Albedo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 5,559
- 1,452
Matokeo ya Form Four Yametoka, Kwa Mara Nyingine tena Zaidi ya Aslimia 80 Wamefeli. Tuyaangalie haya Matokeo katika Mtindo Mwingine ambao uko Tofauti na Mtindo ambao NECTA wametumia kuyawakilisha haya Matokeo kwa Jamii ya Watanzania, Mtindo ambao NECTA walitaka tuamini kwamba waliofaulu ni 50.4%
Note: Idadi ya Wanafunzi waliofanya Mtihani ( Ukijumlisha Students and Private Candidates) walikuwa ni 441,271. Naomba niwazungumzie Only Student Candidates
Jumla ya Wanafunzi waliofanya Mtihani ni 352840
Divisheni One + Two + Three = 42,014 == 11.9%
Divisheni Four = 135,826 =========== 38.5%
Divisheni Zero = 175,000 =========== 49.6%
Kwa hiyo Divisheni Four + Divisheni Zero Jumla yake ni 310,826 ====== 88.1%
Tukae Tujiulize hivi hawa Zero&Four 300,000+ Ni nini Hatima yao? Kinachouma Zaidi ni kwamba Zaidi ya Asilimia 90 yao ni Watoto wa Wazazi wanaishi katika Lindi la Umaskini huku Pesa Zao zikienda Kufanya Shopping Dubai, Kosa lao nini hawa hadi Kustahili matokeo haya? Je Hii ni ndiyo Zawadi ya kuimba Nambari one eeeee eee Nambari one ni CCM? Je Tuendelee kulalamika hivi hivi kama Mwaka jana? Watanzania ni watu wa kusahahu hivi tunakumbuka mwaka Jana?
Ngoja Niwakumbushe Kidogo
Kuna Mtu ameshawahi kujiuliza Hatima ya hawa 65,708 wa mwaka 2009? Hivi hawa walimkosea nini Mungu?
Ngoja niyaweke hivi ili Muelewe nini Nazungumzia
----------------------------------2009 ---------2010 ------------2011
Divisheni ( One, Two and Three)....42,672--------- 42,014 ------------
Disheni Four...............................130,651...................135,826
Divisheni Zero............................ 65,708 ....................175,000
Nauliza Tena Tuendelee kulalamika ili Mwaka huu tena yatukute kama haya?
Ningependa sana JF kama Jukwaa la Great thinker tulijadili hili Suala ambalo mimi naliita ni Janga la kitaifa, tusilifanye likwa ni la Kidini (maana nimeshaona Baadhi ya watu wa Dini moja wakiwacheka wenzao na wenzao wakilaumu Serikali kuipendelea Dini Nyingine). Unapaswa kuwa Mjadala wa kitaifa wenye Lengo la Kuonesha Suluhisho juu ya Tatizo hili kwa manufaa ya watoto zetu, wadogo zetu na Taifa kwa Ujumla
Wana JF Nimamua Kuchokonoa Huu Mjadala naomba Tuchangie tukiwa na Tunatambua kwamba Watoto wa Maskini bila Kujali Dini zao wala Makabila yao Maisha yao yako hatarini.
Karibuni sana
Angalizo: Tusiingize Mambo ya Dini katika Mijadala yenye Tija kwa Taifa Letu
Note: Idadi ya Wanafunzi waliofanya Mtihani ( Ukijumlisha Students and Private Candidates) walikuwa ni 441,271. Naomba niwazungumzie Only Student Candidates
Jumla ya Wanafunzi waliofanya Mtihani ni 352840
Divisheni One + Two + Three = 42,014 == 11.9%
Divisheni Four = 135,826 =========== 38.5%
Divisheni Zero = 175,000 =========== 49.6%
Kwa hiyo Divisheni Four + Divisheni Zero Jumla yake ni 310,826 ====== 88.1%
Tukae Tujiulize hivi hawa Zero&Four 300,000+ Ni nini Hatima yao? Kinachouma Zaidi ni kwamba Zaidi ya Asilimia 90 yao ni Watoto wa Wazazi wanaishi katika Lindi la Umaskini huku Pesa Zao zikienda Kufanya Shopping Dubai, Kosa lao nini hawa hadi Kustahili matokeo haya? Je Hii ni ndiyo Zawadi ya kuimba Nambari one eeeee eee Nambari one ni CCM? Je Tuendelee kulalamika hivi hivi kama Mwaka jana? Watanzania ni watu wa kusahahu hivi tunakumbuka mwaka Jana?
Ngoja Niwakumbushe Kidogo
MATOKEO ya mtihani wa kumaliza kidato cha nne kwa mwaka 2009 yametangazwa jana na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) huku yakionyesha shule za serikali zikiendelea kufanya vibaya kwa kushindwa kuwemo kwenye shule 10 bora huku kiwango cha ufaulu kikizidi kupungua.
Aidha, matokeo ya mtihani huo uliofanyika Oktoba mwaka jana yanaonyesha kushuka kwa kiwango cha ufaulu kwa asilimia 11.2 kwani mwaka 2008 kilikuwa asilimia 83.69 wakati mwaka huu kikishuka hadi kufikia asilimia 72.51
Akitangaza matokeo hayo jana jijini Dar es salam kwenye ofisi za baraza hilo, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dk. Joyce Ndalichako, alisema watahiniwa 351,152 walisajiliwa kufanya mtihani wa kidato cha nne, kati yao wasichana ni 167,591 sawa na asilimia 47.73 na wavulana 183,561 sawa na asilimia 52.27 wakati mwaka 2008 watahiniwa 241,472 walisajiliwa
Alibainisha kuwa watahiniwa 42,672 sawa na asilimia 17.85 wamefaulu katika daraja la kwanza hadi la tatu ambapo wasichana ni 13,788 sawa na asilimia 12.47 na wavulana 28,884 sawa na asilimia 22.48.
Alisema, watahiniwa waliopata daraja la nne ni 130,651 sawa na na asilimia 54.66 wakati waliopata sifuri ni 65,708sawa na asilimi 27.49 idadi inayoonekana kuongezeka tofauti na mwaka jana.
Kuna Mtu ameshawahi kujiuliza Hatima ya hawa 65,708 wa mwaka 2009? Hivi hawa walimkosea nini Mungu?
Ngoja niyaweke hivi ili Muelewe nini Nazungumzia
----------------------------------2009 ---------2010 ------------2011
Divisheni ( One, Two and Three)....42,672--------- 42,014 ------------
Disheni Four...............................130,651...................135,826
Divisheni Zero............................ 65,708 ....................175,000
Nauliza Tena Tuendelee kulalamika ili Mwaka huu tena yatukute kama haya?
Ningependa sana JF kama Jukwaa la Great thinker tulijadili hili Suala ambalo mimi naliita ni Janga la kitaifa, tusilifanye likwa ni la Kidini (maana nimeshaona Baadhi ya watu wa Dini moja wakiwacheka wenzao na wenzao wakilaumu Serikali kuipendelea Dini Nyingine). Unapaswa kuwa Mjadala wa kitaifa wenye Lengo la Kuonesha Suluhisho juu ya Tatizo hili kwa manufaa ya watoto zetu, wadogo zetu na Taifa kwa Ujumla
Wana JF Nimamua Kuchokonoa Huu Mjadala naomba Tuchangie tukiwa na Tunatambua kwamba Watoto wa Maskini bila Kujali Dini zao wala Makabila yao Maisha yao yako hatarini.
Karibuni sana
Angalizo: Tusiingize Mambo ya Dini katika Mijadala yenye Tija kwa Taifa Letu