David Kafulila ahamia NCCR Mageuzi akitokea CHADEMA

David Kafulila ahamia NCCR Mageuzi akitokea CHADEMA

Isipokuwa hao NCCR nao ni vipi wamekimbilia kumpa kadi ya Chama chao bila kuhakikisha kuwa kaachana na Chadema? Mimi hata sura yake inanitia mashaka kuwa si mtu wa kuaminika kiasi hicho.

Boney E.M
Mkuu sio vyema kumjadili mtu basing on maumbile yake,yeye ameumbwa hivyo na hakuna mtu aliyeomba kuwa jinsi alivyo.Mjadili kutokana na hoja.
 
6753d1258973202-a-ncccccccccr.jpg

Halina tofauti na lile la Askari Mgambo

Haijalishi.Naona hili vazi limekugusa sana,yalekea unalipenda sana ndio maana kwako imekuwa ni hoja sana.Washuri CCM nao waige sio mnavaa mirangi mtafikiri mko kwenye mshindano ya urembo.......teh teh teh. Kwa kweli vazi la CHADEMA funika mbaya.
 
in short hawa kina Kafulila hawana tofauti na kina Mrema, ni mpenda madaraka na anataka apate ajira si kuwa ana uchungu na nchi,kama kweli angebaki Chadema aongee na uongozi wayamalize than apewe jimbo!akikosa kupitia hiki chama kilichokosa umaarufu kwa mda sasa atakimbilia CCM quote my words today, watu wa namna hii ni wavurugaji wa vyama so hawapo tayari kumaliza tofauti zao ili kukiusuru chama,ni mchezo mchafu unaendelea may be anapata hata mgao from somewhere who knows?
 
aisee mambo jambo, tusianze kutukanana humu samahani sana, hata kama ni mchanga sana humu lakini habari zipo nyingi mitaani na kichwa kimekomaa sana, mmm nahisi unajingine. humu uwe umeingia leo au jana wote ni great thinkers and we dare talk openly, kama umekwazika kajinyonge basi
 
in short hawa kina Kafulila hawana tofauti na kina Mrema, ni mpenda madaraka na anataka apate ajira si kuwa ana uchungu na nchi,kama kweli angebaki Chadema aongee na uongozi wayamalize than apewe jimbo!

Sasa katika kuhama kutoka katika chama chenye umaarufu zaidi na kuingia katika chama kilichofifia na kuyamaliza katika chama chenye umaarufu ili APEWE ubungo, ni ipi dalili ya kupenda madaraka ama maslahi binafsi?

Wandungu tuache unazi ama kile ninachoita UKADA POFU. Kafulila kafanya makosa kisiasa ya kuondoka CHADEMA kwa namna na wakati huu. Lakini bado ana haki ya kupimwa kwa vigezo vya mtizamo wake mwenyewe na sio hizi siasa za maji chafu tunazoendeleza hapa dhidi yake. Kama wapenda demokrasia ama wanademokrasia tuna wajibu wa kukubali kutofautiana hata pale ambapo tofauti hizo zinapingana na maslahi na matumaini yetu.

Kama ni upungufu wa Kafulila basi ni hulka ya kung'ang'ania na kusimamia misimamo na mitazamo yake bila ya kujali athari zake kwake ama kwa kundi lake lakini sio hili la TAMAA ambalo wengi humu wanajaribu kumvika. Ni wazi hulka hii ya kafulila wengi wetu tumepitia huko lakini ni hatua muhimu katika makuzi ya kila mtu anayeamini katika wito wa kazi za kisiasa na kiungozi. RADICAL stands ni muhimu katika kila kundi ama kizazi kama ilivyo kwa PRAGMATIC stands....

Kafulila umekosea kuondoka CHADEMA lakini naamini huko ulikoenda utaendelea kuwa na misimamo imara ingawa unahitaji kuthamini umuhimu wa mawazo ya wengine, hiyo ni hatua moja muhimu ya sio tu kuwa kiongozi bora na mwanasiasa mahiri bali pia kuwa MWANADEMOKRASIA wa dhati....

Nina uhakika huko NCCR mtaelewana sana na Comrade Bahati Tweve na Comrade Kahangwa....

omarilyas
 
aisee mambo jambo, tusianze kutukanana humu samahani sana, hata kama ni mchanga sana humu lakini habari zipo nyingi mitaani na kichwa kimekomaa sana, mmm nahisi unajingine. humu uwe umeingia leo au jana wote ni great thinkers and we dare talk openly, kama umekwazika kajinyonge basi

Remmy
Mambo.Nimekumiss vipi hujambo lakini?
 
jamaa inasemekana ni swahiba mkubwa wa Zitto hivyo ana access naye wakati woowte atakapo kuliko mtu mwingine yeyote ndani ya CHADEMA hivyo ninaamini atakuwa alimshirikisha Zitto kabla ya kufanya uamuzi.

Na pia ni very independent minded.....

omarilyas
 
Sasa katika kuhama kutoka katika chama chenye umaarufu zaidi na kuingia katika chama kilichofifia na kuyamaliza katika chama chenye umaarufu ili APEWE ubungo, ni ipi dalili ya kupenda madaraka ama maslahi binafsi?

Wandungu tuache unazi ama kile ninachoita UKADA POFU. Kafulila kafanya makosa kisiasa ya kuondoka CHADEMA kwa namna na wakati huu. Lakini bado ana haki ya kupimwa kwa vigezo vya mtizamo wake mwenyewe na sio hizi siasa za maji chafu tunazoendeleza hapa dhidi yake. Kama wapenda demokrasia ama wanademokrasia tuna wajibu wa kukubali kutofautiana hata pale ambapo tofauti hizo zinapingana na maslahi na matumaini yetu.

Kama ni upungufu wa Kafulila basi ni hulka ya kung'ang'ania na kusimamia misimamo na mitazamo yake bila ya kujali athari zake kwake ama kwa kundi lake lakini sio hili la TAMAA ambalo wengi humu wanajaribu kumvika. Ni wazi hulka hii ya kafulila wengi wetu tumepitia huko lakini ni hatua muhimu katika makuzi ya kila mtu anayeamini katika wito wa kazi za kisiasa na kiungozi. RADICAL stands ni muhimu katika kila kundi ama kizazi kama ilivyo kwa PRAGMATIC stands....

Kafulila umekosea kuondoka CHADEMA lakini naamini huko ulikoenda utaendelea kuwa na misimamo imara ingawa unahitaji kuthamini umuhimu wa mawazo ya wengine, hiyo ni hatua moja muhimu ya sio tu kuwa kiongozi bora na mwanasiasa mahiri bali pia kuwa MWANADEMOKRASIA wa dhati....

Nina uhakika huko NCCR mtaelewana sana na Comrade Bahati Tweve na Comrade Kahangwa....

omarilyas

Omarilyas.
Kwa jinsi ninavyomfahamu Kafulila sijawahi kumuona akiwa na misimamo imara kama unavyodai,labda misimamo ya kubishana na ushabiki hayo anayo.Hayo mengine nakubaliana na wewe. Kumwambia kwamba Kafulila amekosea kuhama CHADEMA pia sio sahihi,yeye mwenyewe ameshafanya mahesabu na ameona yuko sahihi wewe ni nani mpaka uone amekosea?Kila mtu ana haki ya kujichagulia chama chochote anachokitaka kwasababu zake anazozijua yeye.
 
Wakuu,
Michango iliyokaa kimatusi na kihasirahasira haitasaidia. Ulizeni kwanza jimbo la Kigoma kusini limekaaje kisiasa, ndipo mtagundua kwa nini Kafulila kaenda NCCR na si kwingine. Ukweli ni kwamba CHADEMA ilimkalia vibaya, ilikuwa hana budi kuondoka huko, sasa wapi aende... ndipo akazingatia hali ya kisiasa jimboni kwake na ushauri alioupata kwa wale wazee wa kigoma, lengo lake ni kuingia bungeni mwakani. Wakuu, yatosha mlivyomtukana Kafulila, yatosha mlivyoidharau NCCR... eti chama cha habari maelezo! Kama kuna chama kimestahimili mengi basi ni hiki, ni chama pekee kinachoendelea kuwepo bila nguvu za fedha bali moyo wa wanachama wake, na huo ndio uanachama wa kweli, kwingine bila hela mbona watu watakimbia tu. Kule CCM, CHADEMA, na CUF, tujiulize ni wangapi watakaa kama hela itakauka huko. Hongera Kafulila kwa uamuzi wako uliosoma mazingira, hongera NCCR kwa ustahimilivu, inshallah siku moja mtaimarika zaidi.

Kwahiyo wewe ni mwanachama NCCR!!! Pole sana mwenzangu, mimi sina chama.
 
Politics is the game of capitalizing one your oponents mistakes, kwa kutumia makosa yao, wewe unafunga magoli yako.Wako wanasiasa ma oportunists wao wanatafuta opportunities, akiona huku hakuna oportunities, anarukia kule, kama alivyosema Mzee Mwanakijiji mahali, usione kipepeo anatanga tanga kwenye maua ukadhani anapenda maua, kumbe anachofuata huko ni asali.Kwa kijana huyu, NCCR ndio mahali pekee penye oportunity anayoitafuta, CCM asingeipata, japo naamini Chadema alikuwa anasimama better chances kuliko huko alikotua.Kwa Chadema, egemeo la kijana huyu lilikuwa Zitto na ni kwa mtandao wa Zitto, angelitwa hilo jimbo huko Kigoma kiulaini kama kumsukuma mlevi. Naamini Zitto angekuwepo, kijana asingehama Chadema.NCCR Kigoma ina nguvu za mtandao wa Sam Ruhuza, hivyo kijana anahama mtandao wa Zitto kujiunga na wa Sam, swali ni jee, ana uwezo wa mass mobilization ya kujiundia mtandao wake utakaompa merits za kusimama nae 2010 dhidi ya CCM? au anategemea atajimegea pande lake Chadema kwenda kuiimarisha NCCR?.Mpeni nafasi aprove his guts.Kama anasoma humu ni muhimu akizingatiaKafulila don't talk dirty kuhusu Chadema, concetrate na hapo ulipo ili uweze kusonga mbele kwa matumaini ya kupanda juu bila kuitelekeza ngazi uliyoitumia kupandia, ili utakapowadia wakati wa kushuka, utaitumia ngazi hiyo hiyo na huko chini utawakuta wale wale waliokupandisha mpaka kupokelewa na James Mbatia mwenyewe.

CHADEMA wakijipanga vizuri wakaweka candidate mzuri tu hilo jimbo hata CHADEMA watachukua, siyo ohoo Zitto ndo awe tegemeo, mbona Biharamulo, Busanda viongozi wote wa CHADEMA pamoja na Zitto walikuwepo?? Uchaguzi wa TZ ni mbinu, hata upige kambi mwaka mzima, unaweza kutoka patupu.
 
CHADEMA wakijipanga vizuri wakaweka candidate mzuri tu hilo jimbo hata CHADEMA watachukua, siyo ohoo Zitto ndo awe tegemeo, mbona Biharamulo, Busanda viongozi wote wa CHADEMA pamoja na Zitto walikuwepo?? Uchaguzi wa TZ ni mbinu, hata upige kambi mwaka mzima, unaweza kutoka patupu.
Zitto ana influence kubwa kigoma utake usitake habari ndo hiyo kijana.
Kam kafulila hakutendewa haki na ustaarabu na uongozi wa chadema kwanini asihame, ilifikia mpaka kuitwa sisimizi, je hiyo ni haki?inamaana hata hawakua na shukurani alipokua akiwafanyia kazi.
 
Zitto ana influence kubwa kigoma utake usitake habari ndo hiyo kijana.
Kam kafulila hakutendewa haki na ustaarabu na uongozi wa chadema kwanini asihame, ilifikia mpaka kuitwa sisimizi, je hiyo ni haki?inamaana hata hawakua na shukurani alipokua akiwafanyia kazi.

Kwani alikuwa anafanya kazi ili apewe shukrani?
 
Me naona jamaa alichemka kumuita mwenzake sisimizi, lakini najua kwaajili kasema Dr Slaa watu mtakaa kimya.Hapo ndipo sometimes naona kuna Bias miongoni mwetu katika kuchangia mada.
 
haya Basi kumuita jamaa sisimizi ni sawa?,Ubinadam upo hapo mkuu?

Mimi mwanzoni nilitaka kumuita Kafulila kuwa ni tembo (yaani - vita vya tembo) lakini baadaye nikagundua kuwa kafulila hajafikia hata size ya kondoo (kama kwenye vita vya kondoo),
 
Back
Top Bottom