Darasa kwa Kubenea na Wabunge wengine

Darasa kwa Kubenea na Wabunge wengine

mwongozo junior

Senior Member
Joined
Jul 28, 2015
Posts
180
Reaction score
65
Tuna mihimili mikuu mitatu kiuongozi kwa mujibu wa Katiba ya JMT. Utawala, Mahakama na Bunge.

Muh. Rais ndiye kiongozi mkuu wa utawala. Vilevile ndiye msimamizi mkuu wa mahakama na bunge. Jaji mkuu na Spika wako chini yake. Kimkoa na kiwilaya, Rais anawakilishwa na Wakuu wa Mikoa pamoja na Wakuu wa Wilaya.

Wakuu Wa wilaya, wakuu Wa mikoa hata ulaya na marekani wapo. Japo majina (title) yanatofautiana, lkn majukumu yao ni kumuwakilisha rais. wabunge kote duniani siyo viongozi Wa kiutendaji (executive).

Nchi zote zina executive, judiciary na legislature. Katika kila nchi executive (Rais na wasaidizi wake) ndiyo watekelezaji Wa sheria kiuongozi. Marekani magavana (tuwaite wakuu Wa mikoa na wilaya) wana nguvu sana kiutendaji.

Licha ya Kubenea kuwa mbunge alipaswa kumheshimu Mkuu Wa wilaya Bila kubishana nae hadharani au kumtukana. Alimuita mhuni na kibaka hadharani.

Makonda ili kuhifadhi ushahidi, aliamua kuteka video camera ya star TV ili ushahidi Wa matusi aliotukanwa usifutwe.

Jiweke katika nafasi ya Makonda. Rais Wa wilaya kutukanwa hadharani. Ikumbukwe kuwa Makonda alikua ameahidi kumpeleka waziri kiwandani Leo.

Kiprotokali baada ya Makonda kuongea na wafanyakazi, Kubenea hakua na haki ya kutaka kuongea baada ya DC. DC aliogopa kuwa maneno ya Kubenea yanaweza chafua hali ya hewa ambayo ilikua imetulia.

Makonda kwa nafasi yake ni mwenyekiti wa ulinzi na usalama katika wilaya anayoiongoza. Pangetokea vifo pale kiwandani angelaumiwa Mkuu Wa wilaya. Kubenea anapaswa kulijua hili.

Tabia ya kijeuri ya Kubenea aliionesha siku ya kufungua bunge alipomuomba Kange Lugola kufuta maneno yake. Alitumia lugha ya kibabe sana bila ulazima. Siku hiyo ndiyo nilibaini kuwa Kubenea ana uwezo mdogo wa kujenga hoja. Ni nadra kwake kutumia busara na hekima. Kubenea ajue kuwa kinga anayo bungeni (legislature) siyo uraiani (executive) kwa akina Makonda.

Kubenea alikua na dhamira ya kuwatetea wafanyakazi Wa kiwanda lakini njia aliyoitumia ya jazba na ubabe haikuwa sahihi. Mwl Nyerere aliwahi kuwaambia wanafunzi Wa UDSM walioandamana kuwa "The objectives you have are genuine but the methods you used to achieve your objectives are improper, thus, tarnishing everything".


Tuweke siasa kando. Tuseme ukweli. Katiba ya 1977 ndiyo ituongoze hata kama INA mapungufu. Inawatambua wakuu wa mikoa na wilaya. Wamepewa madaraka kumuweka mtu ndani iwapo hali iliyopo itawalazimu kufanya hivyo. Sheria ni msumeno.
 
Makonda ... awe Kiranja Mkuu Wa Kukimbiza Mwenge wa Uhuru toka DSM hadi Njombe. Kazi ya Ukuu Wa Wilaya haimfai.
 
Elimu.... Elimu.... Elimu...!!!!!!!!!!!!! (In Lowasa's voice)
 
kubenea amepata somo in a hard way ! alidhani akiwa mbunge basi ndio atakuwa juu ya sheria ,au ataitisha vikao anavyotaka yeye ,,, mi natamani apate kifungo hata cha mwezi liwe somo kwa wabunge wote wapya ...
 
