masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 18,196
- 13,837
Daraja la Makofia pale mto Ruvu lina matatizo.
Mvua za majuzi zimedhihirisha wasi wasi wangu juu ya usanifu wa daraja hili.
Lakini lazima niweke wazi, sitoi maoni kwa kulaumu , bali kwa nia ya kuweka tahadhari ili hatua zichukuliwe kuokoa hasara dhahiri inayoweza kutokea.
Kwa karibu miaka mitatu au minne mfululizo barabara ya Msata~Bagamoyo imebidi kufungwa kupisha mafuriko ya mto Ruvu.
Mafuriko hayo huwa ni makubwa, kiasi kina kinaongezeka kwa kiasi cha mita tatu hadi tano juu ya wastani uliozoeleka.
Na kama mafuriko yatakuwa wakati wa bamvua, yaani bahari kujaa, halinyaweza kuwa mbaya zaidi.
Nimeshuhudia na si mara moja bahari ikigeuza mkondo wa maji pale daraja la chuma linalokatiza mto Ruvu!
Na hapo ndo wasi wasi wangu.
Najiuliza je, usanifu wa barabara umetilia maanani haya yote?
Barabara inayopita bonde hili la Ruvu inaweza kuwa kama kizuio kikubwa cha mto hivyo kutengeneza bwawa, na bwawa hili likijaa na maji.kupita juu ya barabara, huo unakuwa mwisho wa barabara mpya ya Msata~Bagamoyo.
Pengine ni wasi wasi wangu tu, wataalam wa ujenzi TANROADS hebu tondoleeni huu wasi wasi.
Mvua za majuzi zimedhihirisha wasi wasi wangu juu ya usanifu wa daraja hili.
Lakini lazima niweke wazi, sitoi maoni kwa kulaumu , bali kwa nia ya kuweka tahadhari ili hatua zichukuliwe kuokoa hasara dhahiri inayoweza kutokea.
Kwa karibu miaka mitatu au minne mfululizo barabara ya Msata~Bagamoyo imebidi kufungwa kupisha mafuriko ya mto Ruvu.
Mafuriko hayo huwa ni makubwa, kiasi kina kinaongezeka kwa kiasi cha mita tatu hadi tano juu ya wastani uliozoeleka.
Na kama mafuriko yatakuwa wakati wa bamvua, yaani bahari kujaa, halinyaweza kuwa mbaya zaidi.
Nimeshuhudia na si mara moja bahari ikigeuza mkondo wa maji pale daraja la chuma linalokatiza mto Ruvu!
Na hapo ndo wasi wasi wangu.
Najiuliza je, usanifu wa barabara umetilia maanani haya yote?
Barabara inayopita bonde hili la Ruvu inaweza kuwa kama kizuio kikubwa cha mto hivyo kutengeneza bwawa, na bwawa hili likijaa na maji.kupita juu ya barabara, huo unakuwa mwisho wa barabara mpya ya Msata~Bagamoyo.
Pengine ni wasi wasi wangu tu, wataalam wa ujenzi TANROADS hebu tondoleeni huu wasi wasi.