Demokrasia na mila ni pacha

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,315
12,614
Angalia nyumbani kwenu, nyumbani kwako na kwenye familia yenu kama kuna demokrasia ya kiasi gani? Je, wazazi wamewapa watoto demokrasia ya kusema, kutenda na kuamua kiasi gani? Je, baba anaruhisiwa kumuoa mtoto wake? Je, baba anaweza kuvumilia matusi ya mtoto wake? Je, Binti anaweza kumleta boyfriend wake kwa wazazi bila shida? Je, mtoto anaweza kulala chumba cha wazazi wake? Je, watoto wanaweza kujivalia nguo yoyote? Je, mke na watoto wanarudi nyumbani muda wowote?

Demokrasia inaanzia ngazi ya familia. Demokrasia ni kama lugha, lugha isiyozungumzwa nyumbani kwenye familia haiwezi kuzungumzwa vizuri kwenye ngazi ya taifa; na demokrasia isiyotendwa kwa ufasaha kwenye ngazi ya familia haiwezi kutendwa kwa ufasaha kwenye ngazi ya kitaifa.

Ndiyo maana hutuwezi kuvumilia demokrasia ya kutukanana kwenye majukwaa kwakuwa huo sio utamaduni wetu huko majumbani tulikolelewa na tulikozaliwa na kukulia.

Maana majumbani hakuna demokrasia, chekechea hakukua na demokrasia, miaka 7 ya shule ya msingi hakukua na demokrasia shuleni, miaka 4 ya secondary hakuna demokrasia, miaka 2 ya A level wanafumzi hawana demokrasia na hata vyuoni hakuna demokrasia ya kusema, kuvaa, kunyoa, Wala kuahirisha mtihani, hivyo hata majukwaani hakuwezi kuwa na demokrasia pana kiasi hicho cha kuporomosha matusi hadharani bila kuulizwa ulitoa wapi hilo.

Tusiwe kama dodoki zoazoa wa demokrasia ya Magharibi na kuleta Huku kwetu kama ilivyo wakati background zetu ni tofauti sana na zao. Demokrasia ya Wazungu imeanzia kwenye ngazi ya familia, watoto wao hawana acha (don't) nyingi kama watoto wetu. Think globally and act locally.

Mwanasiasa msomi lazima analijua hili, kama ukimuona anatukana hadharani viongozi wake lazima analo lingine moyoni na kichwani zaidi ya siasa na demokrasia. Tumvunje kichwa chake mapema kabla hajavunja vichwa vyetu sote.
 
Angalia nyumbani kwenu, nyumbani kwako na kwenye familia yenu kama Kuna demokrasia ya kiasi gani. Je, wazazi wamewapa watoto demokrasia ya kusema, kutenda na kuamua kiasi gani? Je, baba anaruhisiwa kumuoa mtoto wake? Je, baba anaweza kuvulia matusi ya mtoto wake? Je, Binti anaweza kumleta boyfriend wake kwa wazazi bila shida? Je, mtoto anaweza kulala chumba Cha wazazi wake?

Demokrasia inaanzia ngazi ya familia. Demokrasia ni kama lugha, lugha isiyozungumzwa nyumbani kwenye familia haiwezi kuzungumzwa vizuri kwenye ngazi ya taifa; na demokrasia isiyotendwa kwa ufasaha kwenye ngazi ya familia haiwezi kutendwa kwa ufasaha kwenye ngazi ya kitaifa.

Ndiyo maana hutuwezi kuvumilia demokrasia ya kutukanana kwenye majukwaa kwakuwa huo sio utamaduni wetu huko majumbani tulikolelewa na tulikozaliwa na kukulia. Maana majumbani hakuna demokrasia, chekechea hakukua na demokrasia, miaka 7 ya shule ya msingi hakukua na demokrasia shuleni, miaka 4 ya secondary hakuna demokrasia, miaka 2 ya A level wanafumzi hawana demokrasia na hata vyuoni hakuna demokrasia ya kusema, kuvaa, kunyoa, Wala kuahirisha mtihani, hivyo hata majukwaani hakuwezi kuwa na demokrasia Pana kiasi hicho Cha kuporomosha matusi.

