Devid Mranda wa TPA achia ngazi

Devid Mranda wa TPA achia ngazi

kalanjadd

Member
Joined
Oct 16, 2011
Posts
39
Reaction score
16
Waziri Mwakyembe kafanya jambo kubwa na zuri sana kuwasimamisha kazi wakurugenzi Mgawe,Koshuma,Mfuko na menejea wa bandari bwana Ngamilo kwani hawa ni walikuwa ni tatizo, ila bado kuna tatizo kubwa lingine inapaswa kufanyika haraka la sivyo kila siku uharibifu utaendelea, huyu mkuu wa usalama wa bandari bwana Devid Mranda anapaswa kuondolewa haraka kwani wizi wote unafanyika yeye yuko hapo anashuhudia na kuubariki na hatari sana kwa kwa muda mchache alioko hapo amekuwa tajiri kupindukia akimiliki mahotel,maduka ya vifaa vya ujenzi na Nguo eneo la kariakoo na mwenge

Tunakuomba waziri Mwakyembe muondoe haraka fisadi huyu hana afanyalo ni kuharibu tu.
 
Mranda namjua huyo hafai kabisaaaaaaaaaaaaaa anzeni kumfungia ofisi abaki nje ya geti fisadi mkubwa huyo kibaraka wa Efraem Mgawe yuko hapo kwa umbea kuuza maneno na kusaidia wizi wa makontena
 
Kama hao akina Mgawe walisimamishwa kwa uharifbifu huku huyo Mranda akiwa mkuu wa usalama wa bandari, ni mantiki gani naye asiwajibishwe biblia inasema kilichozaliwa na roho ni roho na kilichozaliwa na mwili ni mwili maadamu akina Mgawe walifanya ufisaid huku Mranda yupo bila shaka nae ni fisadi, ili kujenga uadilifu atimuliwe haraka akiwezekana yeye na hao akina Mgawe waburuzwe mahakamani.
 
Aondolewe tu japo hakutamaliza tatizo kwa sababu tatizo lililopo ni la kimfumo zaidi.
 
Hii laana sijui itaishaje TANZANIA? wizi kila mahali!! akamatwe na afikishwe mahakamani.kumbe PRESIDENT KAGAME alikuwa anasema kweli.
 
Bandarini ni uozo mtupu, halafu sasa hivi kuna mgomo baridi wa kutekeleza majuku . Juzi kati nilimnukuu mfanyakazi mmoja sikuweza kumtambua jina lake akisema "Huko pameshachafuka tayari" hapo akiondoa gari yake kwa kasi kutoka kazini ambapo alitakiwa a-sign izinisho la kutoa magari pale bandarini!!!

PAMEOZA BALAA PALE MAHALA...!
 
Kwani hao walioondolewa wameshafikishwa kwa pilato tayari?mbona hii nchi usanii mwingi sana
vp yule mkurugenzi wa TBS,ooh i forgot wa TANESCO?vipi EPA?
Mwee ukiyafikiria ya hii nchi unaweza pelekwa milembe
 
Mranda namjua tangu 1978 alikuwa pale Ilemelamwanza dili zake ilikuwa kulahgua sukari enzi za ukata wa bidhaa hiyo, sijui uadilifu wa kupewa majukumu makubwa kama hayo hapo bandari aliyapataje!!!!?
 
Kuwatimua haitoshi wafikishwe mahakani na wafilisiwe.
 
Kuwatimua haitoshi wanatakiwa wafikishwe mahakamani na wafilisiwe.
 
Jamani wana jamvi si taratibu atatoka huyo secuirty manager kama wametoka wakuu wake na yeye atafuata na sina uhakika kama waziri ana mamlaka ya moja kwa moja kumuondoa huyo, hivyo itafika zamu yake soon
 
Waziri Mwakyembe kafanya jambo kubwa na zuri sana kuwasimamisha kazi wakurugenzi Mgawe,Koshuma,Mfuko na menejea wa bandari bwana Ngamilo kwani hawa ni walikuwa ni tatizo, ila bado kuna tatizo kubwa lingine inapaswa kufanyika haraka la sivyo kila siku uharibifu utaendelea, huyu mkuu wa usalama wa bandari bwana Devid Mranda anapaswa kuondolewa haraka kwani wizi wote unafanyika yeye yuko hapo anashuhudia na kuubariki na hatari sana kwa kwa muda mchache alioko hapo amekuwa tajiri kupindukia akimiliki mahotel,maduka ya vifaa vya ujenzi na Nguo eneo la kariakoo na mwenge

Tunakuomba waziri Mwakyembe muondoe haraka fisadi huyu hana afanyalo ni kuharibu tu.

TAKUKURUPUKA MKO WAPI KAMA MLIKUWA HAMJUI BASI MMEJULISHWA.
Inaeweka dhahiri kuwa katika maeneo nyeti huwa mnasheheni vyombo vya usalama lakini cha ajabu uovu wote na malalamiko yote yanayohusu uovu huo, vyombo hivyo vyote vimenyamaza kimya mpaka waziri aibue madudu hayo jee nyie mnafanya nini?
 
ndio upumbavu ulioniNIFANYA NITUKANE JANA PALE ROSEGARDEN WAKATI WAKIMSIFIA NA TRENI YAKE NKAWAAMBIA WASHENZI WENGI WA KUONDOA TPA WAMEBAKI TENA KWA KUJULIKANA SASA UNAPIGA KELELE YA WIZI UNAONDOA MKURUGENZI UNAACHA MKUU WA USALAMA ANAELINDA SI USHENZI HUO NA UZANDIKI...SIJUI NCHI INAPOELEKEA ILA NASHAURI HIVI VIJISIFA MNAVYOVITOA AVITAGUSA UKWELI WA MOYO WA MH MREMA AKIWA KAZINI ..MREMA KAMA NI MWIZI ANAONDOA HAPO HAPO NA GAMBA LA POLISI UNARUDISHA LEO WENGINE ATI WAKO UCHUNGUZINI HUKU UCHUNGUZINI WANALALA AKITANDA GANI KILA MTU ANAKIMBILIA UCHUNGUZI
 
Tusipoteze muda na gharama za kuwapeleka mahakamani,hakuna lolote litakaloendelea zaidi ya wao kushinda kesi,

Dawa ni SISIEM tu waondoke madarakani na vibaraka wao,hakuna muda tena wa kupoteza.
 
natumaini ujumbe umemfikia mwakyembe....mranda aondoke na aondoke sasa hivi...safisha bandari nzima tumeshaonewa sana huko bandarini...ni zamu yao kuonja joto la jiwe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom