Ubaya Ubwela
JF-Expert Member
- Jul 24, 2024
- 2,711
- 6,474
Wananchi wa vijiji vya Tsawa na Tipri kata ya Gehandu wilaya ya Mbulu mkoani Manyara wamefurahishwa na kukamilika kwa daraja lililojengwa na kwamba baada ya kuteseka kwa miaka mingi na kusababisha kuwa na changamoto ya kukosa kivuko na kusimamisha kuendelea na shughuli za kiuchumi nyakati za mvua.
Daraja hilo ambalo limegharimu Milioni 158 na lenye uwezo wa kubeba Tani 2.4 na linatarajiwa kudumu kwa miaka 70 limezinduliwa na mkimbiza Mwenge kitaifa Ali Ussi Leo Julai 16, ambapo daraja hilo linatajwa litasaidia wanafunzi wa maeneo hayo kupita kwenda shuleni nyakati zote pamoja na wagonjwa kufikishwa kwenye huduma za Afya kwa wakati.
Daraja hilo ambalo limegharimu Milioni 158 na lenye uwezo wa kubeba Tani 2.4 na linatarajiwa kudumu kwa miaka 70 limezinduliwa na mkimbiza Mwenge kitaifa Ali Ussi Leo Julai 16, ambapo daraja hilo linatajwa litasaidia wanafunzi wa maeneo hayo kupita kwenda shuleni nyakati zote pamoja na wagonjwa kufikishwa kwenye huduma za Afya kwa wakati.