boma2000
JF-Expert Member
- Oct 18, 2009
- 3,280
- 310
Jamani leo asubuhi nimekutana na David Jairo, kilichonishangaza ni kumkuta anatumia gari la serikali Landcruiser V8 wakati nilijua ametolewa serikalini moja moja. nimeshindwa kuelewa sasa anatumia gari yetu, mafuta yetu, dereva wetu sisi watanzania walipa kodi ambao alitusaliti, anatumia kwa misingi gani hivi kapewa cheo gani cha siri huko serikalini ambako sisi watanzania ambao tunatakiwa kumiliki hiyo serikali hatuna SAUTI hata kiduchu mpaka wakati wa uchaguzi ndo tunaambiwa serikali ni yetu si kama inamilikiwa na watu wachache wenye jeuri na kiburi na wanatufanya tuzidi kuwa maskini siku baada ya siku.