samora10
JF-Expert Member
- Jul 21, 2010
- 7,594
- 4,798
Natumaini mnaendelea na weekend yenu kwa utulivu huku tukidigest majipu yaliyotumbuliwa week nzima.
Nataka tu kujua maendeleo ya lile daraja la kigamboni, limefikia wapi? Nakumbuka Mh Rais wakati huo akiwa waziri wa ujenzi aliagiza kandarasi ahakikishe linaanza kupitika september 2015 ila mpaka leo naona kimya.. Kunani kinaendelea? Ujenzi umekwama? Na kama haujakwama nini basi kinasubiriwa ili daraja liweze kuanza kutumika?
Binafsi ni mdau huko kigamboni na nina kiplot changu mitaa ya kibada nilianza msingi ila shuruba za pale feri kuvuka na gari zilinishinda nikaamua nisubiri kwanza daraja lifungiliwe ili niweze kumalizia kibanda changu na kuachana na maisha ya kupanga.
Basi si vibaya kama kuna mtu ana updates akaniwekea hapa kwani ni siku mingi kidogo na hatujui nini kinaendelea, ukipata kapicha ukatupia sio mbaya pia..
Wenu mdau.. Kigamboni resident to be.
Nataka tu kujua maendeleo ya lile daraja la kigamboni, limefikia wapi? Nakumbuka Mh Rais wakati huo akiwa waziri wa ujenzi aliagiza kandarasi ahakikishe linaanza kupitika september 2015 ila mpaka leo naona kimya.. Kunani kinaendelea? Ujenzi umekwama? Na kama haujakwama nini basi kinasubiriwa ili daraja liweze kuanza kutumika?
Binafsi ni mdau huko kigamboni na nina kiplot changu mitaa ya kibada nilianza msingi ila shuruba za pale feri kuvuka na gari zilinishinda nikaamua nisubiri kwanza daraja lifungiliwe ili niweze kumalizia kibanda changu na kuachana na maisha ya kupanga.
Basi si vibaya kama kuna mtu ana updates akaniwekea hapa kwani ni siku mingi kidogo na hatujui nini kinaendelea, ukipata kapicha ukatupia sio mbaya pia..
Wenu mdau.. Kigamboni resident to be.