Dini ni Utamaduni wa watu fulani

Dini ni Utamaduni wa watu fulani

Ramea

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2015
Posts
2,146
Reaction score
4,090
Nitangulie kwa kusema Utamaduni ni neno pana linalojumuisha mfumo mzima wa Maisha, lengo la Uzi huu ni kuonesha ni jinsi gani tulivyoubeba utamaduni wa kigeni na kuufanya dini zetu na pengine tumenufaika nao ama kuumizwa nao pasipo kujua.

Nitawapitisha kwenye vipengele vya utamaduni 'Culture'. Hapa Ukristo nitauita 'Jewish Culture', Uislam kama 'Arabic Culture' na dini ya mwafrika ambayo ni 'African Traditional Religion' nitaiita African Culture. Kwahiyo nitazungumzia utamaduni wa kiyahudi, kiarabu na kiafrika. Sitarajii kupata maswali ya NINI MAANA YA DINI. Hapa hiyo dini yako naijadili Kama tamaduni tu wa watu fulani.

1. Uongozi na siasa. Waafrika walikuwa na tamaduni zao za kupata kiongozi, pia sheria na kanuni zao kabla ya kuletewa tamaduni mpya za kiarabu zilizoletwa na wa Asia hasa waarabu na kiyahudi zilizoletwa na wazungu. Kwenye makabila mengi, kiongozi wa kijadi alivaa kofia mbili, ya kisiasa na kidini kwenye matambiko. Ukristo ukaleta taratibu zake, siasa na dini zilitenganishwa. Huu ni utamaduni wa kiyahudi ambao haukuwa na uhusiano kati ya makuhani na magavana wa kirumi.
Uislam Kama ilivyo utamaduni wa kiarabu. Siasa na dini hufungamana. Ndiyo maana kuna nchi zinazofuata 'Sharia' za kiislam/kiarabu katika kuamua na kuongoza. Hizo zote ni tamaduni tu za watu, siyo maagizo ya Mungu.

2. Music. Waafrika wana vyombo vyao vya muziki 'music instruments' na styles zao za uimbaji 'musical notations'. Zeze, filimbi, ngoma, pembe za wanyama nk... Wakristo wakachukua muziki wa kiyahudi na kirumi uliotajwa kwenye Biblia. Baragumu, tarumbeta, zeze, vinanda...kuwa muziki safi wa kumwimbia Mungu. Kwa wakatoliki Papa Gregory akapendekeza Tuni fulani itumike duniani kote 'Gregorian music'. Hali kadhalika Waislam na kaswida, dufu ambazo ni musical notation za kiarabu wakazifanya nyimbo za kumsifu Mungu. Ni utamaduni tu, Mungu hana aina fulani ya kuimbiwa.

3. Language. Lugha zetu za kibantu zilitumika kuomba na maombi yakapokelewa. Viongozi wa kimila walitambika kwa Lugha zao kwa Miungu yao. Wazungu wakatuletea ukristo katika lugha ya kilatini. Ibada na misa zilifanyika kwa Lugha hii kwa karne kadhaa. Warumi ndiyo walikifanya kilatini kiwe lugha ya Mungu ingawa Mambo yalibadilika badae. Uislam kwakuwa ni utamaduni wa kiarabu, wao Hadi leo huamini Mungu anajua kiarabu tu. Hakijabadilika chochote. Ni utamaduni tu, hata kichina na kijapani Mungu anakisikia.

4. Food. Chakula katika utamaduni wa kiafrika una makatazo na kanuni za kula chakula. Kulikuwa na hadithi zenye kukataza au kuruhusu chakula/mnyama fulani. Utamaduni wa kiyahudi hali kadhalika, Kuna chakula haram na kisicho haramu, ingawa warumi wamefanya yao kugeuza masndiko. Kuna wakristo wanaokula kila kitu na wale wanaochagua kulingana na mapokeo ya agano la kale la kiyahudi. Waislam pia, utamaduni wa kiarabu katika chakula umebebwa kama ulivyo. Haram na Halal ni kadiri ya utamaduni wa kiarabu ambao walifungamana sana na wayahudi. Ndiyo maana, haram zilizopo katika Agano la kale utazikuta kwenye Qur'an.

