,
msomi mzuri hujiheshimu, huwaheshimu wenzake na jamii kwa ujumla
 
Back
Top Bottom