Tusiwe kama dodoki zoazoa wa demokrasia ya Magharibi na kuleta Huku kwetu kama ilivyo wakati background zetu ni tofauti sana. Demokrasia ya Wazungu imeanzia kwenye ngazi ya familia, watoto wao hawana acha (don't) nyingi kama watoto wetu. Think globally and act locally. Mwanasiasa msomi lazima analijua hili, kama ukimuona anatukana analo lingine moyoni na kichwani zaidi ya siasa na demokrasia. Tumvunje kichwa chake kabla hajavunja vichwa vyetu sote.
Bandiko bora kabisa asubuhi ya leo
 
Jirani yangu Mkurya kila uchao huwa anampiga mkewe na watoto mpaka nje ya nyumba yake.....

Ni mpenzi wa CHADEMA na kila uchao husema nchi haina demokrasia ,CCM ina uonevu,katiba iliyopo haina haki.....

Huyu bwana huwa ninamshangaa sana

#Never Give Wisdom To Unworthy As It Is Unjust To The Knowledgeable
 
Jirani yangu Mkurya kila uchao huwa anampiga mkewe na watoto mpaka nje ya nyumba yake.....

Ni mpenzi wa CHADEMA na kila uchao husema nchi haina demokrasia ,CCM ina uonevu,katiba iliyopo haina haki.....

Huyu bwana huwa ninamshangaa sana

#Never Give Wisdom To Unworthy As It Is Unjust To The Knowledgeable
Watu hawajui demokrasia maana yake nini, demokrasia inaanza na wewe na kuishia na wewe pia. Kama nyumbani unapiga mke na watoto kwa kosa la kuvaa nguo fupi na kuchelewa kurudi nyumbani unawezaje kudai demokrasia kama ya Magharibi? Hata Magharibi wanayo demokrasia ya utamaduni na mila zao za kibepari, kiuchumi wao na mazingira yao. Cha kushangaza Kuna Wazungu wengi wanaotamani demokrasia yetu ya kutumza wazee wetu majumbani mwetu, kununuliana vinywaji kwenye bars na tunavyoishi pamoja.

Shida yetu kubwa sio demokrasia bali watendaji wanaotuibia rasilimali zetu bila kuadhibiwa kwa kiwango sawa na kosa walilotenda. Tuna watu wasiofanyakazi sawasawa.
 
Watu hawajui demokrasia maana yake nini, demokrasia inaanza na wewe na kuishia na wewe pia. Kama nyumbani unapiga mke na watoto kwa kosa la kuvaa nguo fupi na kuchelewa kurudi nyumbani unawezaje kudai demokrasia kama ya Magharibi? Hata Magharibi wanayo demokrasia ya utamaduni na mila zao za kibepari, kiuchumi wao na mazingira yao. Cha kushangaza Kuna Wazungu wengi wanaotamani demokrasia yetu ya kutumza wazee wetu majumbani mwetu, kununuliana vinywaji kwenye bars na tunavyoishi pamoja.

Shida yetu kubwa sio demokrasia bali watendaji wanaotuibia rasilimali zetu bila kuadhibiwa kwa kiwango sawa na kosa walilotenda. Tuna watu wasiofanyakazi sawasawa.
Hakika....

Umemaliza kibusara

Yako waziiii wala hayahitaji TOCHI
 
Watu hawajui demokrasia maana yake nini, demokrasia inaanza na wewe na kuishia na wewe pia. Kama nyumbani unapiga mke na watoto kwa kosa la kuvaa nguo fupi na kuchelewa kurudi nyumbani unawezaje kudai demokrasia kama ya Magharibi? Hata Magharibi wanayo demokrasia ya utamaduni na mila zao za kibepari, kiuchumi wao na mazingira yao. Cha kushangaza Kuna Wazungu wengi wanaotamani demokrasia yetu ya kutumza wazee wetu majumbani mwetu, kununuliana vinywaji kwenye bars na tunavyoishi pamoja.