5. Art, craft and Architecture. Sanaa na ubunifu. Waafrika tulikuwa na styles zetu za ujenzi wa nyumba za kuishi na ibada michoro na mapambo. Lakini leo hii nyumba za ibada zetu ni sawa na mahekalu ya kiyahudi na kirumi kwa wakristo, kukiwa na nakshi za misalaba. Kwa waislamu nako ni ramani za nyumba za kiarabu, michoro ya kiarabu na alama za 'Mwezi' ambao ni Mungu wa kiarabu aliyeabudiwa hata kabla ya Uislam. Ni tamaduni za watu tumejitwika.

6. Social interaction. Jamii za kiafrika zilikuwa na namna yake ya kuingiliana na kuhusiana kulingana na umri na jinsia. Ukristo wa kale ulibagua sana wanawake Kama ilivyo tamaduni za kiyahudi. Mwanamke alikuwa ni mtu wa 'kusitiriwa' lakini mambo yakabadilika badae, leo hii anasimama Hadi madhabahuni.
Waislam wao wameichukua tamaduni ya kiarabu Kama ilivyo ya kumsitiri mwanamke na kumfanya kiumbe dhaifu. Hachangamani na mwanaume iwe kwenye ibada hadi matukio ya kifo. Hii ni tamaduni ya kiarabu hadi leo, si maagizo ya Mungu, Ni utamaduni tu.

7. Tradition. Hii dhana ni pana.
~Dressing style, waafrika tulikuwa na namna yetu ya uvaaji, Kama ya masai na wengine, lakini ukristu ukatuletea kanzu na majoho. Hayo ni mavazi ya makuhani wa kiyahudi, si kwamba ukivaa shuka la kimasai Mungu hakusikii. Waislam nao kanzu, juba, hijab ambayo ni mavaz ya kiarabu yakafanywa kuwa mavazi rasmi. Ni utamaduni tu, Mungu hakuagiza uvae hayo ili uwe wake.

~Eating style. Namna ya kula kwa waafrika wa zamani ni tofauti na jamii za leo zilizoathiriwa na tamaduni za kiyahudi na kiarabu. Wapo wanaoamini kuwa na namna fulani ya ukaaji,(mezani au mkeka) Mungu hapendi, kisa tu myahudi au Mwarabu alifanya hivyo. Ni tamaduni zao tumezigeuza kuwa dini.

~Festivals. Sherehe na kumbukizi za kiafrika wa kale ni tofauti na za leo. Mtoto wa kiafrika akizaliwa kulikuwa na taratibu zake hadi anaingia utu uzima. Kuanguka kitovu, siku 40... Kwa wakristo utasikia kuna ubatizo, kipaimara (kipaimara ni hatua ambayo ipo hadi leo kwa wayahudi ambao siyo wakristu).... Pasaka pia ilikuwepo kabla ya ukristo. Na Waislam wana yao kama 'Hakika'..... Ambayo hufanyiwa watoto wa kiarabu kadiri ya tamaduni zao, si maagizo ya Mungu.

~Mazishi. Waafrika tukizika kwa namna tofauti tofauti kulingana na tamaduni ya kabila husika. Kuuacha mwili kwenye mapango na kuhama makazi, kufukia chini.... Ukristu umeleta style yake na Uislam hali kadhalika. Matumizi ya sanda, jeneza, kukafini, kuosha maiti ni tamaduni tu za kiarabu na kiyahudi, siyo maagizo ya Mungu.

~Tohara. Kwa waafrika hili jambo lilikuwepo kwa baadhi ya makabila. Wengine hadi Leo hawatahiriwi. Ni utamaduni wao. Kwa wayahudi ni utamaduni wao tangu kale, hali kadhalika waarabu. Kutahiri kumefanywa Jambo la kidini ingawa Ni utamaduni tu. Si agizo la Mungu kwamba hapokei kiumbe chenye 'govi' kwenye makao yake ya milele. Wapo wazungu na waafrika ambao hadi leo hawatahiriwi.

Karibuni kwa mjadala, kusiwe na malumbano ya kupigania Utamaduni wa kiyahudi Wala kiarabu hapa. Tujadili kwa hoja. Huu ni mtazamo wangu tu, unaweza kuwaza tofauti.
 
