saigilomagema
JF-Expert Member
- Jun 5, 2015
- 4,091
- 6,100
Kama ilivyoripotiwa jana mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru amempeleka mwl. wa shule msingi Mrusha polisi ameteswa huko polisi ameshinda njaa na mateso mengine yasiyoelezeka.
Tangia asubuhi alishinda polisi usiku wa saa 4 alipelekwa na gari ya Halamashauri nyumbani kwake kupekuliwa wakarudi naye mjini na kulala rumande hawakumpa taarifa hata mkuu wake pale shuleni. Hawaruhusu mdhamana, yamekuwa km ya Mbowe. Kisa ni taarifa iliyoandikwa hapa JamiiForums juu ya walimu wapya pale Tunduru kunyanyaswa kwa ushirikiano kati ya ofisi ya Utumishi na Mwanasheria wa Halmashauri aitwaye kwa jina moja Walter.
Huyu bwana kiukweli ndio kawaida yake kuchukua pesa za walimu wapya kiasi cha Shs 82,000/ kila moja kwa vitisho kuwa usipoitoa hutasajiwa ktk mfumo wa ajira. Tulitegemea Mkurugenzi angewachukulia hatua kinyume chake waliochukuliwa pesa wamegeuziwa kipande wakishirikiana na polisi wasio waaminifu pale wilyani Tunduru. Ni walimu wengi waliwatoa pesa kwa njia ya vitisho kuwa wasingesajiliwa, sijui kigezo gani wametumia kumzushia kesi ya uwongo huyu moja.
Mwalimu wetu bado ameshikiliwa polisi hakuna mdhamana hatakiwi mtu kumsogelea wamemchukulia simu yake. Nijui km atatoka akiwa mzima tumwombee. Ana watoto wadogo wawili moja yuko chekechea na anaumwa mwingine yuko darasa la kwanza haijulikani wako ktk hali gani na km wanapata chakula na wamelala wapi ukizingatia moja mdogo ndio mgonjwa. Huu unyama anaoufanya Gasper Zahoro Balyomi(Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru) haujafanywa hata na Adolf Hitler.
Tuna viongozi wanawake lakini inaonekana hawana hata huruma, Rais mama, waziri wa Elimu mama, waziri wa TAMISEMI mama lakini tumeandika hatuoni hatua yoyote.
Wallahi nimemkumba hayati Magufuli haya yasingewezekana. kuna mkuu wa Wilaya, RAS na Mkuu wa Mkoa tena Brigedia Jenerali wa JWTZ Mkurugenzi wa Wilaya ni nyau wa aina gani ktk nchi hii? Halafu anaongea lugha ya kibaguzi eti watu wa kaskazini siwataki ktk Halmashauri yangu, kwanza ana Hamashauri au ni mtumishi tu? Watu wa kaskazini wameikosea nini nchi hii?
Mama Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunaomba msaada wako tunaweza hata kumpoteza huyu mtanzania hali yake ni mbaya sana. Mhalifu Walter (mwanasheria aliyechukua pesa za walimu wanyonge) na maafisa utumishi wilaya ya Tunduru ndio wamemwandalia hati ya mashtaka mtu innocent ambaye hajui hata kinachoendelea ktk mitandao ya kijamii.
Tangia asubuhi alishinda polisi usiku wa saa 4 alipelekwa na gari ya Halamashauri nyumbani kwake kupekuliwa wakarudi naye mjini na kulala rumande hawakumpa taarifa hata mkuu wake pale shuleni. Hawaruhusu mdhamana, yamekuwa km ya Mbowe. Kisa ni taarifa iliyoandikwa hapa JamiiForums juu ya walimu wapya pale Tunduru kunyanyaswa kwa ushirikiano kati ya ofisi ya Utumishi na Mwanasheria wa Halmashauri aitwaye kwa jina moja Walter.
Huyu bwana kiukweli ndio kawaida yake kuchukua pesa za walimu wapya kiasi cha Shs 82,000/ kila moja kwa vitisho kuwa usipoitoa hutasajiwa ktk mfumo wa ajira. Tulitegemea Mkurugenzi angewachukulia hatua kinyume chake waliochukuliwa pesa wamegeuziwa kipande wakishirikiana na polisi wasio waaminifu pale wilyani Tunduru. Ni walimu wengi waliwatoa pesa kwa njia ya vitisho kuwa wasingesajiliwa, sijui kigezo gani wametumia kumzushia kesi ya uwongo huyu moja.
Mwalimu wetu bado ameshikiliwa polisi hakuna mdhamana hatakiwi mtu kumsogelea wamemchukulia simu yake. Nijui km atatoka akiwa mzima tumwombee. Ana watoto wadogo wawili moja yuko chekechea na anaumwa mwingine yuko darasa la kwanza haijulikani wako ktk hali gani na km wanapata chakula na wamelala wapi ukizingatia moja mdogo ndio mgonjwa. Huu unyama anaoufanya Gasper Zahoro Balyomi(Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru) haujafanywa hata na Adolf Hitler.
Tuna viongozi wanawake lakini inaonekana hawana hata huruma, Rais mama, waziri wa Elimu mama, waziri wa TAMISEMI mama lakini tumeandika hatuoni hatua yoyote.
Wallahi nimemkumba hayati Magufuli haya yasingewezekana. kuna mkuu wa Wilaya, RAS na Mkuu wa Mkoa tena Brigedia Jenerali wa JWTZ Mkurugenzi wa Wilaya ni nyau wa aina gani ktk nchi hii? Halafu anaongea lugha ya kibaguzi eti watu wa kaskazini siwataki ktk Halmashauri yangu, kwanza ana Hamashauri au ni mtumishi tu? Watu wa kaskazini wameikosea nini nchi hii?
Mama Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunaomba msaada wako tunaweza hata kumpoteza huyu mtanzania hali yake ni mbaya sana. Mhalifu Walter (mwanasheria aliyechukua pesa za walimu wanyonge) na maafisa utumishi wilaya ya Tunduru ndio wamemwandalia hati ya mashtaka mtu innocent ambaye hajui hata kinachoendelea ktk mitandao ya kijamii.