JustineKitenge2016
Member
- Jul 17, 2016
- 46
- 62
Habari za sa hivi wana jamvi, najua au nafahamu wapo watu wwngi ambao wameshaongea sana kuhusu diploma holders hakuna mapya mimi leo hii nataka niongezee tu, kama mnavofahamu sio watu wote tulipenda kusoma diploma sema upepo ulivyobadilika ndo tukaangalia altenative, ni ukweli usio pingika watanzania walio wengi wanaizarau sana elimu ya diploma sijui sababu ni nini hususani hizi diploma za kawaida ukiachilia hizi za udaktari au mambo yahusiyo afya, kwa upande mimi nilishajiandaa kwa majibu yoyote watu tunasoma kwa bidii lakini mpaka sa hivi nyumbani wananiona muongo yaani mpaka inafikia kipindi ninamkwepa baba kwasababu ya maswali kuhusu hili jambo, mpaka sasa hivi hakuna tamko lolote, wala hata tangazo lolote, je wakulaumiwa ni nani