Umeandika vizuri dini ni sehemu ya utamaduni, sisi kama waafrika tumeacha tamaduni zetu na kukumbatia za wageni na kuziona ndio sahihi zaidi.

Waafrika leo ndio tunazijua dini kuliko hata hao walotuletea. Cha ajabu ni kwamba matatizo karibu yote makubwa yako huku njaa, ujinga, umasikini magonjwa n.k
 
swala la mungu kuleta vitabu ndo hua silielewi kabisa.
kwamba mungu anategemea maandishi kufikia watu wake?
ambao hawajui kusoma ?
ambao bado hawajifikiwa na vitabu mpaka sasa (wapo) ana mpango gani nao?

hizi vitabu vya dini ni utashi wa binadamu tu.
 
swala la mungu kuleta vitabu ndo hua silielewi kabisa.
kwamba mungu anategemea maandishi kufikia watu wake?
ambao hawajui kusoma ?
ambao bado hawajifikiwa na vitabu mpaka sasa (wapo) ana mpango gani nao?

hizi vitabu vya dini ni utashi wa binadamu tu.
Hawakosagi majibu watakuambia wewe unayejua kusoma mfafanulie huyo asiyejua kusoma
 
Hizo zote ni tamaduni tu za watu, siyo maagizo ya Mungu.
hongera sana mtoa mada.ila naomba kuuliza kwa mujibu wa hiyo maneno hapo juu.

Hayo maneno yanaashiria kuwa unakubali nadharia ya Mungu kuwa yupo.

Na unakubali kuwa kuna mambo yanatoka kwa Mungu kuja kwetu,ila siyo hayo ambayo umeyataja,yaani ukikusudia kuwa hayo hayatoki kwa Mungu.

Naomba kuuliza kuwa wewe unatumia mizani ama kipimo gani kujua kuwa haya kweli yanatoka kwa Mungu ?
 
Nitangulie kwa kusema Utamaduni ni neno pana linalojumuisha mfumo mzima wa Maisha, lengo la Uzi huu ni kuonesha ni jinsi gani tulivyoubeba utamaduni wa kigeni na kuufanya dini zetu na pengine tumenufaika nao ama kuumizwa nao pasipo kujua.

Nitawapitisha kwenye vipengele vya utamaduni 'Culture'. Hapa Ukristo nitauita 'Jewish Culture', Uislam kama 'Arabic Culture' na dini ya mwafrika ambayo ni 'African Traditional Religion' nitaiita African Culture. Kwahiyo nitazungumzia utamaduni wa kiyahudi, kiarabu na kiafrika. Sitarajii kupata maswali ya NINI MAANA YA DINI. Hapa hiyo dini yako naijadili Kama tamaduni tu wa watu fulani.

1. Uongozi na siasa. Waafrika walikuwa na tamaduni zao za kupata kiongozi, pia sheria na kanuni zao kabla ya kuletewa tamaduni mpya za kiarabu zilizoletwa na wa Asia hasa waarabu na kiyahudi zilizoletwa na wazungu. Kwenye makabila mengi, kiongozi wa kijadi alivaa kofia mbili, ya kisiasa na kidini kwenye matambiko. Ukristo ukaleta taratibu zake, siasa na dini zilitenganishwa. Huu ni utamaduni wa kiyahudi ambao haukuwa na uhusiano kati ya makuhani na magavana wa kirumi.
Uislam Kama ilivyo utamaduni wa kiarabu. Siasa na dini hufungamana. Ndiyo maana kuna nchi zinazofuata 'Sharia' za kiislam/kiarabu katika kuamua na kuongoza. Hizo zote ni tamaduni tu za watu, siyo maagizo ya Mungu.

2. Music. Waafrika wana vyombo vyao vya muziki 'music instruments' na styles zao za uimbaji 'musical notations'. Zeze, filimbi, ngoma, pembe za wanyama nk... Wakristo wakachukua muziki wa kiyahudi na kirumi uliotajwa kwenye Biblia. Baragumu, tarumbeta, zeze, vinanda...kuwa muziki safi wa kumwimbia Mungu. Kwa wakatoliki Papa Gregory akapendekeza Tuni fulani itumike duniani kote 'Gregorian music'. Hali kadhalika Waislam na kaswida, dufu ambazo ni musical notation za kiarabu wakazifanya nyimbo za kumsifu Mungu. Ni utamaduni tu, Mungu hana aina fulani ya kuimbiwa.

