Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,499
Mkuu wa Wilaya ya Songea, Wilman Kapenjama Ndile, ametoa wito kwa viongozi wa dini kuhakikisha wanasimamia na kuhimiza amani nchini ambacho taifa linaelekea kwenye uchaguzi mkuu.
Akizungumza wakati wa ibada ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Ruvuma, April 20, 2025 Mhe. Ndile alitoa salamu za serikali na kusisitiza umuhimu wa mshikamano wa kitaifa. Alieleza kuwa ni wajibu wa kila kiongozi, hususan wa dini, kuhubiri na kulinda amani, kwa kuwa historia imeonesha jinsi baadhi ya mataifa ya Afrika yalivyoingia kwenye machafuko kutokana na mivutano ya uchaguzi.
“Nchi nyingi barani Afrika zimeathirika na machafuko yanayotokana na chaguzi, jambo ambalo linaweza kuzuiwa endapo tutadumisha maelewano, mshikamano na heshima kwa misingi ya demokrasia. Viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kuhakikisha haya hayaingii nchini mwetu,” Alisema Mhe. Ndile.
Pia Mhe Ndile ameongeza kuwa hivi karibuni kumekuwa na kauli ambazo zimekuwa zikitolewa na baadhi ya wanasiasa ambazo zinaashiria uvunjifu wa amani.
Chanzo: Manara TV
Akizungumza wakati wa ibada ya Pasaka iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Ruvuma, April 20, 2025 Mhe. Ndile alitoa salamu za serikali na kusisitiza umuhimu wa mshikamano wa kitaifa. Alieleza kuwa ni wajibu wa kila kiongozi, hususan wa dini, kuhubiri na kulinda amani, kwa kuwa historia imeonesha jinsi baadhi ya mataifa ya Afrika yalivyoingia kwenye machafuko kutokana na mivutano ya uchaguzi.
“Nchi nyingi barani Afrika zimeathirika na machafuko yanayotokana na chaguzi, jambo ambalo linaweza kuzuiwa endapo tutadumisha maelewano, mshikamano na heshima kwa misingi ya demokrasia. Viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kuhakikisha haya hayaingii nchini mwetu,” Alisema Mhe. Ndile.
Pia Mhe Ndile ameongeza kuwa hivi karibuni kumekuwa na kauli ambazo zimekuwa zikitolewa na baadhi ya wanasiasa ambazo zinaashiria uvunjifu wa amani.