DCs wapanguliwa na kustaafishwa

Huyu jamaa kutoka TRA,Chali Ubunge(CCM-Tarime) mpaka Ukuu wa Wilaya? Si Mwingine ni Bw. Christopher Ryoba Kangoye (Kwimba, Mwanza). Kweli Tanzania kila kitu kinawezekana ukizingatia pesa aliyopoteza pale Tarime kwenye mchakato wa uchaguzi Tarime, na alikuwa anakaribia kustaafu pale TRA, ngoja akapumzikie kwenye ukuu wa wilaya. Wasiwasi wangu isiwe ni sehemu ya kurudushia ile pesa yake aliyotupa kwa rushwa ili achaguliwe.
 
JK ni fisadi na ndiyo maana anaendelea kulea mafisadi. Francis Isaac alitimuliwa UVCCM kwa tuhuma za ufisadi, bado kambeba kama alivyo na kumpa Ukuu wa Wilaya, hivi kweli huyu Rais wetu yuko serious na vita ya mafisadi? Anapeleka msg gani kwa mafisadi wengine? Kwamba endelee kufanya ufisadi mkigundulika nitawahamishia sehemu nyingine! Kaazi kweli kweli.
 
Habari zilizopatika na ni kuwa DCs wamapanguliwa na wengine kustaafishwa bila shaka tuna wanachama wa JF waliopewa SHAVU.
RAIS KIKWETE AFANYA MABADILIKO YA WAKUU WA WILAYA

RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya chini kwa kuwateua wapya 15, kuwastaafisha wengine saba na kuwabadilisha vituo vya kazi 54.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) imeonyesha pia kuwa Wakuu wa Wilaya wawili watapangiwa kazi nyingine na wengine wawili wameteuliwa hivi karibuni kuongoza Jumuiya za Chama Tawala.

Mabadiliko haya yanatarajiwa kuongeza chachu katika usimamizi na ufuatiliaji wa shughuli za maendeleo ili kuiwezesha Serikali kufikia malengo yake, kwa mujibu wa taarifa hiyo.

Wakuu wapya wa Wilaya walioteuliwa ni Bi. Mercy Silla (Arumeru, Arusha), Bw. Norman Sigalla (Hai, Kilimanjaro), Col. Issa E. Njiku (Misenyi, Kagera), Bi. Angelina Mabula (Karagwe, Kagera), Dkt. Rehema Nchimbi (Newala - Mtwara), Francis Isaac (Mbulu, Manyara), Lt. Col. Benedict K. Kitenga (Rorya, Mara) na Lt. Col. Cosmas Kayombo (Mbarali, Mbeya).

Wengine ni Bw. Christopher Ryoba Kangoye (Kwimba, Mwanza); Bi. Queen Mwanshinga Mlozi (Ukerewe, Mwanza); Bi. Fatuma Mwassa (Mvomero, Morogoro); Bi. Fatma Ally (Nanyumbu, Mtwara); Bw. Juma Solomon Madaha (Tunduru, Ruvuma); Bw. Anatory Choya (Kishapu, Shinyanga) na Bw. Erasto Sima (Korogwe, Tanga).

Wakuu wa Wilaya waliostaafishwa na vituo vyao kwenye mabano ni Bw. Elias Maarugu (Misenyi, Kagera); Bw. Deusdedit Mtambalike (Muleba, Kagera); Bw. David Holela (Babati, Manyara); Bi. Hawa Ngulume (Mbarali, Mbeya); Bw. Mashimba H. Mashimba (Kyela, Mbeya); Col. Peter Madaha (Nyamagana, Mwanza) na Bw. Gilbert Dololo (Kibaha , Pwani).

Wakuu wa Wilaya ambao wamepangiwa kupewa kazi nyingine ni Bw. Patrick Tsere aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala (Dar es Salaam) na Bi. Doreen Kisamo aliyekuwa Uyui (Tabora).

Bw. Martin Shigela aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi (Lindi) aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa UVCCM wakati Bi. Husna Mwilima aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai (Kilimanjaro) aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa UWT


Mimi masikitiko yangu ni kwmba form IV wamejazana humo, mfano ni Anatory choya, huyu alikuwa mbunge wa biharamulo magharibi 1995-2005. Aliwahi kufanya kazi uhamiaji sasa eti mkuu wa wilaya...jamani JK sijui anawashauri wa aina gani???
 
