Daycare centre, hazina iliyojificha

thebusdriverclassc

Senior Member
Jan 16, 2014
146
66
Habarini za mchana wadau, natumai mpo salama mkiendelea kutimiza majukumu yenu ya kila siku. Niliwahi kuja na wazo biashara siku zilizopita. Biashara ya M-pesa, nashukuru kwani nilipata michango ya wadau wengi, ikieleza faida na hasara za hii biashara.

Mimi binafsi kutokana na michango niliyopata kwenu, bado nitaifanya sababu naamini "something is better than nothing" hata kama ni sh.100.

Sasa nirudi kwenye mada, wazo ambalo nimelipata sambamba na hilo ni kufungua kituo cha kuwaangalia na kuwahudumia watoto kipindi wazazi hawapo majumbani, (mchana-daycare centre). Nipo Arusha, mimi ni muajiriwa pamoja na mke wangu na hii ni kutafuta kipato cha ziada.

Naomba yeyote mwenye uzoefu, anayefanya au anayeweza kunifanyia mchanganuo wa hiki ninachotaka kufanya anisaidie, gharama na mahitaji muhimu katika kufanikisha hili. Nina mtaji wa million 1.5.

Asanteni sana.
 
Ni wazo zuri sana ukuzingatia wakati huu wazazi wengi wanapata shida ya kupata wadada Wa kazi wazuri wengi wana vibwanga kwa watoto . kikubwa ni kuandaa mazingira mazuri yatakayowarithisha wazazi kuwaacha watoto wao hapo.
 
Wazo ni zuri muhimu cha kufanya kwanza ni eneo linalofikika na lenye mazingira rafiki kwa watoto si kwamba unawapeleka gereji , pili nini unawapatia watoto baada ya kuwachukua kutoka wa wazazi wao hapa huenda ikawa kuwapatia elimu na n.k /, tatu ni kuwasiliana na mamlaka zinazohusika kuhusiana na usajiri wao watakupatia vigezo muhimu vya kufanya
 
Baada ya michango yoote hiyo.
Muhim ni mazingira mazuri kwa watoto.
Day Care center,unajua wazazi huangalia zaidi mazingira,maana level hiyo hawaangalii utafundisha nini,maana hao virukuu wanakuwa hawana issue,sasa focus yao ni kwenye mazingira.

Ila kwa 1.5,baso saana mkuu,maana ujue ni bora nursery school ni rahisi kuliko Dar care center.
Ni gharama kiasi,na usafi wa hali ya juu mno,na wafanyakazi si chini ya 3 mpaka 9.
Ukitaka kujua hilo,nenda sehem ukute watoto wamelianzisha kulia,aisee kazi ngum hii balaa.Bora uambiwe uwapigishe mswaki mbuzi kuliko ku deal na watoto level hiyo.
Kina vikojozi,kuna watemi,kuna waroho,muda woote wanataka kula tuuuuuu,kuna wasioshiba,yaani balaa.wenye kujiharia ndio usiseme.Wenye kupenda kusinzia ohoo hao ndio balaa yaani wakigusa geti full kulala.
 
Mkuu naona kama kiasi hicho ulichonacho ni kidogo kwa kuanzia sababu utahitaji kuwa namazingira safi na yanayovutia, vile vile vifaa kama magodoro kwa ajili ya kupumzikia, vijitu vya kuchezea watoto, vyombo vya chakula n.k, ila kwa kiasi hicho waweza fungua kituo cha watoto cha kujifunza. Kwa mfano mi na Mr wangu tulifungua kituo cha watoto cha kujifunza wanaingia asubuhi wanatoka saa 6 kwakweli tunamshukuru Mungu mambo sio mabaya
 
Mkuu naona kama kiasi hicho ulichonacho ni kidogo kwa kuanzia sababu utahitaji kuwa namazingira safi na yanayovutia, vile vile vifaa kama magodoro kwa ajili ya kupumzikia, vijitu vya kuchezea watoto, vyombo vya chakula n.k, ila kwa kiasi hicho waweza fungua kituo cha watoto cha kujifunza. Kwa mfano mi na Mr wangu tulifungua kituo cha watoto cha kujifunza wanaingia asubuhi wanatoka saa 6 kwakweli tunamshukuru Mungu mambo sio mabaya
Sasa baby si utumwagie maujuzi hapa.
Maana wewe ni mdau,maana kituo cha watoto cha kujifunza sijaelewa kivipi yaani.
 
Sasa baby si utumwagie maujuzi hapa.
Maana wewe ni mdau,maana kituo cha watoto cha kujifunza sijaelewa kivipi yaani.
Sorry nilikua offline, kituo kinakua kama Nursery, ila sasa ukiandika moja kwa moja Nursery utadaiwa usajili kwasababu nursery ni shule hiyo tayari ila kwakua mdau ndio anataka kuanza atumie Children learning centre ila watoto wanasoma kama chekechea mambo yakiwa vizuri anaanza taratibu za kusajili
 
Sorry nilikua offline, kituo kinakua kama Nursery, ila sasa ukiandika moja kwa moja Nursery utadaiwa usajili kwasababu nursery ni shule hiyo tayari ila kwakua mdau ndio anataka kuanza atumie Children learning centre ila watoto wanasoma kama chekechea mambo yakiwa vizuri anaanza taratibu za kusajili
Inakuwa na watoto wa kuanzia umri gani
 
Habarini za mchana wadau, natumai mpo salama mkiendelea kutimiza majukumu yenu ya kila siku...niliwahi kuja na wazo biashara siku zilizopita...biashara ya M-pesa, nashukuru kwani nilipata michango ya wadau wengi, ikieleza faida na hasara za hii biashara.


Mkuu ushafungua hii kitu au bado?
please nicheki inbox
 
Mkuu naona kama kiasi hicho ulichonacho ni kidogo kwa kuanzia sababu utahitaji kuwa namazingira safi na yanayovutia, vile vile vifaa kama magodoro kwa ajili ya kupumzikia, vijitu vya kuchezea watoto, vyombo vya chakula n.k, ila kwa kiasi hicho waweza fungua kituo cha watoto cha kujifunza. Kwa mfano mi na Mr wangu tulifungua kituo cha watoto cha kujifunza wanaingia asubuhi wanatoka saa 6 kwakweli tunamshukuru Mungu mambo sio mabaya
Ungeenda extra ukaelezea zaidi kwa faida ya wengi
 
Baada ya michango yoote hiyo.
Muhim ni mazingira mazuri kwa watoto.
Day Care center,unajua wazazi huangalia zaidi mazingira,maana level hiyo hawaangalii utafundisha nini,maana hao virukuu wanakuwa hawana issue,sasa focus yao ni kwenye mazingira.

Ila kwa 1.5,baso saana mkuu,maana ujue ni bora nursery school ni rahisi kuliko Dar care center.
Ni gharama kiasi,na usafi wa hali ya juu mno,na wafanyakazi si chini ya 3 mpaka 9.
Ukitaka kujua hilo,nenda sehem ukute watoto wamelianzisha kulia,aisee kazi ngum hii balaa.Bora uambiwe uwapigishe mswaki mbuzi kuliko ku deal na watoto level hiyo.
Kina vikojozi,kuna watemi,kuna waroho,muda woote wanataka kula tuuuuuu,kuna wasioshiba,yaani balaa.wenye kujiharia ndio usiseme.Wenye kupenda kusinzia ohoo hao ndio balaa yaani wakigusa geti full kulala.
Umewasahau wachokozi! Wale akina mwakinyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom