Diaspora tumepiga hatua miaka 25!

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,550
8,642
Kuwa diaspora hasa hapa US ilikuwa kitu kigumu sana hasa kwa vijana wengi ambao tuliondoka tukiwa na miaka 1997-2001 baada ya kumaliza high school. Sio tu kulikuwa hakuna Watanzania wengi miaka hiyo 1997-2001 bali wengi walikuwa wadogo hivyo tulikuwa hatuna mifano mingi ya kuiga. Lakini kibaya zaidi wazee wa Kitanzania ambao walikuwa wasomi wakati huo wengi waliwakimbia Watanzania vijana na kuona ni kama mizigo.

Baada ya miaka 25 jumuia zimekuwa na mafanikio sana. Kuna wasomi wengi, wafanyabiashara wengi na hata watoto wa kizazi kipya wengi wamefanikiwa kwenye vyuo vya juu sana. Hizi hatua nyingi wengi hawazifahamu lakini Watanzania wamepiga hatua sana diaspora hasa US

Tushukuru Mungu kwa hili na tuanze mikakati ya kusaidia nchi yetu. Sasa tuna wataalamu kila mahali

07F9CE8F-B7C5-4EBA-822B-9442D95C0C89.jpeg
 
Kuna wakati niliona nchi za Afrika ambazo diaspora wake wanaongoza kutuma pesa kwao either kusaidia ndugu, jamaa na marafiki zao, au kuwekeza kiuchumi.

Tanzania hatukuwa kwenye nafasi nzuri, tulipitwa na nchi ndogo kama Rwanda, naona huu ndio wakati wenu muanze kupambana kwenye eneo hilo.
 
Ukishaona takataka inajiita Diaspora, inaiigiza Maisha mazuri iko mbeleeez.

Halafu kutwa kucha iko busy kwenye mitandao ya Kiswahili kujitapa tapa Mimi Diaspora, Mimi Diaspora unue Hakuna mtu hapo.

Njaaaaaaaaa kaliiiiiii
 
Kuna wakati niliona nchi za Afrika ambazo diaspora wake wanaongoza kutuma pesa kwao either kusaidia ndugu, jamaa na marafiki zao, au kuwekeza kiuchumi.

Tanzania hatukuwa kwenye nafasi nzuri, tulipitwa na nchi ndogo kama Rwanda, naona huu ndio wakati wenu muanze kupambana kwenye eneo hilo.
Madiaspora wakituma hela kwa ndugu zao huwa zinaibwa na kuliwa kabisa. Pia masuala ya sheria ya kupokea hela Tz zimekaa vibaya. Ila Tunakumbushana tu. Mtanzania ni mtanzania tu. Uaminifu ni 0.
 
Kuna wakati niliona nchi za Afrika ambazo diaspora wake wanaongoza kutuma pesa kwao either kusaidia ndugu, jamaa na marafiki zao, au kuwekeza kiuchumi.

Tanzania hatukuwa kwenye nafasi nzuri, tulipitwa na nchi ndogo kama Rwanda, naona huu ndio wakati wenu muanze kupambana kwenye eneo hilo.

Tulikuwa chini lakini ni kama $500M bado sio pesa ndogo ukilinganisha na idadi ya diaspora. Wenzetu wako wengi zaidi. Lakini App za kutuma pesa zilikuwa tatizo

Tatizo kubwa ni sheria zetu za diaspora pesa nyingi kwa mfano kenya wananunua nyumba na kuwekeza kwenye biashara kwa Tanzania sheria sio rafiki hivyo pesa nyingi ni za vitu vidogo vidogo tu. Raisi Samia anabadilisha sheria ili diaspora wawe na uhakika na mali zao
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Ukishaona takataka inajiita Diaspora, inaiigiza Maisha mazuri iko mbeleeez.

Halafu kutwa kucha iko busy kwenye mitandao ya Kiswahili kujitapa tapa Mimi Diaspora, Mimi Diaspora unue Hakuna mtu hapo.

Njaaaaaaaaa kaliiiiiii
Diaspora wengi especially kutoka Tanzania huwa wakifika huko pamoja wanamakaratasi wengi huwa wajiendelezi kielimu wamedhirika na kazi za warehouse na care,pia kuchukiana wenyewe kwa wenyewe upendo uliopo nyumbani nje sio rahisi kuupata
 
Diaspora wengi especially kutoka Tanzania huwa wakifika huko pamoja wanamakaratasi wengi huwa wajiendelezi kielimu wamedhirika na kazi za warehouse na care,pia kuchukiana wenyewe kwa wenyewe upendo uliopo nyumbani nje sio rahisi kuupata
Halafu naona sasa hivi Black American kibao wanahamia sana Africa, hats Tanzania wamejaa kibao.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom