Indigo28
JF-Expert Member
- Oct 27, 2020
- 232
- 475
- Thread starter
- #21
DEVIL’S FAMILY (FAMILIA YA MASHETANI) 08
ANGALIZO: KAMA UPO CHINI YA UMRI WA MIAKA 18. TAFADHALI USISOME HII HADITHI.
ILIPOISHIA
“Tusalimie kuzimu kwa maana sisi na wewe njia yetu ni moja”
Akatoa ishara na mzee Chiko akatupwa ndani ya bwawa la mamba na akaanza kushambuliwa kama walivyo shambuliwa wanaye.
“Moyo wangu sasa una amani na furaha. Jack chagua zawadi yoyote uniambie na nitakupatia”
Mama Jack akazitupa gloves ndani ya bwawa la mamba
“Nitakuambia mama”
“Sawa. Ahaa…..Mume wangu tuondoke”
Jack akawatazama wazazi wake wanao ondoka eneo hilo.
“Kila mmoja akampumzike kesho nina wahitaji sana katika harusi yangu. Kila mtu avalie suti na apendeze kama tulivyo kubaliana”
“Sawa mkuu”
Jack akapena tano na vijana wake na wakaondoka na kumuacha akiwa amesimama mwenyewe pembeni ya bwawa hilo. Ujumbe ukaingia katika simu yake na akafungua ujumbe huo ulio tumwa whatsapp. Akaiona picha ya msichana mrembo kisha akayasoma maandishi ulio ambatana na meseji hiyo.
‘Huyo ni mtoto wa Chiko. Yupo South Korea. Ni hataria sana, mshuhulikie kabla hajarudi nchini kwani akirudi vita yake sio ndogo’
ENDELEA
Jack kwa haraka akampigia mpasha habari.
“Mzee Chiko ana mtoto mwengine?”
“Ndio mkuu, na nina imani kwa kilicho tokea ni lazima ata kuja nchini Tanzania”
“Ana somea nini?”
“Upelelezi”
“Nini?”
“Ndio mkuu ana somea upelelezi”
“Fuc*** hembu hakikisha una nipatia taarifa za wapi ana soma na ni chuo gani na hata kama ana panga safari ya kurudi Tanzania basi hakikisha una jua ni ndege gani atakayo panda”
“Sawa mkuu”
Jack akakata simu, akatembea hadi ilipo nyumba ya eneo hilo la Mbugani.
“Wazee wameondoka?”
Alimuuliza mtunza mbuga ya wanyama
“Ndio boss”
Akaingia ndani ya gari moja na kuelekea moja kwa moja nyumbani kwao. Akafika, kabla ya kushuka ndani ya gari, akavua jaketi la kuzuia risasi, buti pamoja na glove ngumu alizo vaa viganjani mwake, akavaa kobazi zilizomo ndani ya gari, akashuka.
“Umemuona mzee?”
“Ndio wapo hapo sebleni na wageni”
Mfanyakazi mmoja alijibu. Akaingia sebleni na akamkuta baba yake akizungumza na katibu mkuu kutoka ikulu.
“Bwana harusi ndio huyu?”
“Ndio last born wangu”
Mzee Tiger alizungumza akitabasamu.
“Shikamoo”
“Marahaba. Habari za wewe?”
“Nina mshukuru sana MUNGU”
“Hongera sana kijana kwa kufanya maamuzi ya kuoa kwa maana vijana wengi katika kipindi chenu hichi muna ogopa sana kufunga ndoa”
“Hahahaa ni kweli”
“Nimekuja kuangalia mazingira kwa mara ya mwisho kwa maana taarifa ya kilicho tokea kidogo kilitushtua”
“Poleni sana”
“Asante sana.”
“Baba nipo ndani ukimaliza naomba tuonane”
“Sawa”
“Kama ni muhimu muna weza kuzungumza hivi sasa”
“Hapana muheshimiwa, ni mambo madogo madogo ya sherehe”
“Ohooo sawa”
Jack akaondoka sebleni huku katibu mkuu kiongozi pamoja na baba yake wakimtazama.
“Una kijana mkamavu sana. Nimeshikana naye mkono ila ni mzito kama komandooo”
“Huwa ana pendelea sana kufanya mazoezi”
“Kwa nini usimuingize serikalini katika vitengo vyetu vya ulinzi”
“Hahahaaa yeye ndio kila kitu kwa sasa. Una ona umri wangu umesha kimbia hivyo yeye ndio kiongozi wa kila kitu changu”
“Yule kaka yake si yupo?”
“Yupo ila yule bwana akili yake imejikita sana kwenye mambo ya kubuni buni vitu”
“Ohooo nakumbuka hata ule mfumo wa ulinzi wa kisasa alileta yeye ule mradi”
“Ndio ndio hivyo wamegawana majukumu”
“Safi sana”
“Jack Jack”
“Niambie sister”
“Kumeendaje?”
“Kila kitu kipo vizuri”
“Asante MUNGU umerudi salama. Nilikuwa nina jiuliza nita muelezaje Valentina kama kingekutokea chochote kibaya”
“Kuwa na amani sister. Wifi yako yupo wapi?”
“Katika wing wanayo kaa wazazi wake. Wana muandaa kwa ajili ya kesho”
“Sawa. Na ulio wafwata?”
“Wapo kwa sir God wana imba mapambio ya kusifu na kuabudu”
Jack akampiga piga dada yake begani na akaelekea chumbani kwake. Akapitiliza moja kwa moja bafuni, akavua nguo zote na akasimama chini ya bomba la maji ya mvua na kuanza kuoga. Akamaliza kuoga, akajifunga taulo kiunoni na akatoka bafuni, akapiga magoti pembezoni mwa kitanda anacho lala. Akachukua biblia na akaanza kuifungua, akasoma mistari kadhaa kisha akaanza kusali.
‘MUNGU asante kwa kila jambo. Mimi ni mkosefu na ni mwenye dhambi. Nina kuomba sana unisamehe dhambi zangu zote nilizo zifanya kwa kuwaza, kunena na kwa kutenda. Amen’
“Upo karibu sana na MUNGU wako”
Mzee Tiger alizungumza huku akiwa amekaa kwenye moja ya sofa huku ameweka nne.
“MUNGU ndio kila kitu baba. Haijalishi ni mangapi tuna yafanya chini ya hili jua ila yeye ana tusamehe”
“Vizuri. Ni nini ulitaka kuniambia?”
Jack akamchukua simu yake alipo iweka, juu ya meza ya kioo. Akaweka picha ya mtoto wa Chiko.
“Ni nani huyu?”
“Binti wa Chiko”
“Chiko ana mtoto wa kike?”
“Ndio mpasha habari ambaye ana fanya kazi na mzee Chiko ndio amenitumia hiyo picha”
“Bwana Chiko ana watoto watatu tu.”
“Baba wanaume tunapita sehemu nyingi. Huwezi jua ana weza kuwa ni binti yake nje ya ndoa. Tuachane na hayo ila kitu ambacho nimeelezwa kidogo ndio kina changamoto”
“Kitu gani?”
“Huyo binti ana soma South Korea maswala ya upelelezi”
“Ina maana ni mpelelezi?”
Mzee Tiger akaivuta karibu sura ya binti huyo mrembo.
“Ndio na jamaa ana seme ni hatari sana huyo binti. Mbaya ni kwamba sisi hatumjui vizuri kama tulivyo kuwa tuna wajua kaka zake”
“Duuu”
“Ndio baba. Ila nimemuambia jamaa anitafutie taarifa za chuo anacho kisoma. Na kwa kilicho tokea ni lazima ata katisha masomo yake na kuja huku hivyo akija ina tupasa kumshuhulikia mapema kabla hajapiga hatua kwenye upelezi wake”
“Hapana”
“Kwa nini baba….ikiwa ni watu hatari hao”
“Acha arudi, tujue ana fanya kazi katika chombo hani cha usalama hapa nchini. Kisha ndio tumshuhulikie. Ila tukimstukiza na akaponyoka basi ata jificha na akisha jificha basi ata tufikia kwa ukaribu”
Jack akamtazama baba kisha akatingisha kichwa akimaanisha kwamba amemuelewa baba yake.
“Tambua taarifa zake kisha unifahamishe”
“Sawa baba”
“Pumzika. Kesho una hitajika ukiwa na nguvu mpya na mwili umekuchangamka”
“Daaa kuna rafiki zangu sija onana nao na wamekuja kwa ajili yangu baba”
Mzee Tiger akatazama saa yake.
“Kaa nao walau nusu saa au saa moja kisha upumzike”
“Sawa mzee”
Taratibu mzee Tiger akanyanyuka.
“Baba”
“Naam”
“Kwa nini usimueleze ukweli mama?”
Mzee Tiger akatabasamu.
“Nina wasiwasi juu ya ulicho nieleza”
“Mama yako una jua presha zake. Nikimueleza hili basi yeye ndio ata kuwa mgonjwa. Ila wakati sahihi ukisha fika nita ieleza familia nzima”
“Sawa baba”
“Kuwa na amani na acha kunifikiria mimi. Fikiria kuhusiana na ndoa yako”
“Sawa baba”
Mzee Tiger akatoka chumbani kwa Jack. Jack akatembea hadi dirishani na akachungulia eneo la ufukwe wa bahari ambapo kuna bar ambayo rafiki zake na wageni wengine wapo. Akavaa nguo haraka haraka na akaelekea eneo walipo rafiki zake. Akasalimiana nao kwa kukumbatiana.
“Naona ndugu yetu umeamua kutukimbia kwenye ubachelor”
“Bakini humo acha mimi nikaone maisha ya ndoa yapoje?”
“Hakuna ambaye tuna muhoji na akasema kwamba maisha ya ndoa ni matamu”
“Doooo kila mtu na mtu wake bwana. Yakinishinda si natoka bwana”
Wote wakacheka.
“Vipi mumepata huduma nzuri?”
“Nzuri sana hata kwenye hoteli za nyota tano hatupati huduma kama hizi”
“Sawa sawa”
“Jack japo una ishi Tanzania ila maisha yako mazuri sana”
“Kwa nini?”
“Hili eneo ona lilivyo kubwa. Jumba la baba yako limejengwa kama ikulu ya Marekani tena ikulu ya Marekani ni ndogo ujue”
“Kwa mtu wan je ana weza kusema maisha ni mazuri sana ila kwa mimi kusema kweli nina ona ni maisha ya kawaida sana”
“Vipi hugongi maji siku hizi?”
“Kwa leo hapana. Nahitaji kukipambazuka akili yangu iwe vyema, nisije kuamka na hang over nikatia aibu kwenye sherehe.”
“Piga hata bia mbili mshikaji wetu”
“Hapana. Naomba munielewe hilo”
“Tuna heshimu mawazo yako bro”
Jack akamuona James akikatiza akielekea ndani.
“Samahani nina kuja”
Jack akanyanyuka na akamkimbilia James.
“Bro bro”
“Vipi, tumekutafuta hatujakupata?”
“Nilikuwa nina malizia kuunda mfumo mahari wa ulinzi kuanzia wa anga”
“Sawa kuna ishu naomba unisaidie”
“Ishu gani?”
Akamuonyesha picha ya mtoto wa Chiko.
“Nataka kupata taarifa za huyu binti”
“Ni nani?”
“Mtoto wa Chiko”
“Kwanza mumempata Chiko?”
“Yupo kuzimu kwa sasa”
“Weee”
“Na wanaye watatu wa kiume. Tuliwakuta kwenye kiota kimoja kama mandege John tukawabeba wote na wote wameliwa na mamba”
“Khaaa nani katoa oda ya wao kuliwa na mamba?”
“Bi mkubwa”
“Una jua tumezaliwa na shetani mdogo wangu……Wameliwa wakiwa hai au wamekufa”
“Wakiwa hai, tena Chiko akishuhudia mwanaye mmoja baada ya mwengine akiliwa kisha bi mkubwa akamkata makend** yake na mamba wakayala”
“Duuu”
“Sasa ana hatari gani?”
“Ana somea upelelezi South Korea hivyo ina bidi tujihami mapema”
“Nifwate”
Wakaelekea katika ofisi ya James.
“Yule dogo?”
“Nimemfungua kwenye chumba hapo kwanza akili imkae sawa”
“Sasa wa kazi gani si umuue”
“Hapana. Nahimuhitaji kwa kazi zangu”
“Kazi zako mtu kama yeye ni hatari bro. Ana weza kujifanya ni mnyenyekevu kwako na baadae akakugeuka kumbuka tumemchukua kwa njia ya kumteka”
“Usijali nitajua jinsi ya kucheza na akili yake”
James alizungumza huku akikaa katika kiti cha kuzunguka. Akawasha computer yake.
“So unataka kujua nini kuhusina ana yeye?”
“Nijui tu taarifa zake ambazo una weza kuzipata kwenye data base za serikali hususani kwenye majeshi huko”
“Ngoja niangalie”
“Halafu kuna kitu nilisahau kukusikilizisha”
Jack akamsikilizisha James mazungumzo ya mzee Chiko na wanaye.
“Umesikia wanasema wata leta drone zenye silaha zenye umbo la ndege?”
“Nimesikia ila hakuna kitakacho weza kuingia”
“Una uhakika?”
“Asilimia mia moja. Hapa nilikuwa nina fanya testing ya mfumo wa ulinzi wa anga pamoja na walinzi wa raisi kila kitu kipo vizuri”
“Sawa nitafutie huyu binti aisee ameninyima usingizi. Nilijua kwamba Chiko tumemmaliza kumbe kizazi chake bado kipo”
James akaanza kuifanya kazi aliyo pewa na mdogo wake. Hakumaliza dakika tano taarifa za mtoto wa kike wa Chiko zikapatikana.
“Anaitwa Rose Lupini…Mbona hana ubini wa Chiko?”
James aliuliza.
“Lupin ni kabila gani hilo?”
“Sijui dogo. Kuna koo zina majina ya ajabu. Muulize baba”
Jack akampigia baba yake.
“Ndio”
“Baba una fahamu jina la Lupini, lina husiana nini na Chiko?”
“Lupin ni ukoo wa marehemu mke wa Chiko mbona umeuliza?”
“Huyu mtoto wa Chiko ana itwa Rose Lupini ndio maana imekuwa ni ngumu kuweza kujua kama ana mtoto mwengine wa kike”
“Kwa nini alimficha huyo binti yake?”
“Sijui baba”
“Tafuta na ujue ukweli. Naanza kuiona hatari kama alivyo sema huyo mtu wako kuwa kuna hatari ina onekana mbeleni”
“Sawa baba”
James akakata simu na uendelea kusoma taarifa za Rose na kitu kilicho zidi kumchanganya yeye na kaka yake ni kuto kuona ni chombo gani cha ulinzi na usalama anacho fanyia kazi.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. Taratibu wameanza kujua taarifa za mtoto wa kike wa Chiko. Ni kwa nini mzee Chiko amemficha binti yake na ni kwa nini taarifa zake hazionyeshi ni wapi anapo fanyia kazi? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 09.
ANGALIZO: KAMA UPO CHINI YA UMRI WA MIAKA 18. TAFADHALI USISOME HII HADITHI.
ILIPOISHIA
“Tusalimie kuzimu kwa maana sisi na wewe njia yetu ni moja”
Akatoa ishara na mzee Chiko akatupwa ndani ya bwawa la mamba na akaanza kushambuliwa kama walivyo shambuliwa wanaye.
“Moyo wangu sasa una amani na furaha. Jack chagua zawadi yoyote uniambie na nitakupatia”
Mama Jack akazitupa gloves ndani ya bwawa la mamba
“Nitakuambia mama”
“Sawa. Ahaa…..Mume wangu tuondoke”
Jack akawatazama wazazi wake wanao ondoka eneo hilo.
“Kila mmoja akampumzike kesho nina wahitaji sana katika harusi yangu. Kila mtu avalie suti na apendeze kama tulivyo kubaliana”
“Sawa mkuu”
Jack akapena tano na vijana wake na wakaondoka na kumuacha akiwa amesimama mwenyewe pembeni ya bwawa hilo. Ujumbe ukaingia katika simu yake na akafungua ujumbe huo ulio tumwa whatsapp. Akaiona picha ya msichana mrembo kisha akayasoma maandishi ulio ambatana na meseji hiyo.
‘Huyo ni mtoto wa Chiko. Yupo South Korea. Ni hataria sana, mshuhulikie kabla hajarudi nchini kwani akirudi vita yake sio ndogo’
ENDELEA
Jack kwa haraka akampigia mpasha habari.
“Mzee Chiko ana mtoto mwengine?”
“Ndio mkuu, na nina imani kwa kilicho tokea ni lazima ata kuja nchini Tanzania”
“Ana somea nini?”
“Upelelezi”
“Nini?”
“Ndio mkuu ana somea upelelezi”
“Fuc*** hembu hakikisha una nipatia taarifa za wapi ana soma na ni chuo gani na hata kama ana panga safari ya kurudi Tanzania basi hakikisha una jua ni ndege gani atakayo panda”
“Sawa mkuu”
Jack akakata simu, akatembea hadi ilipo nyumba ya eneo hilo la Mbugani.
“Wazee wameondoka?”
Alimuuliza mtunza mbuga ya wanyama
“Ndio boss”
Akaingia ndani ya gari moja na kuelekea moja kwa moja nyumbani kwao. Akafika, kabla ya kushuka ndani ya gari, akavua jaketi la kuzuia risasi, buti pamoja na glove ngumu alizo vaa viganjani mwake, akavaa kobazi zilizomo ndani ya gari, akashuka.
“Umemuona mzee?”
“Ndio wapo hapo sebleni na wageni”
Mfanyakazi mmoja alijibu. Akaingia sebleni na akamkuta baba yake akizungumza na katibu mkuu kutoka ikulu.
“Bwana harusi ndio huyu?”
“Ndio last born wangu”
Mzee Tiger alizungumza akitabasamu.
“Shikamoo”
“Marahaba. Habari za wewe?”
“Nina mshukuru sana MUNGU”
“Hongera sana kijana kwa kufanya maamuzi ya kuoa kwa maana vijana wengi katika kipindi chenu hichi muna ogopa sana kufunga ndoa”
“Hahahaa ni kweli”
“Nimekuja kuangalia mazingira kwa mara ya mwisho kwa maana taarifa ya kilicho tokea kidogo kilitushtua”
“Poleni sana”
“Asante sana.”
“Baba nipo ndani ukimaliza naomba tuonane”
“Sawa”
“Kama ni muhimu muna weza kuzungumza hivi sasa”
“Hapana muheshimiwa, ni mambo madogo madogo ya sherehe”
“Ohooo sawa”
Jack akaondoka sebleni huku katibu mkuu kiongozi pamoja na baba yake wakimtazama.
“Una kijana mkamavu sana. Nimeshikana naye mkono ila ni mzito kama komandooo”
“Huwa ana pendelea sana kufanya mazoezi”
“Kwa nini usimuingize serikalini katika vitengo vyetu vya ulinzi”
“Hahahaaa yeye ndio kila kitu kwa sasa. Una ona umri wangu umesha kimbia hivyo yeye ndio kiongozi wa kila kitu changu”
“Yule kaka yake si yupo?”
“Yupo ila yule bwana akili yake imejikita sana kwenye mambo ya kubuni buni vitu”
“Ohooo nakumbuka hata ule mfumo wa ulinzi wa kisasa alileta yeye ule mradi”
“Ndio ndio hivyo wamegawana majukumu”
“Safi sana”
“Jack Jack”
“Niambie sister”
“Kumeendaje?”
“Kila kitu kipo vizuri”
“Asante MUNGU umerudi salama. Nilikuwa nina jiuliza nita muelezaje Valentina kama kingekutokea chochote kibaya”
“Kuwa na amani sister. Wifi yako yupo wapi?”
“Katika wing wanayo kaa wazazi wake. Wana muandaa kwa ajili ya kesho”
“Sawa. Na ulio wafwata?”
“Wapo kwa sir God wana imba mapambio ya kusifu na kuabudu”
Jack akampiga piga dada yake begani na akaelekea chumbani kwake. Akapitiliza moja kwa moja bafuni, akavua nguo zote na akasimama chini ya bomba la maji ya mvua na kuanza kuoga. Akamaliza kuoga, akajifunga taulo kiunoni na akatoka bafuni, akapiga magoti pembezoni mwa kitanda anacho lala. Akachukua biblia na akaanza kuifungua, akasoma mistari kadhaa kisha akaanza kusali.
‘MUNGU asante kwa kila jambo. Mimi ni mkosefu na ni mwenye dhambi. Nina kuomba sana unisamehe dhambi zangu zote nilizo zifanya kwa kuwaza, kunena na kwa kutenda. Amen’
“Upo karibu sana na MUNGU wako”
Mzee Tiger alizungumza huku akiwa amekaa kwenye moja ya sofa huku ameweka nne.
“MUNGU ndio kila kitu baba. Haijalishi ni mangapi tuna yafanya chini ya hili jua ila yeye ana tusamehe”
“Vizuri. Ni nini ulitaka kuniambia?”
Jack akamchukua simu yake alipo iweka, juu ya meza ya kioo. Akaweka picha ya mtoto wa Chiko.
“Ni nani huyu?”
“Binti wa Chiko”
“Chiko ana mtoto wa kike?”
“Ndio mpasha habari ambaye ana fanya kazi na mzee Chiko ndio amenitumia hiyo picha”
“Bwana Chiko ana watoto watatu tu.”
“Baba wanaume tunapita sehemu nyingi. Huwezi jua ana weza kuwa ni binti yake nje ya ndoa. Tuachane na hayo ila kitu ambacho nimeelezwa kidogo ndio kina changamoto”
“Kitu gani?”
“Huyo binti ana soma South Korea maswala ya upelelezi”
“Ina maana ni mpelelezi?”
Mzee Tiger akaivuta karibu sura ya binti huyo mrembo.
“Ndio na jamaa ana seme ni hatari sana huyo binti. Mbaya ni kwamba sisi hatumjui vizuri kama tulivyo kuwa tuna wajua kaka zake”
“Duuu”
“Ndio baba. Ila nimemuambia jamaa anitafutie taarifa za chuo anacho kisoma. Na kwa kilicho tokea ni lazima ata katisha masomo yake na kuja huku hivyo akija ina tupasa kumshuhulikia mapema kabla hajapiga hatua kwenye upelezi wake”
“Hapana”
“Kwa nini baba….ikiwa ni watu hatari hao”
“Acha arudi, tujue ana fanya kazi katika chombo hani cha usalama hapa nchini. Kisha ndio tumshuhulikie. Ila tukimstukiza na akaponyoka basi ata jificha na akisha jificha basi ata tufikia kwa ukaribu”
Jack akamtazama baba kisha akatingisha kichwa akimaanisha kwamba amemuelewa baba yake.
“Tambua taarifa zake kisha unifahamishe”
“Sawa baba”
“Pumzika. Kesho una hitajika ukiwa na nguvu mpya na mwili umekuchangamka”
“Daaa kuna rafiki zangu sija onana nao na wamekuja kwa ajili yangu baba”
Mzee Tiger akatazama saa yake.
“Kaa nao walau nusu saa au saa moja kisha upumzike”
“Sawa mzee”
Taratibu mzee Tiger akanyanyuka.
“Baba”
“Naam”
“Kwa nini usimueleze ukweli mama?”
Mzee Tiger akatabasamu.
“Nina wasiwasi juu ya ulicho nieleza”
“Mama yako una jua presha zake. Nikimueleza hili basi yeye ndio ata kuwa mgonjwa. Ila wakati sahihi ukisha fika nita ieleza familia nzima”
“Sawa baba”
“Kuwa na amani na acha kunifikiria mimi. Fikiria kuhusiana na ndoa yako”
“Sawa baba”
Mzee Tiger akatoka chumbani kwa Jack. Jack akatembea hadi dirishani na akachungulia eneo la ufukwe wa bahari ambapo kuna bar ambayo rafiki zake na wageni wengine wapo. Akavaa nguo haraka haraka na akaelekea eneo walipo rafiki zake. Akasalimiana nao kwa kukumbatiana.
“Naona ndugu yetu umeamua kutukimbia kwenye ubachelor”
“Bakini humo acha mimi nikaone maisha ya ndoa yapoje?”
“Hakuna ambaye tuna muhoji na akasema kwamba maisha ya ndoa ni matamu”
“Doooo kila mtu na mtu wake bwana. Yakinishinda si natoka bwana”
Wote wakacheka.
“Vipi mumepata huduma nzuri?”
“Nzuri sana hata kwenye hoteli za nyota tano hatupati huduma kama hizi”
“Sawa sawa”
“Jack japo una ishi Tanzania ila maisha yako mazuri sana”
“Kwa nini?”
“Hili eneo ona lilivyo kubwa. Jumba la baba yako limejengwa kama ikulu ya Marekani tena ikulu ya Marekani ni ndogo ujue”
“Kwa mtu wan je ana weza kusema maisha ni mazuri sana ila kwa mimi kusema kweli nina ona ni maisha ya kawaida sana”
“Vipi hugongi maji siku hizi?”
“Kwa leo hapana. Nahitaji kukipambazuka akili yangu iwe vyema, nisije kuamka na hang over nikatia aibu kwenye sherehe.”
“Piga hata bia mbili mshikaji wetu”
“Hapana. Naomba munielewe hilo”
“Tuna heshimu mawazo yako bro”
Jack akamuona James akikatiza akielekea ndani.
“Samahani nina kuja”
Jack akanyanyuka na akamkimbilia James.
“Bro bro”
“Vipi, tumekutafuta hatujakupata?”
“Nilikuwa nina malizia kuunda mfumo mahari wa ulinzi kuanzia wa anga”
“Sawa kuna ishu naomba unisaidie”
“Ishu gani?”
Akamuonyesha picha ya mtoto wa Chiko.
“Nataka kupata taarifa za huyu binti”
“Ni nani?”
“Mtoto wa Chiko”
“Kwanza mumempata Chiko?”
“Yupo kuzimu kwa sasa”
“Weee”
“Na wanaye watatu wa kiume. Tuliwakuta kwenye kiota kimoja kama mandege John tukawabeba wote na wote wameliwa na mamba”
“Khaaa nani katoa oda ya wao kuliwa na mamba?”
“Bi mkubwa”
“Una jua tumezaliwa na shetani mdogo wangu……Wameliwa wakiwa hai au wamekufa”
“Wakiwa hai, tena Chiko akishuhudia mwanaye mmoja baada ya mwengine akiliwa kisha bi mkubwa akamkata makend** yake na mamba wakayala”
“Duuu”
“Sasa ana hatari gani?”
“Ana somea upelelezi South Korea hivyo ina bidi tujihami mapema”
“Nifwate”
Wakaelekea katika ofisi ya James.
“Yule dogo?”
“Nimemfungua kwenye chumba hapo kwanza akili imkae sawa”
“Sasa wa kazi gani si umuue”
“Hapana. Nahimuhitaji kwa kazi zangu”
“Kazi zako mtu kama yeye ni hatari bro. Ana weza kujifanya ni mnyenyekevu kwako na baadae akakugeuka kumbuka tumemchukua kwa njia ya kumteka”
“Usijali nitajua jinsi ya kucheza na akili yake”
James alizungumza huku akikaa katika kiti cha kuzunguka. Akawasha computer yake.
“So unataka kujua nini kuhusina ana yeye?”
“Nijui tu taarifa zake ambazo una weza kuzipata kwenye data base za serikali hususani kwenye majeshi huko”
“Ngoja niangalie”
“Halafu kuna kitu nilisahau kukusikilizisha”
Jack akamsikilizisha James mazungumzo ya mzee Chiko na wanaye.
“Umesikia wanasema wata leta drone zenye silaha zenye umbo la ndege?”
“Nimesikia ila hakuna kitakacho weza kuingia”
“Una uhakika?”
“Asilimia mia moja. Hapa nilikuwa nina fanya testing ya mfumo wa ulinzi wa anga pamoja na walinzi wa raisi kila kitu kipo vizuri”
“Sawa nitafutie huyu binti aisee ameninyima usingizi. Nilijua kwamba Chiko tumemmaliza kumbe kizazi chake bado kipo”
James akaanza kuifanya kazi aliyo pewa na mdogo wake. Hakumaliza dakika tano taarifa za mtoto wa kike wa Chiko zikapatikana.
“Anaitwa Rose Lupini…Mbona hana ubini wa Chiko?”
James aliuliza.
“Lupin ni kabila gani hilo?”
“Sijui dogo. Kuna koo zina majina ya ajabu. Muulize baba”
Jack akampigia baba yake.
“Ndio”
“Baba una fahamu jina la Lupini, lina husiana nini na Chiko?”
“Lupin ni ukoo wa marehemu mke wa Chiko mbona umeuliza?”
“Huyu mtoto wa Chiko ana itwa Rose Lupini ndio maana imekuwa ni ngumu kuweza kujua kama ana mtoto mwengine wa kike”
“Kwa nini alimficha huyo binti yake?”
“Sijui baba”
“Tafuta na ujue ukweli. Naanza kuiona hatari kama alivyo sema huyo mtu wako kuwa kuna hatari ina onekana mbeleni”
“Sawa baba”
James akakata simu na uendelea kusoma taarifa za Rose na kitu kilicho zidi kumchanganya yeye na kaka yake ni kuto kuona ni chombo gani cha ulinzi na usalama anacho fanyia kazi.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. Taratibu wameanza kujua taarifa za mtoto wa kike wa Chiko. Ni kwa nini mzee Chiko amemficha binti yake na ni kwa nini taarifa zake hazionyeshi ni wapi anapo fanyia kazi? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 09.