FortJeasus
JF-Expert Member
- Jan 19, 2012
- 603
- 397
Gazeti la Mwanahalisi ktk toleo lake na.279 ukurasa wake wa Tisa, la wiki hii limechapisha mahojiano kati yake na ndugu Diana Chilolo mbunge wa viti maalumu,CCM mkoa wa Singida.Mwishoni mwa mahojiano, ameeleza kuwa amesoma ktk shule ya Sekondari Mwenge iliyopo mjini Singida.Napenda kuchukua fursa hii kuueleza umma kuwa mama huyu hakuwahi kusoma Mwenge Sekondari na yafaa hapa ifahamike wazi kuwa hana elimu ya sekondari.
Tovuti ya bunge inaonyesha kuwa eti amepitia Mwenge kwa masomo ya Kidato cha Tano na Sita mwaka 1997.Hili katu haliwezi kuwa kweli maana,kwa makusudi kabisa, ameacha kueleza shule alikopatia elimu ya kidato cha Nne.Sote twafahamu kuwa kwa mujibu wa mfumo wa elimu wa Tanzania ,kusoma na kufaulu Kidato cha Nne ni sharti la lazima kwa mtu kuweza kufanya mtihani wa Kidato cha Sita.Kwa hiyo haiwezekani usome Tanzania ktk ngazi ya Kidato cha Sita bila kusoma kidato cha NNE.
Jamii iwe makini na hawa matapeli wa elimu waliotapakaa kote nchini.Nimesoma Mwenge Sekondari na nimekataa kukaa kimya wakati jina la shule yetu linatumiwa na wanasiasa wababaishaji kama huyu mbunge wa viti maalumu.
Tovuti ya bunge inaonyesha kuwa eti amepitia Mwenge kwa masomo ya Kidato cha Tano na Sita mwaka 1997.Hili katu haliwezi kuwa kweli maana,kwa makusudi kabisa, ameacha kueleza shule alikopatia elimu ya kidato cha Nne.Sote twafahamu kuwa kwa mujibu wa mfumo wa elimu wa Tanzania ,kusoma na kufaulu Kidato cha Nne ni sharti la lazima kwa mtu kuweza kufanya mtihani wa Kidato cha Sita.Kwa hiyo haiwezekani usome Tanzania ktk ngazi ya Kidato cha Sita bila kusoma kidato cha NNE.
Jamii iwe makini na hawa matapeli wa elimu waliotapakaa kote nchini.Nimesoma Mwenge Sekondari na nimekataa kukaa kimya wakati jina la shule yetu linatumiwa na wanasiasa wababaishaji kama huyu mbunge wa viti maalumu.