Wafanyakazi wa Barrick miaka ile walikua wakidai haki zao za msingi, na hii ilitokea baada ya wafanyakazi wa migodini kutambua haki zao ambazo walipaswa kuzipata kwenye mikataba ya mwanzo kabisa ambayo Barrick walikuja nayo Tz.
Baada ya watu wachache wenye tamaa wakishirikiana na Deo Mwanyika, walibadilisha mikataba ile na kuondoa baadhi ya vipengele ambavyo vilikuwa vikiwaongezea watumishi wa migodi ya Barrick Tz kupata umate umate wa haja kutokana na kazi ngumu/mazingira hatarishi.
Wafanyakazi wa Barrick Bully waliwahi kufanya mgomo kutokana na kifo cha mchimbaji kilicho tokana na mazingira tatanishi, na hiyo ni baada ya marehemu kuto onekana kwa muda wa siku kadhaa.... Deo Mwanyika alikuja akafanya mambo ya hovyo pamoja na kutoa kauli za kukatisha tamaa kabisa.
Deo huyu huyu ndie alie ishauri management vibaya na hata kupelekea kutokulipwa kwa vifo vya baadhi ya watumishi vilivyo tokea wakiwa ndani ya mgodi.
Deo Mwanyika alipenda kujinufaisha yeye binafsi na hata alifikia hatua ya kujiona kwamba yeye sio mTz mana hata mtu mweusi tena.
Sent using
Jamii Forums mobile app