3. Language. Lugha zetu za kibantu zilitumika kuomba na maombi yakapokelewa. Viongozi wa kimila walitambika kwa Lugha zao kwa Miungu yao. Wazungu wakatuletea ukristo katika lugha ya kilatini. Ibada na misa zilifanyika kwa Lugha hii kwa karne kadhaa. Warumi ndiyo walikifanya kilatini kiwe lugha ya Mungu ingawa Mambo yalibadilika badae. Uislam kwakuwa ni utamaduni wa kiarabu, wao Hadi leo huamini Mungu anajua kiarabu tu. Hakijabadilika chochote. Ni utamaduni tu, hata kichina na kijapani Mungu anakisikia.

4. Food. Chakula katika utamaduni wa kiafrika una makatazo na kanuni za kula chakula. Kulikuwa na hadithi zenye kukataza au kuruhusu chakula/mnyama fulani. Utamaduni wa kiyahudi hali kadhalika, Kuna chakula haram na kisicho haramu, ingawa warumi wamefanya yao kugeuza masndiko. Kuna wakristo wanaokula kila kitu na wale wanaochagua kulingana na mapokeo ya agano la kale la kiyahudi. Waislam pia, utamaduni wa kiarabu katika chakula umebebwa kama ulivyo. Haram na Halal ni kadiri ya utamaduni wa kiarabu ambao walifungamana sana na wayahudi. Ndiyo maana, haram zilizopo katika Agano la kale utazikuta kwenye Qur'an.

5. Art, craft and Architecture. Sanaa na ubunifu. Waafrika tulikuwa na styles zetu za ujenzi wa nyumba za kuishi na ibada michoro na mapambo. Lakini leo hii nyumba za ibada zetu ni sawa na mahekalu ya kiyahudi na kirumi kwa wakristo, kukiwa na nakshi za misalaba. Kwa waislamu nako ni ramani za nyumba za kiarabu, michoro ya kiarabu na alama za 'Mwezi' ambao ni Mungu wa kiarabu aliyeabudiwa hata kabla ya Uislam. Ni tamaduni za watu tumejitwika.

6. Social interaction. Jamii za kiafrika zilikuwa na namna yake ya kuingiliana na kuhusiana kulingana na umri na jinsia. Ukristo wa kale ulibagua sana wanawake Kama ilivyo tamaduni za kiyahudi. Mwanamke alikuwa ni mtu wa 'kusitiriwa' lakini mambo yakabadilika badae, leo hii anasimama Hadi madhabahuni.
Waislam wao wameichukua tamaduni ya kiarabu Kama ilivyo ya kumsitiri mwanamke na kumfanya kiumbe dhaifu. Hachangamani na mwanaume iwe kwenye ibada hadi matukio ya kifo. Hii ni tamaduni ya kiarabu hadi leo, si maagizo ya Mungu, Ni utamaduni tu.

7. Tradition. Hii dhana ni pana.
~Dressing style, waafrika tulikuwa na namna yetu ya uvaaji, Kama ya masai na wengine, lakini ukristu ukatuletea kanzu na majoho. Hayo ni mavazi ya makuhani wa kiyahudi, si kwamba ukivaa shuka la kimasai Mungu hakusikii. Waislam nao kanzu, juba, hijab ambayo ni mavaz ya kiarabu yakafanywa kuwa mavazi rasmi. Ni utamaduni tu, Mungu hakuagiza uvae hayo ili uwe wake.

~Eating style. Namna ya kula kwa waafrika wa zamani ni tofauti na jamii za leo zilizoathiriwa na tamaduni za kiyahudi na kiarabu. Wapo wanaoamini kuwa na namna fulani ya ukaaji,(mezani au mkeka) Mungu hapendi, kisa tu myahudi au Mwarabu alifanya hivyo. Ni tamaduni zao tumezigeuza kuwa dini.

