Wataalam:
Unajua sisi wengine huwa delete ili Computer ipunguze mzigo, na mnaposema files zitaendelea kuwepo
ina maana ipo siku Computer itajaa kabisa (kwa maana ya capacity) yake, na hivyo kuhitaji hatua nyingine
kabisa.........................?
cc:
sijui nini,
Mlamoto
mkuu, fuatilia kwa makini comments zilizotolewa hapo juu zimejitosheleza kabisa...ni kwamba :
unapodelete file kwenda kwenye recycle bin ni sawa na ulimove tu kutoka lilipokuwa kwenda kwenye recycle bin..kwa hiyo ile nafasi iliyokuwa inatumiwa na faili lile inabadilika jina tu ila occuped space inabaki vilevile..
sasa unapoliondoa na kwenye recycle bin ni kwamba unafuta njia zote za hilo file kuwa opened again kwa njia ya kawaida na ile nafasi yake inakuwa marked kuwa empty adress (ingawa lile file lipo) na hii empty adress inaweza kutumika kwa kuhifadhi data zingine,
hivyo hili file ulilolifuta sasa linakuwa kwa lugha rahisi ni kama lipo hewani hivi linaelea(mahali maalum)...na linaweza kufunguliwa si kwa njia ile ya kawaida tena bali mpaka kwa program maalum ya kuweza kuliona ..
na upatikanaji wake unategemea na kadri unavyozidi kuingiza na kufuta mafaili mengine kwenye hdd yako maana kadri ya kuingiza na kufuta mafili yako ndvyo unavyozidi kulisukuma lile file la kwanza kuwa deletd kwenda mbalimbali zaidi na kupoteza uwezekano wa kulipata
(labda uzidi kutumia more powerful tools za ku restore) na ndo maana kuna mdau hapo juu alisema ikitokea bahati mbaya umedelete(empty recyecle bin au format) kitu unachokihitaji bado ni vema usiendelee kuitumia zaidi hiyo hdd kwanza maana restore programs nyingi zinaende kwa order ya time file lilipokuwa deteted...so likiwa mbali zaidi si ajabu program zetu hizi za kawaida za ku recover ikashindwa kulifikia ...
kwa technolojia za wenzetu huko unakuta kuna program zinaweza kurudisha data za hata tangu hdd ilipoanza kutumika from factory (tho sina hakika sana kwa hili) na ndo maana unakuta wale watu wanaofanya mambo yasiotakiwa kubakiza ushahidi wowote wana iharibu kabisa hdd kwa kuivunja vunja completely sababu ikipatakina tu watu wanaona kila kitu kilichoingia humo..
so kwa kujibu swali lako ni kuwa uwezo wa kujaa eti kwa sababu unaingiza data na kuzifuta hivyo zile unazozifuta kujaza nafasi si kweli maana inafika hatua nafasi ilele moja uliyoweka data ya kwanza na kufuta itatumika kuweka data ingine na ukifuta itakuwa allocated kwa data ingine nk...
ila tu kaa ukijua hakuna kitu kisicho na lifespan..itafika tu hatua hdd yenyewe itachoka hiyo write-delete action na ku fail...ingawa ni baada ya mda mrefu sna ikichangiwa na factors nyingine nyingi mf kugongwa gongwa nk..hapo ndipo unakuta pc ina detect kabisa hdd inakaribia ku fail
(nilishashuhudia hii kwa macho yangu kwa pc ina kama miaka 7 sahizi inalete error flani hivi kuwa hdd fail ipo karibu back up your data mapema na nilijaribu kufanya kila kitu kuiokoa ila wapi mpaka kuchange kwenye pc zingine tofautitofauti..error still there mpaka leo naitumia kama flash tu)