JK ni fisadi na ndiyo maana anaendelea kulea mafisadi. Francis Isaac alitimuliwa UVCCM kwa tuhuma za ufisadi, bado kambeba kama alivyo na kumpa Ukuu wa Wilaya, hivi kweli huyu Rais wetu yuko serious na vita ya mafisadi? Anapeleka msg gani kwa mafisadi wengine? Kwamba endelee kufanya ufisadi mkigundulika nitawahamishia sehemu nyingine! Kaazi kweli kweli.

Kaaazi kwelikweli!!!!!!!!!!!!!! Hii ni dalili kuwa hata wale mafisadi waliojiuzulu watakuwa wanaandaliwa maeneo ya kujidai mahali pengine! Muungwana hana aibu!
 
Wakuu, swali langu ni kwamba "Mbona lawama zote anapewa JK, je ni yeye aliamua nani awe wapi au ni washauri wake?". Kama ni washauri wake (ambalo naamini ni sawa sababu Raisi hawezi chagua wakuu wa wilaya, mikoa, wakurugenzi, maPS, etc etc etc kutokea kichwani pake pekee) then tusimlaumu sana manake ni "shared responsibility" hiyo, washauri wanapendekeza yeye ana approve!!

Kurudi kwenye mada ni kwamba kwa vile siwafahamu wote, basi nijiunge kulaumu kwenye mapungufu (kama yapo)!
 
Hayo ni maandalizi ya 2010.Lazima aweke ccm makada.
Hivi ingekuwaje pale ambapo nafasi za u-DC zinatangazwa, watu waombe kama kazi nyingine. Nakumbuka enzi za nyumba Mkapa alikuwa ameanzisha utaratibu wa ma-DED kuomba kazi badala ya kuteuliwa ingawa Kikwete alikuja kuiondoa!
 
Kuna wazee ambao walishapoteza kina shelutete du yule ndio kimeo kabisa...pia yule wa bagamoyo..pia waliowekwaga na sumaye hasa wamama kibaoo walikuwa headteachers kuna kazi kubwa....
 
nimekumbuka maneno ya mkapa,watanzania wana wivu wa kike..kiutendaji frank isac hana tatizo kabisa na kutolewa kwake pale ilikuwa kwa makubaliano kama haya!
Any way,Mercy Silla amefanya nini?ukiangalia kabisa utaona ameandaliwa mtu..
Patrick sere anaweza kupewa nafasi ya Mercy ,
Hv hawa wanajeshi wastaafu na ukuu wa wilaya wapi na wapi?au CDF Naye ana nafasi zake
 
nimekumbuka maneno ya mkapa,watanzania wana wivu wa kike..kiutendaji frank isac hana tatizo kabisa na kutolewa kwake pale ilikuwa kwa makubaliano kama haya!
Any way,Mercy Silla amefanya nini?ukiangalia kabisa utaona ameandaliwa mtu..
Patrick sere anaweza kupewa nafasi ya Mercy ,
Hv hawa wanajeshi wastaafu na ukuu wa wilaya wapi na wapi?au CDF Naye ana nafasi zake
Huu je ni wivu wa kiume?
 
Tunaomba full list ya waliohamishwa....maana jumla waliohamishwa wapo 54 taarifa haijakamilika
 
Huu je ni wivu wa kiume?

Ona sasa unaposhindwa kujenga hoja,hayo yametoka wapi?mie nimeuliza kwa nia njema ili nijue,au na wewe unataka uwe maarufu tu kupitia kupinga hoja za Gembe?

Babu yako Mwanakijiji huwa ana kumsemo flani ka ukweli sana,kila mtu anaweza kuandika maneno ila kupanga maneno ni sanaa wanaoiweza wachache !wewe siyo mmoja wao!
 
Ona sasa unaposhindwa kujenga hoja,hayo yametoka wapi?mie nimeuliza kwa nia njema ili nijue,au na wewe unataka uwe maarufu tu kupitia kupinga hoja za Gembe?

Babu yako Mwanakijiji huwa ana kumsemo flani ka ukweli sana,kila mtu anaweza kuandika maneno ila kupanga maneno ni sanaa wanaoiweza wachache !wewe siyo mmoja wao!
Ama kweli nyani haoni kundule!kama bodi twende
 
Back
Top Bottom