Tuanze kwa kubadili lugha kwanza, iko hivi; Lawyer ni mwanasheria, Advocate ni wakili.
Tuanzie hapa sasa:
Kila Wakili ni Mwanasheria, ila sio kila Mwanasheria ni Wakili
Kimsingi, mtu yeyote aweza kuwa Mwanasheria ikiwa atasoma taaluma ya sheria kwa ngazi ya shahada (LL.B), lakini ili kuwa Wakili ni mchakato mrefu zaidi.
Mchakato wa mwanasheria kuwa wakili:
Mchakato huu unawahusu tu wale waliohitimu shahada ya sheria kuanzia mwaka 2008 na kuendelea.
Kwamba baada ya kupata shahada ya sheria utatakiwa uende tena chuo cha sheria (law school) ukasome na kufaulu Post Graduate Diploma in Legal Practice ndipo upate sifa ya kuwa wakili.
Baada ya kuipata hiyo sifa bado hujawa wakili, wewe bado ni mwanasheria. Ili uwe wakili utatakiwa ufungue maombi maalumu (petition) kwenda kwa jaji mkuu kumuomba akupokee na akuapishe, naye baada ya kukufuatilia tabia na mwenendo wako, kukufanyia upembuzi wa maandishi katika nyaraka zako zote na mahojiano yakinifu ya mdomo (interview) akiridhika ndipo atapanga siku ya kukuapisha.
Ndipo baada ya kuapishwa sasa utakuwa wakili.
Sent using Jamii Forums mobile app
Tuanzie hapa sasa:
Kila Wakili ni Mwanasheria, ila sio kila Mwanasheria ni Wakili
Kimsingi, mtu yeyote aweza kuwa Mwanasheria ikiwa atasoma taaluma ya sheria kwa ngazi ya shahada (LL.B), lakini ili kuwa Wakili ni mchakato mrefu zaidi.
Mchakato wa mwanasheria kuwa wakili:
Mchakato huu unawahusu tu wale waliohitimu shahada ya sheria kuanzia mwaka 2008 na kuendelea.
Kwamba baada ya kupata shahada ya sheria utatakiwa uende tena chuo cha sheria (law school) ukasome na kufaulu Post Graduate Diploma in Legal Practice ndipo upate sifa ya kuwa wakili.
Baada ya kuipata hiyo sifa bado hujawa wakili, wewe bado ni mwanasheria. Ili uwe wakili utatakiwa ufungue maombi maalumu (petition) kwenda kwa jaji mkuu kumuomba akupokee na akuapishe, naye baada ya kukufuatilia tabia na mwenendo wako, kukufanyia upembuzi wa maandishi katika nyaraka zako zote na mahojiano yakinifu ya mdomo (interview) akiridhika ndipo atapanga siku ya kukuapisha.
Ndipo baada ya kuapishwa sasa utakuwa wakili.
Sent using Jamii Forums mobile app