Wabunge wanapaswa kuheshimu muhimili mingine ya na sio kujiona wao ndio kila kitu, vurugu zao ni ndani ya bunge huku nje wafate sheria na taratoibu za nchi
 
Hata kama Makonda kufanya kosa gani la kiutendaji, tuweke unazi pembeni, watu wazima tena viongozi kuitana mhuni au kibaka ni " below the belt".
 
Umeandika point mkuu, lazima ifike mahali serikali ieshimiwe sasa kuna kenge wanataka mkuu wa wilaya ajichekeshe tu baada ya kutukanwa hadharani.

Hiyo haikubariki hata kama Kubenea anadhani ilikuwa ni haki yake lakini mipaka ya mkuu wa wilaya aiheshimu na akikaidi na kutoa Lugha za kudharirisha atafikishwa mahakamani tu.
 
Elimu unayotoa kwa watu wenye mahaba ngumu kuelewa. Mahaba in hatari Chongo anaita kengeza. Ukweli unabaki palepale serikali ndiyo wasimamizi Wa utekelezaji Wa sheria. Si kazi ya mbunge kutatua migogoro ya kazi kazi hiyo ni ya vyama kisekta vikisimamiwa kisheria na Serikali.

Kubenea Jana tumemsikia akimpa masharti muwekezaji, ati ili awatulize wagomaji akubali ungezeko la asilimia 40 Kwa vigezo gani? Si kazi take, angeshia kusikiliza kilio cha wafanyakazi na kuwasilisha\shinikiza malalamiko yao sehemu zinazihusika. Asubiri kuchaguliwa kwenye kamati za bunge apate nafasi ya kuikagua na kuihoji serikali.
 
Kwahiyo wewe kilaza hii ---- ndio unaita darasa?

Makonda ni kibaka kwasababu ameiba sana simu za wajumbe wa bunge la katiba!!

Itakua busara ushahidi unaoonesha kuwa ni kibaka mpelekee kubenea ukamsaidie. Ameshitakuwa kwa kumtukana Mkuu Wa wilaya kuwa ni kibaka huku akiwa kazini
 
Yaani wewe ni kilaza hasa, halafu usijekuta hata una cheo mahali na unaongoza watu
 
Kubenea Kafanya Kosa na Makonda kafanya kosa.

Kosa la kubenea halikulazimaka/si la kimahakama bali la kiofisi zaidi sio la kupelekwa mahakamani ... ingawa linabakia kuwa kosa. Na hivo ndio alivokosea Makonda kijana aliyekosa nidhamu na kumpiga JAJI.
 
hahaha! ati kubenea alimpa masharti muwekezaji..aongeze mshahara ..??! hivi huyu jamaa anajua mipaka yake kweli ?!!

CDM wabunge wenu wapya muwape semina elekezi ... yeye si executive ! anachotakiwa na kusikiliza shida za wananchi wake na kupeleka malalamiko sehemu husika yeye ni mjumbe wa wananchi , mtumwa , kazi yake ni kutumwa na wananchi wake na kupeleka shida zao huko juu...

 
Kuna wakuu wa wilaya ambao mkuu wa nchi anatakiwa kuwabadilisha upesi sana ili kulinda heshima ya serikali yake na mmoja wao ni huyo Makonda wa Kinondoni. Toka ameteuliwa imekuwa ni shida tu kila siku kuwasweka watu lupango!!
 
...........
Wakuu Wa wilaya, wakuu Wa mikoa hata ulaya na marekani wapo. wabunge kote duniani siyo viongozi Wa kiutendaji (executive).
[/QUOTE] ........

Hili neno marekani kwani si sawa na USA?!! Au akili yangu inaanza kuzeeka, maana mleta uzi unasema hujasema hicho kitu.
 
Back
Top Bottom