Pasco ulipozaliwa umeoshwa kwa jimbo gani? Una Ubishi wa Kizanaki hasa!Ikiwa watu milioni 50 wanawadhibiti watu milioni moja(Ratio 50:1)hapo kuna ubakaji au mauaji. UsizungumzIe jambo la kufikirika,hubiri jambo la kuepukika. Jiulize chama gani kinacho historia ya fujo na mauaji Zanzibar? Kuanzia mauaji ya 1964, kuja kwa mauaji ya 2001, kuja kwa fujo za Janjaweed, Mazombie na hatimae Jecha. Unataka nini kitokee kingine kikufurahishe? Alioumwa na nyoka akiona ukoka hushituka! Damu ya wazanzibari ni lulu(most Precious),ni zaidi ya Jecha,ni zaidi ya CCM.
Sijui Pasco mungu gani aniemuabudu, mungu ambaye yuko, flexible,anaye yumbishika,mtia ulimi puani mwake.Tofauti na Mungu wangu mimi ana msimamo, batili huendelea kuwa batili, haramu huwa haramu hata ukitekelezwa na Alhaj kama Jecha na wala haihitaji sala, vurugu, maandamano,kubatilishwa au kuharamishwa mara ya pili.
Wakati wakereketwa na watawala wakisheherekea tukio hilo, Alhaj Jecha anazidi kuwa mpweke,mashakani kwa kusumbuliwa, kusutwa na nafsi yake mwenyewe.Kapotezewa uhuru wake , furaha, kuchanganyika na waumuni wenzake na aliowazoea, kutembea au kutembelewa. Kwa ufupi amekuwa kama sawa na kigoriwa kizamani wa kitumbatu ambae hatoki ndani zaidi ya kuchungulia dirishani akiomba kutokea mchumba wa kuja kumposa!