DC Rorya awasweka walimu mahabusu wiki moja bila dhamana

Sesimba

Senior Member
Dec 20, 2016
189
382
Walimu wawili wa Shule ya Sekondari Musa Akasha iliyoko wilayani Rorya Mkoa wa Mara wamesota mahabusu kwa wiki moja bila dhamana kwa amri ya Mkuu wa Wilaya kwa kosa la kuadhibu mwanafunzi ambaye alifika shukeni akiwa amevalia viatu vya plastiki ambavyo si sare ya shule.

Walimu hao walikamatwa tangu alhamisi tarehe 22/08/2019,wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime jana na kuachiwa kwa dhamana baada ya kudhaminiwa na viongozi wa CWT Rorya.

Taarifa zinadokeza kuwa DC Chacha alitoa onyo kali kwa Mwalimu yeyote atakayekwenda kuwajulia hali wenzie huko mahabusu na hata kuwawekea dhamana ndo Chama Cha Walimu CWT kilijitosa kuwadhamini mahakamani.

My take..

Inawezekana walimu Hawa wamefanya kosa kweli maana Ni taarifa ya upande mmoja pekee ndo tunayo

Sijui ni kwa nini vyombo vya habari Rorya vimekaa kimya juu ya kadhia hii.Walimu wa nchi hii wamegeuka kuwa ngazi kwa watawala uchwara kutafuta umaarufu na hatimaye kupanda vyeo.

Huu ni mwendelezo wa manyanyaso ya watawala dhidi ya walimu wa nchi hii.Sijui ni lini haya yatakuwa na mwisho? Ikumbukwe tu kwamba mwalimu huyu anayetendewa haya ameelemewa na changamoto lukuki ambazo zinaathiri utendaji wake wa kazi.

Walimu wanafanya kazi katika mazingira magumu,hawana nyongera ya mshahara kwa miaka kadhaa sasa,hawalipwi madeni yao lakini kwa watawala wetu njia pekee ya kuwafariji na kuwatia moyo walimu ni kuwasweka mahabusu na kuwanyima dhamana.

Tatizo la yote haya ni sababu tunatawaliwa na viongozi ambao hawana hofu ya Mungu ndani yao.Kwao vyeo ni Mungu,hawaoni shida kukuumiza ilimradi tu waifurahishe mamlaka ya uteuzi ili wafikiriwe kwa nafasi za juu zaidi.

Poleni Walimu wa Musa Akasha.Lakini pia hovyo kabisa Mkuu wa Shule hiyo uliyeogopa hata kwenda kuwajulia hali walimu wako wakiwa mahabusu kwa siku zote hizo.

Wanajukwaa Je hii Ni kweli? Je Ni kweli DC mamlaka ya kutoa amri ya kumuweka mtu rumande kwa wiki nzima bila kumpeleka mahakamani?
 
Nimepata msamiati kutoka nchi jirani leo; mis-leaders.
Nchi hii inaendeshwa na mis-leaders safari hii, sio leaders.
 
Sisi tulienda shule peku, hawo wanaona plastic sio sare, shida yote ni elimu bure, walikua wapigaji, sasa hamna kitu wanahaha, mikopo bank, Saccoss na Micro-finance hasira zote anabebeshwa mwanafunzi..........
 
Sisi tulienda shule peku, hawo wanaona plastic sio sare, shida yote ni elimu bure, walikua wapigaji, sasa hamna kitu wanahaha, mikopo bank, Saccoss na Micro-finance hasira zote anabebeshwa mwanafunzi..........
Well said👏🏽
 
Mwenye uzi tafadhali angalia tarehe, vingenevyo uzi huu unakosa uhalali kwani inaonekana tarehe 22.8.2019.ambayo bado hatujaifikia.
 
Swala sio kwenda peku shule,au elimu bure,swali la msingi ni kwamba huyo mkuu wa wilaya aliye mbumbumbu wa sheria,na mbumbumbu wa fikra,ana mamlaka ya kumuweka raia yeyote yule "lock up" kwa wiki nzima bila dhamana wala kumfikisha mahakamani?

Hao ndo wakuu wa wilaya wanazaliwa kupitia nyuchi chafu za mama zao!
Shenzi type!
Sisi tulienda shule peku, hawo wanaona plastic sio sare, shida yote ni elimu bure, walikua wapigaji, sasa hamna kitu wanahaha, mikopo bank, Saccoss na Micro-finance hasira zote anabebeshwa mwanafunzi..........
 
Ili uwe mwalimu lazima uwe umefeli masomo darasani. Sasa nashauri walimu wasilipwe mishahara na wawe wanachapwa na madiwani au watendaji wa vijiji
Wewe hujielewi kabisa aliekwambia ili uwe mwalimu lazima uwe umefeli darasani nani kakudanganya????.......

Hio sio kweli kuna watu wameenda ualimu wana divisheni one wewe unaongea pumba gani.......???....

Au wewe walimu waliokufundisha walikua wenye divishen four???...

Acha dharau kabisa....
 
mosi: yes, walimu hao ni wapuuzi wanapaswa kuadhibiwa kwa kitendo chao cha hovyo ni kijinga, lakini taratibu za kuadhibu watumishi wa umma zinafaamika
pili: jeshi la polisi ni wapuuzi kwa kukubali kuvunja sheria na kumshikilia mtu kwa zaidi ya saa 24 bila mashtaka yoyote ati kwavile mkuu wa wilaya amesema, kwanini polisi hampigi simu kwa wakubwa zenu kupata clarification ya haya mambo? piga simu kwa RPC au makao makuu kisha waachie watuhumiwa, akija DC mwambie umepata maagizo toka juu.
 
Swala sio kwenda peku shule,au elimu bure,swali la msingi ni kwamba huyo mkuu wa wilaya aliye mbumbumbu wa sheria,na mbumbumbu wa fikra,ana mamlaka ya kumuweka raia yeyote yule "lock up" kwa wiki nzima bila dhamana wala kumfikisha mahakamani?

Hao ndo wakuu wa wilaya wanazaliwa kupitia nyuchi chafu za mama zao!
Shenzi type!
Mahakama sio mama yako Ikupe chakula pale wanapohisi una njaa, kama haki ya dhamana imekiukwa inabidi kesi ifunguliwe yakudemand polisi wawapeleke mahakamani ASAP!

Habeas corpus - Habeas corpus (/ˈheɪbiəs ˈkɔːrpəs/ ; Medieval Latin meaning "[we, a Court, command] that you have the body [of the detainee brought before us]")[1] is a recourse in law through which a person can report an unlawful detention or imprisonment to a court and request that the court order the custodian of the person, usually a prison official, to bring the prisoner to court, to determine whether the detention is lawful
 
Ili uwe mwalimu lazima uwe umefeli masomo darasani. Sasa nashauri walimu wasilipwe mishahara na wawe wanachapwa na madiwani au watendaji wa vijiji
Wakati huo na wewe umefundishwa na nani hadi ukajua kusoma na kuandika hiki ulicho andika? Kweli umeonesha uwezo mdogo sana wa kufikiri
 
Hivi vyeo vifutwe hawa jamaa hawana kazi yoyote ile na ndiyo chanzo kikuu cha migogoro katika Halmashauri zetu nchini.
 
Back
Top Bottom