Msweet
JF-Expert Member
- Mar 26, 2014
- 3,241
- 4,445
Mshana jr, asante sana kaka kwa elimu hii. Nakwambia kuna jamaa mmoja alimkopesha jirani yake shs laki 7 akataka apewe hati ya nyumba kama dhamana, kwa vile mkopaji alikua na shida kuubwa maana mkewe alikua mahututi anahitaji pesa amsafirishe akatibiwe Muhimbili, akakubali, wakaandikishana ila akamuwekea riba asilimia 50% ya mkopo, baba wa watu akasaini huyo akamkimbiza mkewe Dar, muda wa kurejesha jamaa bado yupo Dar anauguza, akajulishwa kuwa nyumba yake itakua si yake tena kwa muda wa wiki moja maana makubaliano yamekiukwa. Baba akaomba aongezewe muda atalipa pesa zote na kwamba hali ya mkewe bado si nzuri na hawezi muacha, weeee jamaa akaweka ma broker, wacha wamtishe yule baba, masikini hadi akapata stroke nae akalazwa nyumba mwenye hela zake kajibebea. Hii ilinihuzunisha saana, ila walitokea wasamalia wema wakaingilia kati sakata hili, jamaa akalipwa pesa zake nyumba ikabaki. Lakin nahisi laana lazima impate mkopeshaji kwa vikwazo alivyomuwekea mwenzie.
Inasikitisha sana ....