Ni kweli alichofanya Jecha ni ubakaji wa demokrasia, ni kitendo haramu na batili.
Na baada ya kubaka hiyo tarehe 25 October, akaahidi kubaka tena, na tarehe akaitangaza.
Cha ajabu aliyebakwa, hakuchukua hatua yoyote kupinga ubakwaji huo, na tarehe ya kurejelewa kwa ubakaji ilipofika, mbakwaji akasusa kwenda eneo la ubakaji wa mwanzo, akafuatwa huko huko aliko na akabakwa tena huku ametulia tuli!.
Batili, isipobatilishwa inageuka halali, na haramu isipoharimishwa inakuwa halali. Uchaguzi wa marudio wa Zanzibar, japo ulisababishwa na sababu batil, na haramu, kwa vile hazikubatilishwa, wala kuharimishwa, then ukageuka ni uchaguzi halali, huru na wa haki, na aliyechaguliwa ni rais halali wa Zanzibar, uchaguzi mwingine ni hadi 2020!.
Pasco