Depo inakuaje huko CCP Moshi

Depo inakuaje huko CCP Moshi

Madem...hasa kuruta wenzako usijiushishe....maana km kuna afande nae kampenda utakokona mpk mwisho, mazoezi sio magumu, mchakamchaka sala ya asubuhi saa10 bigula hupigwa lenye tone ""Hukuja kulala ! hukuja kulala:"", kama huna ujuzi unafikiri unaweza tumika basi ni shushi mbaya..utakwepa fatiki zisizo na maana na kutesana...ujuzi kama "mwanamichezo soka, handball, & volleyball etc., ufundi km unao umeme, magari....unaweza pata kitengo ukiwa depo....lakini pia kupunguza stress kwa masuala mateso hapo na mawazo ficha makucha yako kwa kipindi chote kama kujiunga na vikundi vya dini ( kwa dhehebu lako) kuna kusali, kuimba, hapo inasaidia kupata marafiki hii mara nying watu wanafanya hiv wapite hapoo duh wakisha Passout wako kazini utawakimbia pombe madem zinaanza.... but kumbuka " Kumaliza ukuruta kweli ni kaaazi kubwa hata ndege wa angani watakushigilia" duh huu wimbo uimbwa sana kule......!!!! some Hints but ni uzoefu wangu wa depo ya zamani sana sana......hapo kamishna harun Mahundi....sijui sasa hivi lakin zingatia hayo dogo..sisi tulitupa gwanda chini kitambo sana...
 
kaka mkubwa hapo juu ameongea vizuri sana expirience yake mm nineenda karibuni na nmeshaenda depo mara 2..ya recruit na ya inspectorate na stil npo kwenye hii kampuni nikifundisha kwenye moja ya vyuo vya maafisa kama upo serious nipigie tuonane nikupe expirience vizuri na wat should u do.0717088069
 
Kwanza unatakiwa kuwa na nia hyo itakusaidia kiwa mvumilivu
Nidhamu ya hali ya juu sn
Usiwe na kiherehere
Ushirikiano na wenzako
Mengne utayaona hukohuko nakuyakabil lkn lazma uwe na NIA kwanza la cvyo upara tu unakukmbza
Mengne km ya jkt tu
 
Sasa kama mafunzo yenyewe ndio haya halafu polisi hawawezi kushika hata mwizi mmoja wanaishia kubambikiza kesi na kudai rushwa mabarabatani hicho chuo si kifungwe tu? Hovyo Pathetic
 
huwaga hatuingii jamii forum tupo bize kulipua mabomu ya machozi hata tukipata muda wakati wa kulinda bank bundle huwa linazingua
 
polisi mbona shumbwela ,chenja kimtindo na vizoez vya hapa na pale .njoo kiumeni ushone na kutulia pushup hazna idadi ,msosi huwez shiba full vijogoo ,ukiwa namba WA kwata unaweza achia nyoya. much respect tpdf
 
Mi nilikuwa huko miaka kama 10 nikitumikia jeshi. Nilichokiona na kibaya hasa kwa makuruta though si wote wengi wao ni sawa na genge la wahalifu. Yaani walioshindwa life mtaani. Mzizi wa jeshi la polisi kuwa na mtazamo hasi toka kwa jamii ni hapa.

Mafunzo yanayotolewa ni mazuri sana na wala sijutii kwa nini nilijiunga na na jeshi hilo japo nilikuja jiondoa kwa sababu nyingine kabisa. Sasa nije ktk mafunzo yenyewe; kwanza haya ni mafunzo maalum kuyajua kabla haikusaidii kitu kwa kuwa kila kuruta ana tabia zake za asili.

Pili heshima iwe ni zaidi ya mia mia bila kujali kama ni ya uoga au kwa mujibu wa taratibu. Hii ni muhimu sana kwani mara nyingi hii huwa sababu ya wengi kukimbia mafunzo (hata kukimbia pia iwe kwa siri la sivyo nao ni msala).

Heshima hiyo ni juu ya
Kuwa msafi muda wote na hasa master parade la kila siku asubuhi baada ya mchakmchaka wa saa tisa. Sasa wee uendelee kulala wakati buruji limepulizwá. Utajuta ukikutwa. (hapa namkumbuka sana afande mikwara ambaye kwa sasa hayupo tena ccp ila nina uhakika taarifa zake mtazipata tu).

