Daraja la Mfugale linatengeneza foleni

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Uwekezaji wa thamani kubwa kwenye miundombinu ya daraja la juu la Mfugale jijini Ilala mkoani DSM umepoteza dhima yake na thamani ya fedha iliyowekezwa pale kutokana na kwamba mradi umepunguza foleni kwa asilimia ndogo tu ambayo haiwezi kuakisika kwenye uhalisia wa maisha ya watu.

Mradi ulilenga kuwahisha viongozi kwenda na kutoka uwanja wa ndege. Barabara ya Mandela tokea Ubungo inaliingizia taifa fedha nyingi kuliko ya Nyerere kipande cha kutokea mjini hadi darajani.

Kosa hilo limerudiwa tena kwenye daraja la juu la makutano ya Nyerere na Kawawa eneo la Chang'ombe, daraja limelenga kusafirisha viongozi kwenda uwanja wa ndege. Huenda miradi kama hiyo kwa maeneo yaliyosalia ya Morocco, Mwenge, Magomeni na Uhasibu ujenzi ukafanyika kisiasa.

Kuna janga la foleni kwenye barabara ya Mandela hususan Mwananchi kuja Mfugale na Uhasibu kuja Mfugale.

Nini kifanyike Mfugale:

1. Nadhani makosa yasahihishwe kwa kuondoa taa za kuongozea magari chini ya daraja na kujenga mzunguko (roundabout) ili kupunguza foleni zinazosababishwa na taa kupitisha magari kwa zamu.

2. Ijengwe barabara ya njia mbili ya chini ya ardhi baada ya kupita njia ya reli kuvuka daraja hadi kuibukia usawa wa TBC ili gari za Ubungo - Bandarini zipite chini kwa chini.

3. Kama namba mbili hapo juu haiwezekani basi zijengwe barabara double za pembezoni mwa daraja ili kwamba gari za kwenda kulia na kushoto kwa daraja zisilazimike kupindukia katikati ya barabara ya chini ya daraja (kwenye taa) na kwamba barabara hiyo ya chini itabaki maalum kwa gari za Bandarini, Temeke nk na pia gari za Ubungo nk.

Tukizingatia ushauri huu hakutakuwa na haja ya kujenga bypass (mchepuko) ya kuondoa foleni ya Buguruni mataa.

Tujadili.

 
Wakati tunajadili haya mambo ya ma fly over kwenye miaka ya 2006 huko nilikuja na wazo la kupitisha underground lane. Lakini niliwaonya wataalamu kuwa Dar ni jiji la mafuriko. Endapo watapitisha option ya underground lane basi waje na drainage system ya uhakika.

Ndio maana unaona mpaka sasa option ya underground lane haijatekelezwa kwa kuhofia mafuriko.
 
Kwamba sisi tunaenda kkoo-gongo la mbali bado tunatumia masaa mawili kwenye taa tazara!!?..fikiria babu
 
Wakati tunajadili haya mambo ya ma fly over kwenye miaka ya 2006 huko nilikuja na wazo la kupitisha underground lane. Lakini niliwaonya wataalamu kuwa Dar ni jiji la mafuriko. Endapo watapitisha option ya underground lane basi waje na drainage system ya uhakika.
Ndio maana unaona mpaka sasa option ya underground lane haijatekelezwa kwa kuhofia mafuriko.
Mkuu.

Uliona mbali miaka hiyooo...
 
Kwamba sisi tunaenda kkoo-gongo la mbali bado tunatumia masaa mawili kwenye taa tazara!!?..fikiria babu
Mandela inasafirisha makontena mangapi kwa siku kulinganisha na k'koo - gongo la mbali? Mnaingiza shilingi ngapi hizo za daladala na magari ya makontena yanaingiza shilingi ngapi kwa taifa rafiki yangu?

Uchumi wa usafirishaji (transport economy) unatakiwa uamue haya mambo badala ya siasa.
 
Mandela inasafirisha makontena mangapi kwa siku kulinganisha na k'koo - gongo la mbali? Mnaingiza shilingi ngapi hizo za daladala na magari ya makontena yanaingiza shilingi ngapi rafiki yangu?
Mwigulu akisema uchumi ujadiliwe na wachumi mnabisha...hao watu wa kwenye daladala wanaenda harusini!?..unajua foleni zinapoteza kiasi gani kwenye uchumi!?
 
Uwekezaji wa thamani kubwa kwenye miundombinu ya daraja la juu la Mfugale jijini Ilala mkoani DSM umepoteza dhima yake na thamani ya fedha iliyowekezwa pale kutokana na kwamba mradi umepunguza foleni kwa asilimia ndogo tu ambayo haiwezi kuakisika kwenye uhalisia wa maisha ya watu.

Mradi ulilenga kuwahisha viongozi kwenda na kutoka uwanja wa ndege. Barabara ya Mandela tokea Ubungo inaliingizia taifa fedha nyingi kuliko ya Nyerere kipande cha kutokea mjini hadi darajani.

Kosa hilo limerudiwa tena kwenye daraja la juu la makutano ya Nyerere na Kawawa eneo la Chang'ombe, daraja limelenga kusafirisha viongozi kwenda uwanja wa ndege. Huenda miradi kama hiyo kwa maeneo yaliyosalia ya Morocco, Mwenge, Magomeni na Uhasibu ujenzi ukafanyika kisiasa.

Kuna janga la foleni kwenye barabara ya Mandela hususan Mwananchi kuja Mfugale na Uhasibu kuja Mfugale.

Nini kifanyike Mfugale:

1. Nadhani makosa yasahihishwe kwa kuondoa taa za kuongozea magari chini ya daraja na kujenga mzunguko (roundabout) ili kupunguza foleni zinazosababishwa na taa kupitisha magari kwa zamu.

2. Ijengwe barabara ya njia mbili ya chini ya ardhi baada ya kupita njia ya reli kuvuka daraja hadi kuibukia usawa wa TBC ili gari za Ubungo - Bandarini zipite chini kwa chini.

3. Kama namba mbili hapo juu haiwezekani basi zijengwe barabara double za pembezoni mwa daraja ili kwamba gari za kwenda kulia na kushoto kwa daraja zisilazimike kupindukia katikati ya barabara ya chini ya daraja (kwenye taa) na kwamba barabara hiyo ya chini itabaki maalum kwa gari za Bandarini, Temeke nk na pia gari za Ubungo nk.

Tukizingatia ushauri huu hakutakuwa na haja ya kujenga bypass (mchepuko) ya kuondoa foleni ya Buguruni mataa.

Tujadili.

Wapo "wataalamu" wao humu wanasubiri input ya mitandaoni wafanyie kazi kama kawaida yao.
 
Uwekezaji wa thamani kubwa kwenye miundombinu ya daraja la juu la Mfugale jijini Ilala mkoani DSM umepoteza dhima yake na thamani ya fedha iliyowekezwa pale kutokana na kwamba mradi umepunguza foleni kwa asilimia ndogo tu ambayo haiwezi kuakisika kwenye uhalisia wa maisha ya watu.

Mradi ulilenga kuwahisha viongozi kwenda na kutoka uwanja wa ndege. Barabara ya Mandela tokea Ubungo inaliingizia taifa fedha nyingi kuliko ya Nyerere kipande cha kutokea mjini hadi darajani.

Kosa hilo limerudiwa tena kwenye daraja la juu la makutano ya Nyerere na Kawawa eneo la Chang'ombe, daraja limelenga kusafirisha viongozi kwenda uwanja wa ndege. Huenda miradi kama hiyo kwa maeneo yaliyosalia ya Morocco, Mwenge, Magomeni na Uhasibu ujenzi ukafanyika kisiasa.

Kuna janga la foleni kwenye barabara ya Mandela hususan Mwananchi kuja Mfugale na Uhasibu kuja Mfugale.

Nini kifanyike Mfugale:

1. Nadhani makosa yasahihishwe kwa kuondoa taa za kuongozea magari chini ya daraja na kujenga mzunguko (roundabout) ili kupunguza foleni zinazosababishwa na taa kupitisha magari kwa zamu.

2. Ijengwe barabara ya njia mbili ya chini ya ardhi baada ya kupita njia ya reli kuvuka daraja hadi kuibukia usawa wa TBC ili gari za Ubungo - Bandarini zipite chini kwa chini.

3. Kama namba mbili hapo juu haiwezekani basi zijengwe barabara double za pembezoni mwa daraja ili kwamba gari za kwenda kulia na kushoto kwa daraja zisilazimike kupindukia katikati ya barabara ya chini ya daraja (kwenye taa) na kwamba barabara hiyo ya chini itabaki maalum kwa gari za Bandarini, Temeke nk na pia gari za Ubungo nk.

Tukizingatia ushauri huu hakutakuwa na haja ya kujenga bypass (mchepuko) ya kuondoa foleni ya Buguruni mataa.

Tujadili.


Bado yapo mengi mtayaona kuhusu miradi ya Magufuli, mingi ilifanywa bila kufikiri vizuri na kwa lengo la kujipatia sifa binafsi na of course kupiga hela nyingi, na amefanikiwa sana kwa hili lakini watanzania ndio kwanza baadhi wanaanza kufunguka akili zao. Watanzania jiandaeni kuona madudu ya kutisha!
 
Back
Top Bottom