Wadau JF salam,
Kimekuwa kilio cha wanadaoa wengi sana kwenye familia zao juu ya ujio wa michepuko au nyumba ndogo.. na niongeze kwa kusema imekuwa kama kamtindo fulani sasa kwa wanandoa..
Naomba niwarudishe kidogo kwenye asili ya mtu mwesi, kwa haraka nikifuatilia naona asili yetu kabla ya ujio wa wazungu au wakoloni na sera zao za mke mmoja kwa kila familia, babu zetu walikuwa na wake zaidi ya mmoja, hapa nisimung'unye maneno, yaani walikuwa na wake wengi sana..
Na kama msomaji wa mada hii, haukubaliani na nami hebu jiulize tafadhari, kwenye familia yako kama unafatilia histoa ya ukoo wako utagundua BABU YAKO WA BABU YAKO ALIKUWA NA MKE ZAIDI YA MMOJA,Maana yake wake wengi.
Sasa wadau mkubaliane na mimi kama tunaamini kuwa kuna magonjwa ya kurithi kwenye koo kwanini kusiwe na kurithi hizi tabia za MABABU ZETU WA KIAFRIKA ZA KUWA NA WAKE WENGI,,
Ninacho amini mimi nikuwa,tatizo la michepuo au nyumba ndogo lililo ingia sasa ni issue ya kurithi, ijapo kuwa tumeucha utamanduni wetu na kufuata wa kishenzi, namanisha wa kizungu wa kuwa na mke mmoja..
Lakini lengo la mzungu lilikuwa kupunguza idadi ya sisi kuzaliana wakati tu tegemezi..
Mtazamo wangu, inabidi mabinti walikalie kikao kulijadili kwa kina na haswa kwenye makicheni part, kuliko kuacha hali ilivyo sasa,na ufumbuzi wao waulete hapa JF na sisi wababa tutauchangia..
Karibuni sana wadau..!!