Shida yetu kubwa sio demokrasia bali watendaji wanaotuibia rasilimali zetu bila kuadhibiwa kwa kiwango sawa na kosa walilotenda. Tuna watu wasiofanyakazi sawasawa.
Huwezi kulifananisha taifa na familia.
 
Taifa sio mfano wa familia, mifano yako haina uhalisia.
Kwenye taifa kuna katiba kwenye familia hakuna katiba.
Hakuna Katiba inayotungwa tofauti na mila na desturi ya watu wake. Mfano, katiba haiwezi kuruhusu baba amuoe mtoto wake, au mtoto kuzaa na mama yake. Hakuna Katiba inayoruhusu demokrasia ya kumchinja mwanao kwakuwa ni mwanao.
 
Angalia nyumbani kwenu, nyumbani kwako na kwenye familia yenu kama Kuna demokrasia ya kiasi gani. Je, wazazi wamewapa watoto demokrasia ya kusema, kutenda na kuamua kiasi gani? Je, baba anaruhisiwa kumuoa mtoto wake? Je, baba anaweza kuvumilia matusi ya mtoto wake? Je, Binti anaweza kumleta boyfriend wake kwa wazazi bila shida? Je, mtoto anaweza kulala chumba Cha wazazi wake?

Demokrasia inaanzia ngazi ya familia. Demokrasia ni kama lugha, lugha isiyozungumzwa nyumbani kwenye familia haiwezi kuzungumzwa vizuri kwenye ngazi ya taifa; na demokrasia isiyotendwa kwa ufasaha kwenye ngazi ya familia haiwezi kutendwa kwa ufasaha kwenye ngazi ya kitaifa.

Ndiyo maana hutuwezi kuvumilia demokrasia ya kutukanana kwenye majukwaa kwakuwa huo sio utamaduni wetu huko majumbani tulikolelewa na tulikozaliwa na kukulia. Maana majumbani hakuna demokrasia, chekechea hakukua na demokrasia, miaka 7 ya shule ya msingi hakukua na demokrasia shuleni, miaka 4 ya secondary hakuna demokrasia, miaka 2 ya A level wanafumzi hawana demokrasia na hata vyuoni hakuna demokrasia ya kusema, kuvaa, kunyoa, Wala kuahirisha mtihani, hivyo hata majukwaani hakuwezi kuwa na demokrasia pana kiasi hicho cha kuporomosha matusi hadharani bila kuulizwa ulitoa wapi hilo.

Tusiwe kama dodoki zoazoa wa demokrasia ya Magharibi na kuleta Huku kwetu kama ilivyo wakati background zetu ni tofauti sana. Demokrasia ya Wazungu imeanzia kwenye ngazi ya familia, watoto wao hawana acha (don't) nyingi kama watoto wetu. Think globally and act locally. Mwanasiasa msomi lazima analijua hili, kama ukimuona anatukana hadharani viongozi wake lazima analo lingine moyoni na kichwani zaidi ya siasa na demokrasia. Tumvunje kichwa chake kabla hajavunja vichwa vyetu sote.
Kongole nyingi sana kwa bandiko litakaloishi kipindi kirefu sana bila kupoteza maana
 
Hakuna Katiba inayotungwa tofauti na mila na desturi ya watu wake. Mfano, katiba haiwezi kuruhusu baba amuoe mtoto wake, au mtoto kuzaa na mama yake. Hakuna Katiba inayoruhusu demokrasia ya kumchinja mwanao kwakuwa ni mwanao.
Mila na desturi za Africa zilikuwa ni Ufalme na Uchifu ila sasa hivi tuna Marais karibia bara lote, uarabuni sasa hivi kuna viongozi wanawake, Marekani watu weusi na wanawake wanapiga kura karne hii.

