kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
KATIKA hali ambayo isiyo ya kawaida askari wa Usalama barabarani (trafiki) wa kituo cha Gerezani manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam, amemtwanga makofi dereva wa gari hadharani kwa kile kilichodaiwa alikiuka taratibu za barabarani.
Tukio hilo la aina yake lilitokea eneo la gerezani leo ambapo dereva huyo alikuwa akiendesha gari dogo aina ya Pick-up lenye namba za usajili T 595 BMR.
Askari huyo ameshuhudiwa na watu waliokuwa karibu na maeneo hayo ikiwemo nifahamishe akifungua mlango wa gari hilo na kumtwanga makopfi dereva huyo ambaye djina lake halikuweza kupatikana mara moja mara baada ya dereva huyo kukaidi kusimama wakati aliposimamsihwa na askari huyo na kuendelea kuendesha gari yake.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Mohamed Mpinga amesema dereva huyo alikamatwa hapo kwa kuwa alipokuwa akitokea barabara ya Nyerere eneo la Tazara alitanua njia na aliposimamishwa hakusimama na alipofika eneo la mataa ya Kamata ndipo alikamatwa baada ya askari kupigiana simu.
Hata hivyo Kamanda huyo alisema ataendelea kutoa taarifa zaidi kuhusiana na tukio hilo
Tukio hilo la aina yake lilitokea eneo la gerezani leo ambapo dereva huyo alikuwa akiendesha gari dogo aina ya Pick-up lenye namba za usajili T 595 BMR.
Askari huyo ameshuhudiwa na watu waliokuwa karibu na maeneo hayo ikiwemo nifahamishe akifungua mlango wa gari hilo na kumtwanga makopfi dereva huyo ambaye djina lake halikuweza kupatikana mara moja mara baada ya dereva huyo kukaidi kusimama wakati aliposimamsihwa na askari huyo na kuendelea kuendesha gari yake.
Hata hivyo Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Mohamed Mpinga amesema dereva huyo alikamatwa hapo kwa kuwa alipokuwa akitokea barabara ya Nyerere eneo la Tazara alitanua njia na aliposimamishwa hakusimama na alipofika eneo la mataa ya Kamata ndipo alikamatwa baada ya askari kupigiana simu.
Hata hivyo Kamanda huyo alisema ataendelea kutoa taarifa zaidi kuhusiana na tukio hilo