Harvey Specter
Member
- Jun 26, 2024
- 33
- 46
Huduma ya mabasi ya mwendokasi iliyotarajiwa kuanza leo Septemba Mosi, 2025 katika barabara ya Mbagala, imesogezwa mbele ikiwa ni sababu ya kutokamilika kwa miundombinu muhimu kama mageti janja na kituo cha kujazia gesi.
Akizungumza lna gazeti la Mwananchi leo Jumatatu, Septemba mosi 2025 , Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart), Dk Athuman Kihamia, amesema kuchelewa kuanza kwa huduma hiyo kunatokana na changamoto hizo, licha ya mabasi kuwa tayari yamewasili. "Mageti janja kwa ajili ya ukataji wa tiketi bado hayajafungwa na kituo cha kujazia gesi kilichopo kwenye karakana ya Mbagala nacho hakijakamilika" alisema Dk. Kihamia.
Ameahidi kutoa taarifa rasmi kuhusu maendeleo ya ujenzi huo tutaitoa baada ya wiki moja kutokea leo.
Ikumbukwe Mabasi hayo 151 yaliwasili katika karakana ya Mbagala Rangi Tatu tangu usiku wa Agosti 29, 2025.
Je wakati wanaahidi kuanza safari hizo siku ya leo Septemba Mosi, 2025 hawakua na taarifa kamili za maendeleo ya miundo mbinu hiyo, ndio wameshtukizwa leo???
Akizungumza lna gazeti la Mwananchi leo Jumatatu, Septemba mosi 2025 , Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart), Dk Athuman Kihamia, amesema kuchelewa kuanza kwa huduma hiyo kunatokana na changamoto hizo, licha ya mabasi kuwa tayari yamewasili. "Mageti janja kwa ajili ya ukataji wa tiketi bado hayajafungwa na kituo cha kujazia gesi kilichopo kwenye karakana ya Mbagala nacho hakijakamilika" alisema Dk. Kihamia.
Ameahidi kutoa taarifa rasmi kuhusu maendeleo ya ujenzi huo tutaitoa baada ya wiki moja kutokea leo.
Ikumbukwe Mabasi hayo 151 yaliwasili katika karakana ya Mbagala Rangi Tatu tangu usiku wa Agosti 29, 2025.
Je wakati wanaahidi kuanza safari hizo siku ya leo Septemba Mosi, 2025 hawakua na taarifa kamili za maendeleo ya miundo mbinu hiyo, ndio wameshtukizwa leo???