Mlamoto
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 351
- 138
Asante sana kwa maelezo, na kuna mdau Mlamoto amemaliza kabisa kwa kusema haiwezi kujaa.
Msinichoke bado mgeni kwenye hayo mambo:
Kama ndiyo hivyo ni kama hakuna limit (ukiacha lifespan), vipi kuhusu hizi capacity unaambiwa Hard disk gb5, Ram and Hdd so on hiyo haimaanishi kwamba kuna limit kuhifadhi data? ndiyo maana sisi bila kujua tuna-delete tukidhani tunameondoa kila kitu ili kupata space kubwa (hasa tunapoona computer inakuwa slow), kwa maelezo mengine hiyo HDD ukiacha life span haiwezi kujaa kabisa na kutoruhusu trash kutoka recyclebin ziingie?
Limit ya kuhifadhi data ipo kama hautafuta mafaili. Kwa ufahamu wako, Hdd za sasa hivi ni kubwa mno, hakuna 5gb tena!
Hard disk lifespan yake ni wastani wa miaka 5.
kwa hivyo usinunue hard disk used kamwe.
hard disks zina motor ambazo zinazunguka kama mara 5400, 7200, 15000 kwa dakika. Hivyo baada ya muda zinachoka.
kuna aina mpya ya storage inaitwa SSD. Solid state disk. inatumia technology ya flash disk kutunza data, ndo nzuri kwa sasa, haichoki mapema na inahimili mikimiki, haitumii motor
kuwa slow kwa computer yako haisababishwi na kujazwa vitu Kwenye computer.! No! Unless imejaa sana.
inasababishwa na program zinazojaza RAM yako na zile zinazo ifanya processor iwe bize muda mrefu.
Huwa zinaingia pamoja na program unazoweka. nyingi zina autostart. Nyingi ni za kidaku... huku zikijinadi kuwa zinafanya auto-update. ukweli ni kuwa zinapeleka information kadhaa kwa walio zitengeneza na hata kwengineko.... watch out!!!!