Uvumilivu utasaidia kuondoka na unyeke (utaulizia unyeke ni nini ukifika ccp kisha utanijulisha) hapo ccp. Hapa pana mchakamchaka wa saa tisa usiku ukizingatia kulala ni saa nne usiku. Pili pana gwaride la kutosha kuujenga mwili. Ukiwa goigoi hapa wee utakuwa mtu ea kukaba siki kila siku na hili linaweza kukudababishia tifu siku noja na hasa ukimkuta afande asiyeelewaelewa. Kaulize pia haya maneno yanamaanisha nini. Gwaride linapigwa uwanja wa damu (nadhani uliitwa hivi kutokana na shughuli yake kuwa pevu. Sikuwahi kuambiwa kwa nini uliitwa hivyo). Ukubwawake ni wastani wa kama viwanja 10 - 12 vya soka.

Nakumbuka zilikuwepo kombania nne: A, B, C na kombania kuu. Usiombe ukapangiwa kombania ya maafande wanoko. Unaweza kukimbia depo.

Mambo ya kusimamisha minazi acha kabisa. Wee vhukua kufuli funga kwani kuna mawili. Utafukuzwa au utagongana na virusi. Haijslishi kama wote mmepima na kukutwa wazima. Ukumbuke kuna maafande nao huwagonga makuruta wa kike.

Kea mengi zaidi au part two utapewa baada ya mafunzo uyapate ya huku mtaani

The Listener
Ex Detective
 
Hakuna depo la kuogopa dogo! depo unaenda na pass ya kunyooshea nguo? uko ni urembo urembo tu na kufukuzana bila sababu
 
Hakuna depo la kuogopa dogo! depo unaenda na pass ya kunyooshea nguo? uko ni urembo urembo tu na kufukuzana bila sababu

ndugu yangu umenifanya nicheke saana asubuhi hii,eti depo unaenda pasi ya kunyooshea nfuo...
 
ndugu yangu umenifanya nicheke saana asubuhi hii,eti depo unaenda pasi ya kunyooshea nfuo...

Hahahahahahaha askari anakua smart bana unadhan hawana maana kuweka pasi hahahahaha ila hata mm jamaa kanichekesha saana aisee
 
Mi nilikuwa huko miaka kama 10 nikitumikia jeshi. Nilichokiona na kibaya hasa kwa makuruta though si wote wengi wao ni sawa na genge la wahalifu. Yaani walioshindwa life mtaani. Mzizi wa jeshi la polisi kuwa na mtazamo hasi toka kwa jamii ni hapa.

Mafunzo yanayotolewa ni mazuri sana na wala sijutii kwa nini nilijiunga na na jeshi hilo japo nilikuja jiondoa kwa sababu nyingine kabisa. Sasa nije ktk mafunzo yenyewe; kwanza haya ni mafunzo maalum kuyajua kabla haikusaidii kitu kwa kuwa kila kuruta ana tabia zake za asili.

Pili heshima iwe ni zaidi ya mia mia bila kujali kama ni ya uoga au kwa mujibu wa taratibu. Hii ni muhimu sana kwani mara nyingi hii huwa sababu ya wengi kukimbia mafunzo (hata kukimbia pia iwe kwa siri la sivyo nao ni msala).

Heshima hiyo ni juu ya
Kuwa msafi muda wote na hasa master parade la kila siku asubuhi baada ya mchakmchaka wa saa tisa. Sasa wee uendelee kulala wakati buruji limepulizwá. Utajuta ukikutwa. (hapa namkumbuka sana afande mikwara ambaye kwa sasa hayupo tena ccp ila nina uhakika taarifa zake mtazipata tu).

Uvumilivu utasaidia kuondoka na unyeke (utaulizia unyeke ni nini ukifika ccp kisha utanijulisha) hapo ccp. Hapa pana mchakamchaka wa saa tisa usiku ukizingatia kulala ni saa nne usiku. Pili pana gwaride la kutosha kuujenga mwili. Ukiwa goigoi hapa wee utakuwa mtu ea kukaba siki kila siku na hili linaweza kukudababishia tifu siku noja na hasa ukimkuta afande asiyeelewaelewa. Kaulize pia haya maneno yanamaanisha nini. Gwaride linapigwa uwanja wa damu (nadhani uliitwa hivi kutokana na shughuli yake kuwa pevu. Sikuwahi kuambiwa kwa nini uliitwa hivyo). Ukubwawake ni wastani wa kama viwanja 10 - 12 vya soka.

Nakumbuka zilikuwepo kombania nne: A, B, C na kombania kuu. Usiombe ukapangiwa kombania ya maafande wanoko. Unaweza kukimbia depo.

Mambo ya kusimamisha minazi acha kabisa. Wee vhukua kufuli funga kwani kuna mawili. Utafukuzwa au utagongana na virusi. Haijslishi kama wote mmepima na kukutwa wazima. Ukumbuke kuna maafande nao huwagonga makuruta wa kike.

Kea mengi zaidi au part two utapewa baada ya mafunzo uyapate ya huku mtaani

The Listener
Ex Detective

daaah umempa lonja za nguvu yeye aende tu kila kitu atakijua huko maadam amrfungua moyo acha aende by the way hongera bana kumbe ulikua CID safi sana so umebobea kwenye epstionage safi sana chief
 
daaah umempa lonja za nguvu yeye aende tu kila kitu atakijua huko maadam amrfungua moyo acha aende by the way hongera bana kumbe ulikua CID safi sana so umebobea kwenye epstionage safi sana chief

yaah. pande hizo nimebobea na wakati fulani kabla sijavunjwa moyo wa kuendelea na kazi hiyo nilipenda sana kwenda somea masuala zaidi juu ya major crime investigation. Nadhani dogo atakuwa kaupata huu ujumbe na ataufanyia kazi. Jana niliwaona vijana wengi wakiwa katika mabasi maeneo ya hapo train station nadhani ndo walikuwa wanaelekea huko kama sikosei. Na tena hiyo simu yake aifiche mbali sana kwani ni msala mwingine huo

The Listener
Ex Detective
 
kuhusu pasi unatakiwa unyooshe nguo kila siku ila pasi utaipata wapi utajua mwenyewe. Kama utakuwa unagongea kwa wenzako hiyo ni juu yako wewe mwenyewe ila ujue utakuwa kila siku unakuwa wa mwisho kujiandaa na masuala ya kupiga pasi hapo buti hujaring'arisha hadi liwe mithili ya kioo cha kujitazamia (wakati mwingine buti huwa linazima na huo ni uchafu pia).

Mimi nakumbuka nilinunua pasi kiatika duka la chuo na wewe nakushauri ufanye hivyo ili kuwa na peace of mind katika suala la kulinyoosha hilo guo. zamani tulitumia starch though nimesikia (sina uhakika) miaka hii hilo wameliona halina tija kwa makuruta.

kwa kuwa ulihitaji na some techniques nakupa ya kulivaa hilo suruali wakati wa kuelekea parade. Panda juu ya deka; kama si lako omba usije leta msala na wenzako kisha jinyooshe wakati unaingia katika hiyo suruali taratibu. hapa ni vyema uombe msaada kwa wenzako wakushikie hilo suruali wakati wewe unashuka taratibu toka juu. Hii ni muhimu kwani mikunjo ya nguo nayo inahesabika kama uchafu na tifu lake utalijua kama ukiamua siku moja kuamua kwenda parade kama RAMBO (OVYO OVYO KAMA YULE STAR ALIVYOKUWA ALIPOKUWA AKIPOKEA KICHAPO TOKA KWA MAADUI).

Dogo uliza tu utajuzwa. Kumbuka kuna shule ambayo kimsingi kama ni suala la muda linakaribiana kabisa na muda wa masuala ya parade

DAAAAAH. Dogo umenikumbusha mbali sana imenibidi nicheke sana nikikumbuka kuna kituko nilikifanya bila mtu kutambua na nikafanikiwa though wanaplatoon wenzangu walifaidika pia

The Listener
Ex Detective
 
Back
Top Bottom