Dawa ya kukojoa mkojo wa manjano (yellow)

Dawa ya kukojoa mkojo wa manjano (yellow)

Pia nashauri uwe unakula miwa hasa ile yenye maganda meusi, pia mchaichai kama alivyokusahuri member hapo juu na maji yatasaidia sana kusafisha figo zako. Pia hebu wasiliana na namba hii 0713 242058 anaweza kukupatia virutubisho vya figo. Ana dawa nzuri sana hata kwa wale wenye shida ya viungo, ni virutubisho tu si dawa za kienyeji.
 
Kule kwetu Katavi mara nyingi ukiugua ugonjwa huo wa kukojoa mkojo wa manjano ulikuwa unakula miwa flani mitamu inaitwa Bungala sasa sijui upande uliopo miwa hiyo kama inapatikana ili ujaribu kuila kwa wiki moja tu kazi kwisha
 
wanajamii nimeelimika vya kutosha sana nawashukuruni
 
Wana jamii naombeni msaada wenu nina tatizo la kukojoa mkojo wa njano sana kwa muda wa miaka mitatu sasa nimekwenda hospitali lakini inaonekana sina tatizo, naomba kujua dawa yake nn wana jamvi. Tatizo hili limekua ni kero kwangu hata ninywe maji mengi vip baada ya muda mfupi tu hali inajirudia tena.

Rangi ya njano kwenye mkojo hutokana na kemikali inayoitwa urobilinojeni. Urobilinojeni ni zao la bilirubini na bilirubini ni zao la chembechembe nyekundu za damu, hivyo ili kujibu hili kunahitaji mambo haya kuzingatiwa:

1: kuangalia hali ya ufanyaji kazi wa ini.

2: Kuangalia kama kuna hali inayosababisha kufa kwa kasi kubwa kwa chembe chembe nyekundu za damu.

3: Matumizi ya vyakula/dawa vinavyoweza kuchangia kubali rangi ya mkojo.

4: Kuangalia kama kiasi cha maji unayokunywa kinaendana na asili ya kazi unayoifanya na eneo ulilopo (joto).
 
Back
Top Bottom