Kawapendelea wapi?? Kibiblia mbona neema ipo kwa watu wote. Hapo mwanzoni according to bible dunia nzima ilikuwa inamuabudu Mungu rejea Adam na Noah.... Ila baada ya Kuja Nimrod dini za kipagan zikasambaa dunia nzima na wote wakamuacha Mungu alibakia tu Shem na kizazi chake ambako ndio Abraham alitokea.
Hivyo kwa kuwa Abraham alikuwa mwaminifu kwa huyo Mungu yaani YAHWEH ndio akaamua kuweka naye mkataba huu
Mwanzo 12:1-3
1
BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;
2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;
3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.
Kwahiyo Israel ilikuwa great sio sababu ya kupendelewa bali sababu ya kurithi baraka za Abraham.
Lakini hio ilikuwa agano la kale kwa sasa dunia nzima wamekua wana wa Abraham as long as wanafuata imani ya Mungu wa Abraham yaani YAHWEH
Galatia 3
29
Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.
Kwa maelezo zaidi soma huu uzi wangu utapata mbili tatu kuwa Israel haipendelewi bali wote tupo sawa na hta kuwazidi kwa mbali sana kwenye macho ya MUNGU.
Habari za jioni wana JF mada ya leo ni sensitive kidogo maana inagusa moja ya topic zenye utata katika ulimwengu wa imani ila ningependa tusome kwa utulivu uzi wote alafu tujadiliane kwa hoja ili tuweze kusolve hili swali la karne nyingi sasa. UTANGULIZI Mwanzoni kulikuwa na agano kati ya...
www.jamiiforums.com