Simiyu Yetu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2013
- 18,949
- 4,643
Mkuu sina cha kuongeza kwenye coment zako naungana na wewe kabisa huyu mzee anamadoa mengi sana halafu mimi nasema kila siku hawa waliojitangaza kugombea urais inawezekana asipatikane hata mmoja kuwa Rais jk siyo kama tunavyodhani ataleta mgombea mwenye uadulifu siyo wezi kama lowasa.Watanzania bwana kumbe wengi wenu bado wachumia tumbo..mimi kama mtanzania wa kawaida ambaye sina kundi nadhani bwana Diallo ametupa just 'food for thought' ya kusaidia kumjua mgombea wetu wa urais 2015. sasa ss badala ya kupembua na kuchanganya na akili zetu mnamzonga bwana Diallo,,hizo ni njaa tu inawezekana kuna mambo amesema ya kweli na tulikuwa hatuna uwezo wa kuyajua kutoka kwa huyo mgombea wetu kipenzi.kwangu mimi kumshambulia whistleblower ni kupoteza maana nzima ya information. bwana Diallo sio mgombea na Membe sijui anaingiaje..huo wote ni upotofu. tusubiri majibu kutoka kwa Lowassa akikanusha hayo au athibitishe uongo wa hayo..Ningekuwa Lowassa kesho ningeenda uwanja wa taifa nikakimbia kuzunguka mara 10 na wapiga picha huru. hii ingetosha kumwumbua Diallo kuliko hii kazi mnayofanya hapa..umma wote umeshaanza kuamini huyo jamaa ni mgonjwa sana..kwa wanaoangalia mchezo wa ngumi bondia akiona mpinzani anamchubuko basi huendelea kulenga hapo hapo hadi amshinde..mshaurini mzee aje na hoja sio kutumia mamluki..kwa wale wanaosema hana papara za kujibu ni kweli yy ameshawaibia waTanzania na sasa amewanunua wajinga wengi kwa pesa ya wizi sasa wanamsemea kwa niaba yake kumbe mnataka afanye nn tena..tuamke jamani tuache njaa tusaidie nchi ipate kiongozi mzuri na sio mtu mwenye madoa madoa..kwangu mm sioni anayefaa kati ya Lowassa na Membe wote ni mizigo tu..hivi maandishi mengi humu jamvini ni kuonyesha jinsi watz tulivyopotea njia na kuelekea upande tofauti kiasi kwamba kurudi tunashindwa.