Dini, Utamaduni na Mazingira

WAKUONDOKA

Member
Oct 8, 2014
46
24
Niliwahi kuwaza na kujiuliza hivi wakati mababu zetu wanapokea ustaarabu mpya/dini walikuwa na taratibu zao za kuishi na kila taratibu zilikuwa na mazingira ambayo watu wanaishi chini ya kivuli cha Utamaduni.Ujio wa dini ulikuta watu na mazingira yao na tamaduni zao.
Ila dini zikaingilia tamaduni na mazingira ya watu(ama kwa uzuri/kwa ubaya) zikaja na taratibu mpya za kuishi kwa watu, kwa mf:dini ya kiislam ktk mazingira ilipokuta watu iliingiza utamaduni wa kiarabu(uislam ni imani
haina utamaduni)
1.Iliwavika kofia na kanzu (ikaondoa asili ya Uvaaji)
2.Ikawabatiza majina mapya (ikaondoa asili ya watu) kutoka ktk mazingira yao
Kwa mf: Leo ukimuuliza mtu Maana ya jina Juma au Seif hajui maana yake.
Angalizo: majina ya kibantu yalikuwa yakitolewa kuendana na mazingira/asili yake.
Ilihali hata ukristo unabeba mazila yaleyale ya uislam yani leo ukimuuliza mtu akupe maana ya jina Robert au Daud hajui.
Tafakari yangu...
1.Ivi haikuwa busara kwa mtu akaachwa na mazingira/tamaduni yake apokee imani tu.
Faida yake:
Ingesaidia kuacha watu wakaishi bila hila kwa sababu wako tofauti kiimani ila tamaduni wanashare pamoja.
2.Ingekuwa busara pia watu wakabaki na majina ya asili ikabaki imani tu
Faida yake:
Hii pia ingeacha watu wawe wamoja bila kubaguana kwa majina kwamba uyu ni muislam uyu ni mkristo.
3.Ingesaidia pia imani za watu kubaki moyoni na ingeimarisha zaidi hali ya kuvumiliana kidini(Religious tolerance)

Majumuisho ya yote hapo juu yangesaidia pia kuondoa ubinafsi ktk imani kwa sasa kila mmoja anaona mungu wake ndo sahihi ila si mungu wa mwenzake.
Nawasilisha,nakaribisha michango,mawazo mapya,kukosolewa.
 
Huu ulikuwa ukoloni tu wa kutawala akili za watu kabla ya kuhitimisha na utawala wa miili ya waafrika. Kama ni imani ingepaswa ibaki hivyo na si kubadilisha majina ya watu. Nchi za ulaya ambao ndiyo walioeneza ukristo huku Afrika, hawakubalisha majina yao ili yafanane na ya wayahudi waliowapelekea dini yao.
Hapa nakubaliana na Dr. Remmy aliyewahi kuimba kuwa kuwa tulinde mila na desturi zetu, akitolea mfano kuwa mzungu hakubali kuitwa MASAWE au SHIJA. Hata mwarabu hawezi kukubali kuitwa MKUDE au KOMBA. Kwanini sisi tukubali tu? Je, hizo dini walizoleta zimaamuru waumini wake waitwe kwa majina ya kigeni? Naomba kujua.
 
Mimi pia naomba kuuliza,tunashuhudia kwamba kila dini inafuvitia upande wake kwamba usipofuata mfumo wake hutokwenda mbinguni au peponi swali je wale wazee wetu waliokufa kabla ya kuingia dini hizi watakwenda motoni kwa kutokufuata moja ya dini hizi?
 
Mimi pia naomba kuuliza,tunashuhudia kwamba kila dini inafuvitia upande wake kwamba usipofuata mfumo wake hutokwenda mbinguni au peponi swali je wale wazee wetu waliokufa kabla ya kuingia dini hizi watakwenda motoni kwa kutokufuata moja ya dini hizi?
Hilo swali nimewahi kumuuliza mzee mmoja anaijua biblia vizuri lakini mwisho wa siku akaniambia wale hawataenda motoni kwasababu walikuwa hawajui lolote na akasema kama mtu ukifanya dhambi na haujui kwamba ni dhambi hiyo inakuwa sio dhambi.

Nikaja kusoma tena magazeti ya mashahidi wa yehova nikakuta wanatofautiana kuhusu swala la mungu kuja kuwachoma moto binadamu wote wenye dhambi.
Wanasema wanaamini mungu hawezi kuwa mpumbavu kiasi hicho aje kuwachoma watu moto.

Na nikajaribu kuwafuatilia kiundani zaidi wenyewe wanaamini kwamba mungu hakuumba ulimwengu kwa siku 6 ya saba akapumzika wanasema huenda mungu alitumia maelfu ya miaka kuumba ulimwengu wanasema huu ulimwengu ni mkubwa sana.
 
Back
Top Bottom