Dini na Serikali zinapotumia meza moja isiyokuwa na viti

I thought fools normally write short stupid, nonsense sentences, but i was wrong. Look at this fool!!! Maelezo mareeeefu halafu pumba tupu. Pole sana. Tuna safari ndefu sana....
Hakika unaumia mashavu kufikiri, Kiingereza gani hicho angalia "short stupid " hakuna sentensi kama hiyo au huo muunganiko wa "short stupid ".Hakika shule wengine nilienda kukariri ujinga
 
I thought fools normally write short stupid, nonsense sentences, but i was wrong. Look at this fool!!! Maelezo mareeeefu halafu pumba tupu. Pole sana. Tuna safari ndefu sana....
Mkuu acha kutafsiri kiswahili kwenda Kiingereza umeandika mchanganyiko wa kachumbari na maharage, Haieleweki sentensi unaongelea wakati upi uliopo, uliopita au ujao, au wakati unaoendelea angalia sentensi hii "I thought fools normally " nani alikufundisha muunganiko huu wa thought Kama Past halafu fools normally, Hakika kazi ya kufundisha watoto ni shida
 
Maelfu wasio kuwa na access au upatikanaji wa hizo Waraka wanamsikiliza nani ? Hawa Viongozi wa dini ni kwa ajili ya waumini wao, Wengine sidhani Kama nyaraka zinawahusu kwani hawaamini katika Viongozi au makanisa hayo, Nyaraka zingetumika kujenga Kanisa na sio mapambano na watawala, watawala huja na wanapita haya makanisa Afrika yapo muda mrefu
Tafadhali naomba nionyeshe nyaraka ya dini inayopapambana na serikali,maana umerudia maneno "nyaraka kupambana na serikali" zaidi ya mara moja.
 
Tafadhali naomba nionyeshe nyaraka ya dini inayopapambana na serikali,maana umerudia maneno "nyaraka kupambana na serikali" zaidi ya mara moja.
Zinapatikana pale Azania front au nenda Kanisa la wabenedictine la St Joseph pale mjini omba Waraka kuelekea pasaka 2018 utapewa copy au Tafuta uzi humu soma
 
Zinapatikana pale Azania front au nenda Kanisa la wabenedictine la St Joseph pale mjini omba Waraka kuelekea pasaka 2018 utapewa copy au Tafuta uzi humu soma
Mosi,mimi sipo TZ.
Pili,weka hapa jukwaani kwa faida ya wengi ili sote tuone "mpambano" huo wa nyaraka za dini na serikali.
 
Maelfu wasio kuwa na access au upatikanaji wa hizo Waraka wanamsikiliza nani ? Hawa Viongozi wa dini ni kwa ajili ya waumini wao, Wengine sidhani Kama nyaraka zinawahusu kwani hawaamini katika Viongozi au makanisa hayo, Nyaraka zingetumika kujenga Kanisa na sio mapambano na watawala, watawala huja na wanapita haya makanisa Afrika yapo muda mrefu
1. Kama zingekuwa nyaraka kuhusu jinsi ya kuabudu labda ungekuwa sahihi, lakini nyaraka hizi zinavipengele vihusivyo jinsi serikali yetu inavyo tutawala na madhara yataokanayo na hayo. Hivyo basi misimamo iliyo katika nyaraka hizo hugusa waumini wao na wasio waumini wao yaani watanzania wote kwa ujumla.
2. Kama nilivyo eleza hapo juu, hili ni jukumu la KIROHO la taasisi za dini kuona kwamba serikali ikitoka nje ya msitari inabidi waikumbushe. Bahati mbaya serikali ndio iliyoyumia lugha ya ulichokiita mapambano. "Wewe Askofu", "Ndani ya siku kumi" , "hatua kali zaidi" etc.
3. Viongozi wa dini sio kwa ajili ya waumini wao tu ndiyo maana wanatakiwa wawe makini katika yale wanayo yaongelea au kufanyia kazi. Tuna kwa mfano vyuo vikuu vya dini (mfano MUM, SAUT, Tumaini etc), huduma za afya (pamoja na hosipitali za rufaa), masekondari chungu nzima. Taasisi hizi kwa kazi na uwekezaji waliofanya na wanaoufanya zisingependa kuwa na ugomvi na serikali hivyo wakisema kitu mhusika anatakiwa awe makini. Husema tu pale wanapo ona kuna ulazima wa kusema.
 
Wakati wanapotoa waraka au nasaha au maoni kwa viongozi wa dini ya Kiislamu hasa huku Zanzibar, tunaambiwa tusichanganye dini na siasa, wakati hii siasa tunayo hubiri ilianzia katika dini, angalia miaka ya AD katika vitabu vya Mungu, vinavyo elezea historia ya mitume ya Mungu pamoja na wafalme wakati huo, pia zamani viongozi wa dini ndio walio kuwa wakitumika kama justice, kwa kutumia vitabu vya Mungu.

Kwa kadri miaka Inavyo kwenda, viongozi wakaona kwamba dini unawazua kufanya mambo ambayo yako kinyume kwenye law ya dini, wakaanza kutunga sheria mpya ambazo zita toa uhuru zaidi kwao, na kuwalinda wanao wataka.

Leo hii viongozi wa dini ni sumu kwa viongozi na serikali, iwe muislam au Christo lkn zaidi uislam, viongozi wa dini ya Kiislamu kila siku gerezani, na mpaka leo hii viongozi wa Uwamsho wapo gerezani
 
Back
Top Bottom