~Festivals. Sherehe na kumbukizi za kiafrika wa kale ni tofauti na za leo. Mtoto wa kiafrika akizaliwa kulikuwa na taratibu zake hadi anaingia utu uzima. Kuanguka kitovu, siku 40... Kwa wakristo utasikia kuna ubatizo, kipaimara (kipaimara ni hatua ambayo ipo hadi leo kwa wayahudi ambao siyo wakristu).... Pasaka pia ilikuwepo kabla ya ukristo. Na Waislam wana yao kama 'Hakika'..... Ambayo hufanyiwa watoto wa kiarabu kadiri ya tamaduni zao, si maagizo ya Mungu.

~Mazishi. Waafrika tukizika kwa namna tofauti tofauti kulingana na tamaduni ya kabila husika. Kuuacha mwili kwenye mapango na kuhama makazi, kufukia chini.... Ukristu umeleta style yake na Uislam hali kadhalika. Matumizi ya sanda, jeneza, kukafini, kuosha maiti ni tamaduni tu za kiarabu na kiyahudi, siyo maagizo ya Mungu.

~Tohara. Kwa waafrika hili jambo lilikuwepo kwa baadhi ya makabila. Wengine hadi Leo hawatahiriwi. Ni utamaduni wao. Kwa wayahudi ni utamaduni wao tangu kale, hali kadhalika waarabu. Kutahiri kumefanywa Jambo la kidini ingawa Ni utamaduni tu. Si agizo la Mungu kwamba hapokei kiumbe chenye 'govi' kwenye makao yake ya milele. Wapo wazungu na waafrika ambao hadi leo hawatahiriwi.

Karibuni kwa mjadala, kusiwe na malumbano ya kupigania Utamaduni wa kiyahudi Wala kiarabu hapa. Tujadili kwa hoja. Huu ni mtazamo wangu tu, unaweza kuwaza tofauti.

Kuna wafia dini wa kufata mkumbo ukijaribu kuwaeleza mambo wanakupinga

Kwenye sWala la uvaaji hapo wanawake wanapovaa nguo na kuacha vitovu wazi wanakwambia sio utamaduni wetu tena nilisikitishwa sana kuskia kauli kama hii ikitoka kwa mkuu wa nchi, nakumbuka kipindI cha nyuma hata wadada wanaovaa nguo fupi barabarani walikuwa wanaadhibiwa kwa kigezo kuwa sio utamaduni wetu,

Leo hii mtu akienda kwa mganga wa asili hata kutibiwa magonjwa ya kawaida anaonekana mchawi
tumeitupa mizimu yetu tumemuinua yesu wa wazungu na Muhammad wa waarabu

Inasikitisha sana
 
hongera sana mtoa mada.ila naomba kuuliza kwa mujibu wa hiyo maneno hapo juu.

Hayo maneno yanaashiria kuwa unakubali nadharia ya Mungu kuwa yupo.

Na unakubali kuwa kuna mambo yanatoka kwa Mungu kuja kwetu,ila siyo hayo ambayo umeyataja,yaani ukikusudia kuwa hayo hayatoki kwa Mungu.

Naomba kuuliza kuwa wewe unatumia mizani ama kipimo gani kujua kuwa haya kweli yanatoka kwa Mungu ?
Kiufupi naamini Mungu yupo, na amejidhihirisha wazi kabisa. Kila jamii dunia mzima nguvu ya Mungu ipo. Kuna dini kubwa sita duniani. Kote Mungu anajionesha. Kuna
~Judaism
~Christianity
~Islam
~Hinduism
~Budhism
~Sikhism
Mtawa(monk) wa kibudha anaweza fanya maajabu makubwa sana ya kutembea juu ya maji au kutembea bila kukanyaga ardhi(kupaa) Kama Yesu. Lakini si mkristu Wala mwislam.
 
swala la mungu kuleta vitabu ndo hua silielewi kabisa.
kwamba mungu anategemea maandishi kufikia watu wake?
ambao hawajui kusoma ?
ambao bado hawajifikiwa na vitabu mpaka sasa (wapo) ana mpango gani nao?

hizi vitabu vya dini ni utashi wa binadamu tu.
Kuna maandiko yenye akili kubwa sana(wakatoliki watanisahihisha) kama ya Saint Thomas Aquinas na Ignas of Loyola. Kama wangeishi kabla ya Biblia, maandiko yao yangetumika kama 'kitabu kitakatifu' na pengine wangeitwa Mitume wa dini fulani.
 
Back
Top Bottom