Dawa hii ya mitishamba ina walakini ichunguzwe

Dawa hii ya mitishamba ina walakini ichunguzwe

Mabobish

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2018
Posts
367
Reaction score
282
Dawa yenye picha hapa chini kama inavyojieleza ni dawa Magumashi kabisa, inavyoelekea imewekwa tu majani ya makavu ya kunde au majani ya maharage kisha kuwekwa kwenye karatasi ya rangi na kuuzwa kama dawa ya kutibu maradhi yalioandikwa katika hiyo karatasi.

Dawa hii nimeinunua Dodoma kwa binti mmoja anajiita Subira kwa maelezo yake anasema anaishi maeneo ya Makole lakini siku alipokuwa akiuza alinikuta maeneo ya ChakoniChako Bar, kwa kweli kanilamba takribani 45,000/= kwa paketi moja na niliwachukulia na wenzangu 2 kwa maana ya jumla ya paketi 3 na maelekezo ni kwamba dozi yake ni siku 3 kwa maana ya kijiko cha chai 1x1 kwa siku 3 tu kwa kunywea ktk kinywaji chochote, na matokeo yake yataanza kuonekana Massa 2 na kuendelea tangu kuanza kutumika.

Cha ajabu na kusikitisha tangu tumeitumia zimepita siku 6 hakuna matokeo yoyote chanya zaidi tumetapeliwa na huyo Dada Subira akipigiwa simu japo atoe ufafanuzi tangu alipoelezwa tatizo hapokei simu na wala hajibu meseji jambo linaloashiria anafanya utapeli wa kukusanya hela za watu kwa kuuza dawa fake na huenda ikichunguzwa kiundani inaweza kuwa na madhara makubwa kwa matumizi ya binadamu.

Chonde wenye tatizo kama langu chukueni tahadhali na dawa hiyo hususani na huyo Binti muuzajiView attachment 864987
IMG_20180913_093256.jpg
 
anyway tuachane na dawa kwasbb mamlaka husika itashughulikia.

kiatu kama hicho kwenye picha yakos sh ngapi mkuu?
 
Haya madawa mengine tuwe waangalifu sana,sijawahi kusikia dawa inatibu multiple disease tena na magonjwa ya mishipa ya damu na moyo???? Akili za kuambiwa changanya na zako
 
Haya madawa mengine tuwe waangalifu sana,sijawahi kusikia dawa inatibu multiple disease tena na magonjwa ya mishipa ya damu na moyo???? Akili za kuambiwa changanya na zako
hushangazwi na mwarobaini wa mwakipesile?
 
Dawa yenye picha hapa chini kama inavyojieleza ni dawa Magumashi kabisa, inavyoelekea imewekwa tu majani ya makavu ya kunde au majani ya maharage kisha kuwekwa kwenye karatasi ya rangi na kuuzwa kama dawa ya kutibu maradhi yalioandikwa katika hiyo karatasi. Dawa hii nimeinunua Dodoma kwa binti mmoja anajiita Subira kwa maelezo yake anasema anaishi maeneo ya Makole lakini siku alipokuwa akiuza alinikuta maeneo ya ChakoniChako Bar, kwa kweli kanilamba takribani 45,000/= kwa paketi moja na niliwachukulia na wenzangu 2 kwa maana ya jumla ya paketi 3 na maelekezo ni kwamba dozi yake ni siku 3 kwa maana ya kijiko cha chai 1x1 kwa siku 3 tu kwa kunywea ktk kinywaji chochote, na matokeo yake yataanza kuonekana Massa 2 na kuendelea tangu kuanza kutumika. Cha ajabu na kusikitisha tangu tumeitumia zimepita siku 6 hakuna matokeo yoyote chanya zaidi tumetapeliwa na huyo Dada Subira akipigiwa simu japo atoe ufafanuzi tangu alipoelezwa tatizo hapokei simu na wala hajibu meseji jambo linaloashiria anafanya utapeli wa kukusanya hela za watu kwa kuuza dawa fake na huenda ikichunguzwa kiundani inaweza kuwa na madhara makubwa kwa matumizi ya binadamu. Chonde wenye tatizo kama langu chukueni tahadhali na dawa hiyo hususani na huyo Binti muuzajiView attachment 864987View attachment 864988
Kutokana na maelezo yako ni kuwa una shida umekunywa ili kutatua shida zako za kiume hapo nitakuelewa kuwa dawa haikufanya kazi. AU umekunywa na wewe huna shida tajwa lakini unategemea kupata matokeo fulani ambayo huwezi pata kama huna shida husika, hapo vipi?
 
Haya madawa mengine tuwe waangalifu sana,sijawahi kusikia dawa inatibu multiple disease tena na magonjwa ya mishipa ya damu na moyo???? Akili za kuambiwa changanya na zako
Nakubaliana na ushauri wako Mkuu
 
Kutokana na maelezo yako ni kuwa una shida umekunywa ili kutatua shida zako za kiume hapo nitakuelewa kuwa dawa haikufanya kazi. AU umekunywa na wewe huna shida tajwa lakini unategemea kupata matokeo fulani ambayo huwezi pata kama huna shida husika, hapo vipi?
Nina shida mkuu Ila nimetapiliwa na kibaya zaidi kumbuka nimesema dawa hii niliwanunulia na wenzangu 2 wenye tatizo kama langu, matokeo yake wote haijatusadia kitu chochote ukilinganisha na kiki za muuzaji kuwa inaanza kufanyakazi w.e.f ndani ya Massa 2 tangu kuanza kutumika. Sasa zimepita siku 6 wakati dozi yake ni siku 3 ngoma bilabila
 
Yaani watu mnakutana bar mnauziana hayo majani ya porini unaanza kulalama humu na post ndeefu.

Ukitapeliwa kausha ndo mwanzo wa kujanjaruka.
 
Back
Top Bottom