Human rights are universal, sio suala la mila na desturi za jamii fulani. Mambo mengine ni common sense na maendeleo ya ustaarabu wala sio suala la mila na desturi za jamii fulani. Duniani kote hakuna nchi inaruhusu watoto na wazazi kuoana au binadamu kuchinjana.
 
Angalia nyumbani kwenu, nyumbani kwako na kwenye familia yenu kama Kuna demokrasia ya kiasi gani. Je, wazazi wamewapa watoto demokrasia ya kusema, kutenda na kuamua kiasi gani? Je, baba anaruhisiwa kumuoa mtoto wake? Je, baba anaweza kuvumilia matusi ya mtoto wake? Je, Binti anaweza kumleta boyfriend wake kwa wazazi bila shida? Je, mtoto anaweza kulala chumba Cha wazazi wake?

Demokrasia inaanzia ngazi ya familia. Demokrasia ni kama lugha, lugha isiyozungumzwa nyumbani kwenye familia haiwezi kuzungumzwa vizuri kwenye ngazi ya taifa; na demokrasia isiyotendwa kwa ufasaha kwenye ngazi ya familia haiwezi kutendwa kwa ufasaha kwenye ngazi ya kitaifa.

Ndiyo maana hutuwezi kuvumilia demokrasia ya kutukanana kwenye majukwaa kwakuwa huo sio utamaduni wetu huko majumbani tulikolelewa na tulikozaliwa na kukulia. Maana majumbani hakuna demokrasia, chekechea hakukua na demokrasia, miaka 7 ya shule ya msingi hakukua na demokrasia shuleni, miaka 4 ya secondary hakuna demokrasia, miaka 2 ya A level wanafumzi hawana demokrasia na hata vyuoni hakuna demokrasia ya kusema, kuvaa, kunyoa, Wala kuahirisha mtihani, hivyo hata majukwaani hakuwezi kuwa na demokrasia pana kiasi hicho cha kuporomosha matusi hadharani bila kuulizwa ulitoa wapi hilo.

Tusiwe kama dodoki zoazoa wa demokrasia ya Magharibi na kuleta Huku kwetu kama ilivyo wakati background zetu ni tofauti sana. Demokrasia ya Wazungu imeanzia kwenye ngazi ya familia, watoto wao hawana acha (don't) nyingi kama watoto wetu. Think globally and act locally. Mwanasiasa msomi lazima analijua hili, kama ukimuona anatukana hadharani viongozi wake lazima analo lingine moyoni na kichwani zaidi ya siasa na demokrasia. Tumvunje kichwa chake kabla hajavunja vichwa vyetu sote.

Ndiyo maana watu wanahoji nani alisema western democracy is a universal democracy!?
 
Hakuna Katiba inayotungwa tofauti na mila na desturi ya watu wake. Mfano, katiba haiwezi kuruhusu baba amuoe mtoto wake, au mtoto kuzaa na mama yake. Hakuna Katiba inayoruhusu demokrasia ya kumchinja mwanao kwakuwa ni mwanao.
Mbona unaongea mambo obvious. Katiba ni framework haigusii specifics Kama unavyosema. Specifics zinaguswa na sheria. Huwezi kuta katiba inaongelea nani anaowa na nani haolewi, hiyo utaikuta kwenye sheria ya ndoa.
 
Taifa sio mfano wa familia, mifano yako haina uhalisia.
Kwenye taifa kuna katiba kwenye familia hakuna katiba.
Jamaa akili yake ni fupi sana,hajui kuwa mtoto huwa anakuwa chini ya mzazi kwasababu uwezo wake wakuchakata mambo bado ni mdogo yaan bado anakuwa ni mchanga kiakili hvyo huhitaji muongozo wa wazazi

Sasa kitaifa huku ni watu wazima na wana elimu kukuzidi huwez kuwaendesha kama unavyoendesha familia yako
 
Back
Top Bottom