Remmy
JF-Expert Member
- Jun 9, 2009
- 4,701
- 1,799
David Kafulila kuhamia NCCR
Kuna nyepesinyepesi kuwa yule sisimizi wa CHADEMA kuhamia NCCR MAGEUZi kama alivyodai yeye kuwa anahitaji kuleta mabadiliko ya kisiasa nchini.
Yule aliyekuwa Ofisa Habari wa Chadema, amekaribishwa muda mfupi uliopita ndani ya chama kingine cha upinzani cha NCCR-Mageuzi.
David Kafulila alikikimbia Chadema mapema wiki hii inayomalizika leo na kuwatuhumu viongozi wa chama hicho, Freeman Achikaeli Mbowe na katibu wake mkuu, Dk. Wilbroad Slaa, amepokewa na Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia jijini Dar es Salaam na kupewa kadi ya uanachama.
Kafulila amesema kuwa ameamua kujiunga na NCCR kwa kuwa huko anaamini ataendeleza jitihada zake za kuimarisha upinzani Tanzania, ingawapia nadhani anajipanga ili kutimiza ndoto yake ya kuwania ubunge Kigoma Kusini baada ya kunusa kuwa Chadema wasingempitisha.
Kafulila, hadi anapewa kadi hiyo, ni mwanachama wa kawaida tu, ingawa kuna tetesi kuwa ameandaliwa cheo fulani hapo makao makuu, hasa cha habari ili kuanza kazi ya 'kuipaisha' NCCR mbele ya umma wa Watanzania.
Tusubiri tuone mwisho wake